|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
In the News Room |
Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Kilimo, Mifugo na Maji inakamilisha ziara yake : Mhe. Gideon Cheyo (MB) Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo Mifugo na Maji Habari zaidi |  | | kwa kutembelea mashamba ya ngano ya West Kilimanjaro na pia katika Bwawa la Nyumba ya Mungu kabla ya Wajumbe hao kurejea jijini Dar es salaam.
Katika zira hiyo wajumbe walipata fursa ya kuona shughuli mbalimbali katika Miradi ya Kilimo na Umwagiliaji. Miongoni mwa miradi iliyotembelewa ni pamoja na Skimu ya umwagiliaji maji ya Mto wa Mbu. Aidha, wajumbe hao waliwatembelea wakulima wa maua ambayo yanasafirishwa nje ya nchi.
Kabla ya ziara hiyo Wajumbe hao walipata nafasi ya kupitia na kuijadili taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika.
|
| Ombi Letu ni Matrekta – Mhe. Waziri Mkuu : Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Waziri wa Kilimo wa China, Bw. Niu Dun Habari zaidi |  | | Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda amemweleza Naibu Waziri wa Kilimo na Uvuvi wa Jamhuri ya Watu wa China, Bw. Niu Dun kuwa Tanzania inahitaji msaada zaidi wa matrekta madogo na makubwa ili iweze kupiga hatua katika Kilimo cha kisasa na chenye tija.
Maelezo hayo ameyatoa kwa Naibu Waziri huyo kutoka China baada ya kumtembelea Ofisini kwake akiwa na ujumbe wa watu 12 akiwemo Balozi wa China nchini, Bw. Lik Xnsheng.
Awali kabla ya kutoa ombi hilo Waziri Mkuu alimpongeza Waziri huyo wa Serikali ya Watu wa China kwa kukubali kusaini mkataba wa ushirikiano katika biashara ya uvuvi wa samaki katika kina kirefu cha bahari ambapo Tanzania imekuwa ikiibiwa rasilimali hiyo muhimu kwa miaka kadhaa.
Kabla ya kwenda Ofisi ya Waziri Mkuu, Naibu Waziri huyo alitembelea Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika na kupokelewa na Naibu Waziri Mhe. Dkt. Mathayo David Mathayo.
Katika Mkutano huo Waziri Mathayo aliainisha maeneo ambayo yanahitaji ushirikiano zaidi katika kuyatekeleza kwa pamoja kati ya Tanzania na China kwa lengo la kuongeza ufanisi katika Sekta ya Kilimo.
|
| |
|
|
|
|
|
|
|
 |
|
|
|
|
 |
|
|
 |
|
|
 |
|
|
 |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
| Programes, Projects and other web pages |
|
 |
|
 |
|
 |
|
 |
|
 |
| |
 |
|
 |
|
 |
|
 |
|
 |
|
|
| Last update: 26 February, 2010 |