In the News Room
The Web Kilimo web
Home | Budget Speeches | Publications | Agricultural Statistics | Legislations and Regulations | Web Links
 

Wizara Kushirikiana na Indonesia Kukuza Kilimo

Naibu Katibu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bi. Sophia Kaduma wa nne Kulia, akiwa  pamoja na Tume ya Ushirikiano wa Pamoja katika sekta ya kilimo.

 

Tume ya pamoja ya Ushirikiano katika sekta ya kilimo  ya Wizara ya Kilimo Chakula na ushirika imejadili maeneo ya kushirikina kwa awamu ya pili na serikali ya Indonesia  ili kuongeza tija na uzalishaji katika kilimo.

Akizungumza na tume kutoka pande zote mbili Tanzania na Indonesia Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Mama Sophia Kaduma alisema majadiliano hayo yanalenga kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya kilimo pamoja na upatikanaji wa masoko.

Mama Kaduma alisema ushirikiano baina ya nchi hizo mbili utahusisha katika kujenga uwezo wa wakulima, masuala ya utafiti pamoja na upatikanaji wa masoko ya mazao.

Katika kujenga uwezo Mama kaduma alisema Tanzania na Indonesia itashirikiana katika mafunzo ya Muda mfupi na mrefu pamoja na kubadilishana wakufunzi ambao wataenda kufundisha vyuo mbalimbali vilivyopo katika nchi hizo.

Katika mafunzo ya muda mfupi serikali ya Indonesia itafadhili  masomo ya  Uchumi Kilimo na kilimo cha bustani hasa katika maeneo  ya utafiti, usindikaji na mbegu.

 
Alifafanua kukuwa Indosesi itafadhili mafunzo kwa wakulima 15 chini ya mpango wa Ushirikiano wa nchi za kusini   ambapo wakulima 12 watatoka Tanzania Bara na watatu watatoka Tanzania Visiwani.

Aliongeza kuwa masoma hayo yataanza tarehe 1-9/07/1213 na Tanzania itagharamia nauli za washiriki wa program hiyo pamoja na pesa za kujikimu.

Kwa upande wa mafunzo ya muda mrefu katika kujenga uwezo, serikali ya Indonesia itatoa ufadhili kwa watu watatu  ambao watasoma shahada ya uzamili na uzamifu na mmoja  ambaye atasoma masomo  yalio chini ya shahada ya kwanza.

Pia alisema nchi hizo mbili zitashirikana katika mambo ya utafiti wa mazao hasa katika mazao ya pamba, mpunga na viungo mbalimbali.

Alifafanua kuwa utafiti huo utahusisha mambo ya GMO, majaribioa mashambani, uzalishaji wa mbegu bora, magonjwa, usindikaji na uimarishaji wa vituo vya utafiti.

Mama Kaduma alisema pian nchi hizo zimekubalia kushirikiana katika katika masoko kwa kubadilishana taarifa za masoko na taratibu mbalimblia ili kuboresha biashara ya bidhaa za kilimo kati ya nchi zote mbili.

Alifafaunua kuwa licha ya kushirikiana katika masoko pia Serikali ya Indonesia itashiriki katika maonesho ya kimataifa ya wafanya biashara yafanyika Dar es Salaam (Sabasaba) pamoja na maonesho ya wakulima ya Nane Nane.

Ushirikianao baina ya nchi hizo mbili unalenga kuongeza tija katika kilimo, kuongeza upatikanaji wa masoko, kuongeza uzalishaji wa mazao pamoja na kukuza kipato cha mkulima.

 

 

 

 

Mifumo ya Asili ya Kilimo Kuendelezwa Kuinua Kilimo

Mazao yaliyostawi vizuri yakionyesha mojawapo ya aina ya kilimo Asili cha Mseto

Wadau wa kilimo, sera, mazingira, utawala, na mashirika ya kimataifa, wametoa wito wa kubaini mifumo asili ya Kilimo kwa kutambua mchango katika uhakika wa chakula na kipato.

Wito huo ulitolewa katika warsha iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyojumuisha wadau hao ili kutathmini mchango wa mifumo asili ya kilimo na changamoto zilizopo ili kuiboresha na kiendeleza.

Ilibainika kuwa Tanzania ina mifumo mingi ya asili ya kilimo na mifugo ambayo imedumu kwa taribani zaidi ya miaka 100 hadi 700.

Katika kipindi hicho, mifumo mingi imekumbana na mabadiliko ya hali ya hewa lakini imekabili na kudumu, hii inaonyesha kuwa kuna vitu vingi vya kujifunza katika mifumo hiyo.

Aidha, wadau wamependekeza mifumo ya asili ya kilimo na ufugaji kuingizwa katika sera kati ya zilizopo ili ipate nguvu ya kusimamiwa na kuendelezwa hasa ikizingatiwa umuhimu wake katika kuimarisha usalama wa chakula na kipato kwa kaya na taifa kwa ujumla.
 
Pia wametaka mashirika ya kimataifa yaendelee kuchangia kwa rasilimali uendelezaji wa mifumo asili endelevu kwani manufaa yake ya mazingira ni ya ulimwengu.

Afisa Mkuu wa Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Firmat Banzi alisema kuwa mifumo asili ya kilimo ina haja ya kuendelezwa ili kuboresha na kuimarisha maarifa asili kuwezesha ushiriki wa wakulima katika utunzaji wa mifumo hiyo.

Alifafanua kuwa uendelezaji wa mifumo hiyo utawapa fursa wakulima kuweza kushiriki kikamilifu katika kilimo wakiwa na uhakika wa kupata mazao mengi kuweza kujitosheleza kwa chakula na kujiongezea kipato pamoja na kuboresha hifadhi ya mazingira hasa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Washiriki kwa pamoja wamepitisha azimio linalotambua mchango wa mifumo ya asili ya kilimo na ufugaji na wametoa wito wa kubaini mifumo asili iliyopo nchini, kutathmini mchango wake na changamoto kwa lengo la kuiboresha na kuiendeleza.

 

 

Wakulima na Wafanyabiashara Kuhudhuria Maonesho ya Kilimo Sudani ya Kusini

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Eng Christopher Chiza katika picha ya pamoja na msafara wa watu 14 waliokwenda ziara ya mafunzo ya kilimo Sudani ya Kusini, Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Bibi Sophia Kaduma.

 

Serikali kupitia Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imepeleka wakulima na wafanya biashara wa mazao ya kilimo wapatao 14 katika ziara ya mafunzo katika nchi ya Sudani Kusini.

Akizungumza na waandishi wa habari Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Christopher Chiza alisema hatua hiyo imekuja baada ya kupata mualiko kutoka kwa Waziri wa Kilimo wa nchini Sudan Kusini walipokuwa katika mkutano wa Jukwaa la Mapinduzi ya Kijani (Agra) uliofanyika mjini Arusha.

 “Tumewateua ninyi muwe mabalozi wetu huko Sudan Kusini ili mtakaporejea muweze kuwafikishia wakulima wetu yale mtakayojifunza huko, pia muainishe mazao ambayo yana masoko kwa wingi nchini Sudan.”alisema waziri.

Waziri alisema kuwa mazao mengi ya Tanzania yamekuwa yakipatikana nchini Sudan kama vitunguu, na mchele  kwa bei ya juu lakini mkulima wa Tanzania  anakuwa hafaidiki hivyo kuwataka kuainisha fursa za masoko ili kuongeza kipato.

Waziri aliwahimiza wakulima na wafanyabiashara hao kuainisha fursa mbalimbali ambazo wakulima wa Tanzania wanaweza kunufaika nazo.

Wakulima kwa upande wao wameishukuru Serikali kwa kuwapatia fursa hiyo muhimu ambayo itawawezesha kujifunza na kuahidi kuwa mabalozi wazuri wa wakulima nchini na kuwa chachu ya mabadiliko pindi watakaporejea.

Wakulima na wafanyabiashara wametakiwa kuangalia uwezekano wa kuongeza tija katika mazao kwa kusindika mazao na kuweka nembo ya Tanzania. Aidha, wakulima wametakiwa kutokuuza mazao mashambani kiholela bali wavune na kuyaongezea thamani.

Naye mkuu wa msafara huo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Eng.  Mbogo Futakamba alisema wakulima na wafanyabiashara hao watapata nafasi ya  kuangalia na kujifunza  vikwazo vya kibiashara vilivyopo nchini Sudan ya Kusini ili kuweza kuvifanyia kazi watakaporejea nchini ili kurahisisha ufanyaji biashara nchini humo.

“Ziara hii ya mafunzo itawapa fursa wafanyabiashara na wakulima kujifunza uendeshaji biashara na pia watahudhuria maonesho ya wakulima” aliongeza  Futakamba.

Msafara huu pia utajumuisha wakuu wa wilaya ya Bahi Betty Mkwasa na wilaya ya Kakonko Ndugu Peter Toima  Kiroya na  utaongozwa na Naibu katibu Mkuu toka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Mbogo Futakamba, ziara hiyo ni  ya siku tano.

 

 

AMAGRO Yakabidhiwa Vifaa  vya Kupambana na Nzi wa Embe

Mtaalamu kutoka kitengo cha uthibiti  Visumbufu wa Mimea Kibiolojia Nsami Elibariki akitoa maelezo ya matumizi sahihi ya moja ya vifaa vilivyotolewa na Kituo cha Kimataifa cha Uthibiti Wadudu Waharibifu wa Mazao.


Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imekabidhi vifaa vya  kupambana na Nzi wa embe kwa Chama cha Wakulima wa Embe (AMAGRO) ili kuboresha kilimo cha embe hapa nchini, hafla hiyo ilifanyika katika kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Mikocheni kilichopo Jijini Dar es Salaamu.
Awali Mratibu wa  Mradi wa Udhibiti Nzi wa  waharibifu wa matunda kutoka kitengo cha Afya ya Mimea cha Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Janet Muganyizi alifahamisha kuwa vifaa hivyo vimetoka  Kituo cha Kimatasifa cha kuthibiti Wadudu waharibifu  (ICIPE) chenye makao makuu yake Nairobi nchini Kenya.
Kwa mujibu wa Muganyizi kituo hicho pia kilitoa mafunzo kwa wakulima  huko Kibaha mkoani Pwani  ikiwa ni sehemu ya msaada wa kituo hicho kuboresha kilimo cha embe hapa nchini  miongoni mwa wakulima wa Tanzania.
“Jumla ya wakulima 150 toka ktika mikoa 15 watanufaika na msaada huo muhimu wa kukabiliana na Nzi wa Embe mingoni mwa wakulima wa zao hili” alifahamisha Muganyizi katika hotuba yake ya kumkaribisha mgeni rasmi.

Aliitaja baadhi ya mikoa hiyo kuwa ni   Mbeya, Dar es Salaamu, Pwani, Morogoro, Tanga, Tabora, Dodoma, Mwanza , Iringa, Kilimanjaro, Songea,  Arusha na Lindi.
Vifaa vilivyokabidhiwa katika hafla hiyo kuwa ni lita 20 za kivutia madume, lita 40 za chambo  na mitego 3,000, vikiwa na thamani ya Dola za Kimarekani 6,071 ambayo ni sawa na zaidi ya 9,700,000 zikiwa gharama za ununuzi, alifahamisha Muganyizi.
Naye mgeni rasmi katika hafla hiyo ya makabidhiano ya vifaa hivyo Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao toka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bwana Beatus Malema aliwataka wakulima wa embe walionufaika na msaada wa vifaa hivi kuwa  viwe ni mchangamoto katika kuboresha uzalishaji wa embe zenye ubora ili kuweza kushinda na  kupata nafasi  katika soko la Afrika Mashariki na Dunia.
“ Huu ndio mwanzo kwa ndugu zangu wakulima kuboresha  zao la embe ili tuweze kupiga hatua na kupata soko la uhakika kwa maufaa yetu wenyewe”  aliongeza  Malema
Malema aliwataka wakulima kufuata misingi bora ya uazalishaji wa zao hili ikiwemo usafi katika shamba, kutumia wadudu rafdiki wa mkulima wanaoshambulia Nzi hawa na kwa kutumia mitego ya kunasa Nzi wa embe.
Pia  aliwataka wakulima kuyatumia mafunzo wanayopata toka kwa watalaamu wa kilimo ili kuboresha zao hili la embe kwani vinginevyo wataishia kulima kilimo kisicho na tija.
“ Tukiamua kufanya kweli kuboresha zao la embe tunaweza kubadili maisha yetu na kutoka hapa tulpo katika maisha yetu”  Malema aliwasisitiza wakulima hao.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Embe hapa nchini  ndugu Burton Nsape aliishukuru sana serikali kwa msaada huu muhimu kwa wakulima wa embe hapa nchini, ambao utawasaidia sana kuboresha zao hili na pia utakuwa mwanzo wa kupambana na mdudu Nzi.
“Msaada huu mliotupa utakuwa changamoto kubwa kwao kuboresha zao hili kwa manifaa yao na Taifa kwa ujumla” alisisitiza Nsape wakati akitoa shukrani zake kwa serikali kwa niaba ya wanachama wenzake.
Pia Nsape aliitika serikali issiishie hapa bali iweze kuwafikia wakulima wengine wadogo ili kuboresha kilimo cha zao la embe miongoni mwa wakulima hapa nchini.
Naye mtalaamu wa kilimo toka kitengo cha Uthibiti Visumbufu wa Mimea Kibaolojia  katika kituo cha Kibaha mkoani Pwani Nsami Elibariki aliwataka  wakulima kufuata taratibu za matumizi sahihi  ya vifaa hivi ili kuboresha zao la kilimo cha embe.
Chama cha Wakulima wa zao la Embe kilianza mwaka 2001 kwa kuwa wanachama toka mikoa 15 ya hapa nchini kikwa na lengo kuu la kuboresha kilimo cha embe kwa kuwatanisha wakulima wa zao hili kupambana na changamoto ya kilimo cha zao hili.

 

 

Tanzania Yahimizwa Kuwekeza Sudani ya Kusini

Kiongozi wa msafara wa ziara ya mafunzo ya kilimo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Mbogo Futakamba akizungumza na Waandishi wa Habari Mda mfupi baada ya  kurejea kutoka Sudani ya Kusini.

 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Mbogo Futakamba amesema kuwa  Sudan ya Kusini  ina fursa nyingi ambazo zinaweza kuinufaisha Tanzania kiuchumi kwa siku za usoni.
“Kuna fursa nyingi za uwekezaji hasa katika biashara ya mazao ya chakula kama ndizi na mahindi pamoja na biashara ya pembejeo za kilimo, pia tunaweza kwenda kutoa huduma za ugani ”, aliongeza Futakamba.
Fursa nyingine katika nchi hiyo changa  ni uwekezaji katika nishati ya jua na upepo kutokana na kutokuwa na vyanzo vingine vya uhakika vya  umeme.
Fursa nyingine alizobainisha Eng. Futakamba ni pamoja na uwekezaji katika ujenzi wa miundombinu, hoteli, viwanda vya sukari, uanzishwaji wa kampuni za ushauri wa kitaalamu  pamoja na uanzishaji wa biashara ya vyakula.
Akizungumzia changamoto zilizopo nchini Sudani Kusini Eng. Futakamba alisema kuwa Tanzania haina balozi nchini humo jambo ambalo linakwamisha uingiaji nchini humo kwa watanzania,  hivyo kuiomba serikali kuanzisha balozi nchini humo.
Kwa mujibu wa Eng. Futakamba changamoto nyingine ni huduma za kifedha  ili kuwasaidia wawekezaji wa Tanzania kuwekeza Sudani ya Kusini ni  kutokuwepo kwa taasisi za kifedha nchini humo zenye matawi Tanzania, hivyo kuzitaka taasisi za kifedha kuangalia uwezekano  wa kuwekeza katika nchi hiyo ili kuweza kuwasaidia wawekezaji wa Tanzania.
Aidha, taasisi hizo za kifedha zitasaidia katika kuwawezesha mitaji wafanyabiashara wakubwa na wadogo ili waweze kuendesha shughuli za uwekezaji nchini humo.
Eng. Futakamba  ametoa wito kwa watanzania kuchangamkia fursa hizo kwa kujipanga katika sera za uwekezaji na kuhakikisha kunakuwa na hati za makubaliano baina ya taasisi husika ili kurahishisha shughuli za uwekezaji.
Naye mkuu wa Wilaya ya Bahi Betty Mkwasa alisema kuwa suala la usafiri ni changamoto nyingine kubwa, hivyo kuwataka wadau wa sekta ya usafiri kuwekeza katika usafiri wa kutoka Tanzania kwenda nchini Sudan ya Kusini ili kurahisisha usafirishaji wa bidhaa na watu.
Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kakonko ndugu Peter Toima alisema kuwa watanzania wanaaminika  kimataifa hivyo wachangamkie nafasi hiyo mapema na kuahidi kuwahimiza wadau wao mara watakapo rejea katika wilaya zao kuweza kutumia fursa hizo.
Mkulima wa ndizi kutoka Kagera Bi Akwilina Frances  alisema kuwa wameweza kujionea fursa nyingi nchini Sudani ya Kusini na kubainisha kuwa watanzania wachangamkie fursa hizo kuepuka walanguzi wanaochukua mazao ya Tanzania na kuweka nembo ya nchi nyingine baada ya kuyaongezea thamani.
Ameiomba serikali kuimarisha sekta ya usafirishaji wa ndani ya nchi kuweza kurahisisha kutoa mazao ya wakulima kutoka vijijini kwenda  katika masoko na kuweza kusafirishwa nje ya nchi.
“Nawasihi watanzania wenzangu pamoja na fursa hizo tusije tukauza mazao yote tuongeze nguvu tuzalishe na ziada ya kuweza kuuza nje ya nchi na sisi tuweze kuwa na uhakika wa chakula”, alisema bi. Akwelina.
Bw. Dadrahim Rendis mwakilishi wa wafanyabiashara kutoka wilayani  Kahama alisema kuwa watanzania wanauwezo mkubwa kuweza kutumia fursa hizo hivyo wawe na uthubutu wajiamini wachangamkie fursa hizo mapema.

Ujumbe huo uliondoka nchini tar 26 novemba 2012 kufuatia mwaliko wa waziri wa Kilimo wa Sudani ya Kusini baada ya mazungumzo na Waziri mwenzake wa Kilimo Chakula na Ushirika nchini  Tanzania Mhe. Eng. Christopher Chiza kwenda kutembelea nchi hiyo ili kujifunza na kujionea fursa zilizopo katika sekta ya kilimo na biashara

 

 

Chiza Ainisha Fursa za Kilimo

Waziri wa Kilimo Chaklula na Ushirika Mhe. Eng Christopher Chiza akiongoza mkutano wa wataalamu kutoka Uturuki na maafisa wa wizara hiyo, kulia ni waziri wa Chakula Kilimo na Mifugo wa Uturuki Mhe. Mehdi Eker.

 

 

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Eng. Christopher Kajoro Chiza ameainisha fursa za kilimo ambazo inaweza kushirikiana na serikali ya Uturuki katika kuinua kilimo hapa nchini.

Eng. Chiza aliyasema hayo wakati akizungumza na ujumbe maalumu kutoka  Uturuki ukiongozwa na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Mehdi Eker, ambao ulifika Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kubadilishana mawazo katika kushirikiana uboreshaji wa kilimo.

Moja ya fursa alizobainisha ni pamoja na uwekezaji wa sekta binafsi katika kilimo, sekta ambayo bado haijafanya vya kutosha katika kuinua kilimo.

“Tanzania ina eneo kubwa la kuwekeza katika kilimo lakini bado sekta binafsi haijachukua nafasi yake katika kuinua kilimo” aliongeza Eng. Chiza

Miundo mbinu katika kilimo cha umwagiliaji maji ni sehemu moja ambayo serikali ya Tanzania inaweza kushirikiana na Uturuki na watu wake katika kuboresha kilimo hapa nchini kwa kujenga miundo mbinu bora katika kilimo.

“Bado nchi yetu ina miundo mbinu hafifu  ya teknolojia ya matumizi ya maji katika kuinua kilimo hapa nchini” alifahamisha Eng. Chiza.

Mheshimiwa Eng. Chiza aliitaka pia serikali ya Uturuki kushirikiana na Tanzania katika kuanzisha mpango kabambe wa kuwashirikisha vijana wa Tanzania katika kuinua kilimo hapa nchini.

“ Vijana wetu wanahitaji kupewa moyo ili washiriki kikamilifu katika shughuli za kilimo ili kweli tuweze kufanikiwa katika kilimo chetu kwani vijana ndio nguvu kazi,” aliainisha Mhe. Chiza.

Eneo lingine ambalo Mhe. Eng. Chiza aliuambia ujumbe wa Uturuki kuweza kushirikiana na Tanzania ni kilimo cha maua.

Aliongeza kuwa mfumo wa usafirishaji wa bidhaa za maua hadi katika soko lake bado ni tatizo nchini kwetu, hinyo aliomba Uturuki kushirikiana na Tanzania katika eneo hili ili kuinua kilimo hiki.

Mbali ya fursa hizo pia  Mhe. Eng. Chiza pia aliwafahamisha wajumbe kuwa matumizi ya zana bora za kilimo bado ni kiwango cha chini sana, kwani ni wakulima asilimia 10 tu wanatumia zana bora katika kilimo zikiwemo tractor.

Awali aliwafahamisha  wajumbe hao kuwa   Tanzania ina eneo zaidi ya   milinoni 44  linalofaa kwa kilimo lakini ni asilimia 25 tu linatumika.

Serikali ya Uturuki kupitia ujumbe huo  imeonyesha nia ya kushirikiana Tanzania katika sekta ya umwagiliaji, uzalishaji wa mbegu na kuwekeza katika uzalishaji wa mbolea.

Maeneo mengine ambayo serikali ya Uturuki  imesema kuwa iko tayari kufanya kazi kwa kushirikiana na  serikali ya Tanzania kuwa ni eneo la afya ya mimea, kilimo cha maua na mifugo.

Maamuzi yaliyofikiwa katika mkutano huo ni kuunda kamati maalumu kwa kushirikisha watalaamu wa Tanzania na Uturuki ili kuchambua na kuona maeneo ya kushirikiana katika kuinua kilimo.

 

Wizara Kufufua Mifumo Asili ya Kilimo

Mfumo wa Kilimo cha asili aina ya Kiamba unaotumiwa na kabila la Wachaga.

 

Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imeanzisha Mradi wa kufufua Mifumo muhimu ya asili ya kilimo Duniani (Global Importance Agricutural Heritage System- GIAHS) ili kuendeleza Kilimo cha asili (Oranic Farming) na kumpunguzia mkulima gharama za uzalishaji.

Mradi huo unatekelezwa na Shirika la chakula Duniani (FAO) ambao unalenga kutambua mifumo ya asili na endelevu ya kilimo na ufugaji ili kumsaidia mkulima.

Afisa Mkuu wa Kilimo kutoka Idara ya Matumizi Bora ya Ardhi Bw.  Firmat Banzi
alisema mradi unagharimu zaidi ya dola laki mbili ambazo zimetolewa na Serikali ya Ujerumani.

Alisema kuwa katika Afrika Mashariki nchi ya Tanzania na Kenya ilichaguliwa kufufua mifumo hiyo kwa kuwa na sehemu muhimu za kilimo zanazotumia mifumo hiyo.

Aliongeza kuwa baada ya kuchanguliwa nchi ya Tanzani ilipendekeza mifumo mitatu ya kilimo asili ambayo ni Kihamba ambao hutumiwa na wachaga, Ndiva wa Wapare na Ngoro ambao hutumiwa na kabila la wamatengo.

Alifafanua kuwa mifumo hiyo mitatu ilifanyiwa utafiti na baadaye mfumo wa kichanga ulichaguliwa na kuanza kutumika. 

Aidha, alisema kijiji cha Chimbe juu kilichopo wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro ndio kilichonufaika na mradi huo na sasa unafikia hatua ya mwisho katika utekelezaji wake.

Hatua hiyo imekuja baada ya tafiti mbalimbali kuonesha kushuka kwa bei ya zao la kahawa na kusema kuwa kilimo asili huongeza bei za mazao kwa kuwa mazao yanayolimwa hayatumii kemikali na badala yake hutumia mbolea ya asili kama vile samadi, aliongeza Bw. Banzi.

Mradi huo utasaidia kuboresha zao la kahawa kwa kutumia mbinu husishi za  kukabiliana na wadudu waharibifu wa mazao.

Alifafanua kuwa  mradi unajumuisha utayarishaji wa vitalu vya miche, ukarabati wa mifumo asili ya umwagiliaji na utayarishaji wa mbolea za asili kama vile samadi.

Ili kuhakikisha mradi huu unaendelea Bw. Banzi alisema wameshirikisha wadau mbalimbali ambao watasaidia kuangalia kwa karibu maendeleo ya mradi, alitaja wadau hao kuwa ni Chama cha Ushirika KNCU cha Kilimanjaro pamoja na halmashauri ya wilaya.

Mifumo ya asili ya kilimo ilianza kupendekezwa dunia toka mwaka 2002 na baadhi ya nchi zimeanza kutumia mifumo hii, baadhi ya nchi hizo ni Japani, Philipino, China na Ujerumani.

 

Sekta Binafs Yatakiwa Kushirikiana na Serikali katika Kuendeleza Kilimo

Makamu wa raisi wa serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Gharib Bilal amewataka wakulima kushirikiana na Serikali pamoja na sekta binafi na kutumia rasilimali zilizopo ili kuharakisha mapindizi ya kijani.

Dkt Bilal aliyasema hayo hivi karibuni katika maonesho ya sikukuu ya wakulima Nane Nane yaliyofikia kilele oktaba 8 mwaka huu katika viwanja vya Nzuguni mjini Dodoma.

Alifafanua kuwa Serikali kupitia mpango wa kukuza kilimo katika ukanda wa kusini mwa Tanzania (Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania) imezamilia kuvutia uwekezaji huo wa sekta binafsi katika kilimo.

Aidha, alisema serkali tayari imeanza kuuandaa mpango wa Awamu ya pili wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo utakaojulikana kama ASDPII.

Hatua hiyo imekuja baada ya awamu ya kwanza ya programu ya kuendeleza sekta ya kilimo nchini iliyoanza mwaka 2006 kufikia kikomo mwezi juni 2013.

Aliongeza kuwa katika hatua nyingine serikali kupitia programu kabambe ya kuendeleza kilimo barani Afrika (Comprehesive Africa Agricultural Development Programme-CAADP) pia imezamilia kuongeza ushirikishwaji huo wa sekta binafsi.

Dkt Bilal aliwahamasisha wawekezaji kutoka sekta binafsi kujitokeza kwa wingi ili kuongeza nguvu za serikali katika kufika lengo la Mapinduzi ya Kijani.

 

 

Mafunzo ya Nanenae Yawafurahisha Wakulima

Wakulima wamefurahia mafunzo mbalimbali ya kuendesha  kilimo  yaliyokuwa yanatolewa katika maonyesho ya wakulima Nane Nane yaliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Nzuguni mkoani Dodoma.
Wakulima hao, waliongeza kuwa licha ya kujifunza mambo mbalimbali pia wameweza kupata mbembejeo za Kilimo kwa bei nafuu na kwa urahisi.
Alisema wakulima wameweza kujifunza mambo mbalimbali katika mashamba darasa yaliyoandaliwa na maofisa Kilimo kama mfano kwa wakulima waliokuja katika maonyesho hayo.

“Nimefurahia sana maonyesho hayo kwani yameniwezesha kupata pembejeo kama vile mtambo wa kupukuchi mahindi (global cycle solution) ambao unazwa kwa bei nafuu”, alisema Bwana Alex Sori mkulima wa mahindi kutoka Hombolo.
“Kwa kweli maonyesho haya yameniwezesha kujivunza vitu mbalimbali na jisi ya kukufanya Kilimo changu kuwa cha kisasa zaidi, nimejifunza aina mbalimbali za mbegu na jisi ya kuzipanda ili kuniwezesha kuweza kuvuna mzao mengi”, alisema Bwana Edwini Makaya mkulima kutoka wilayani Chamwino.
Aliongeza kuwa wameweza kujifunza aina mbalimbali za mbegu na jisi ya kupnda katika utaalaamu ambao utawawezesha kuvuna mazao mengi yatakoayoweza kuwaongezea kipata chao.

Bwana Sori aliwashauri wakulima kujenga tabia ya kutembelea maonyesho hayo kwani watawawezesha  kupata mbegu bora na kwa bei nafuu.
Pia alisema kupitia maonyesho hayo ameweza kujifunza teknolojia mbalmbli ambazo ni za kisasa kama vile Kilimo cha umwagiliaji na jinsi ya kutumia zana bora za Kilimo zikiwemo matrekta.

“Hakika maonyesho haya yamenipatia elimu ya namna ya kutumia zana mbalimbali za Kilimo ambazo nimekuwa sijawahi hata kiziona na nilizokuwa nazisikia, leo hii niomeweza kuziona kwa macho yangu na kupatiwa mafunzo ya jinsi ya kuzitumia”, alisema Bibi Magreti Haule, mkulima kutoka Wilayani Kongwa.
Katika maonyesho hayo wakulima pia waliweza kujifunza jinsi ya kudhibiti waduu waharibifu katika mazao mbalimbali kwa kutumia madawa ili kupunguza uharibifu wa mazao.

 

 

Wakulima waaswa juu ya Sensa ya maendeleo ya Kilimo

Wakulima na wadau wa Kilimo wameaswa kutopuuza zoezi la Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika tarehe 26 mwez huu.
Wito huo ulitolewa na  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal katika kilele cha sherehe sikukuu ya wakulima Nane nane iliyofanyika katika viwanja vya Zuguni, mjini Dodoma.
Aidha Dkt Bilal aliwataka wakulima pamoja na wadau wote wa Kilimo kutoa ushirikiano kwa wahudumu wa Sensa ili kufanikisha zoezi hilo muhimu.
“Sensa  ni muhimu katika maendeleo ya nchi na pamoja na watu wake kwani inawezesha Serikali na wadau wake kupanga mikakati sahihi ya maendeleo kwa manufaa ya wote”, Alifafanua Dkt Bilal.
Hata hivyo Dkt Bilal alifafanua kuwa  katika  Sekta ya Kilimo hutoa fursa ya kutambua idadi ya  wakulima na wadau wote wanaotoa huduma katika sekta ya Kilimo ili kupanga mipango katika kuboresha sekta hiyo.
Katika hotuba aliyoitoa Dokta Bilal katika maadhimisho hayo aliwataka wakulima na wadau wengine wa Kilimo kutumia nafasi hiyo muhimu  walionao hasa wakiwa ni sehemu kubwa ya Watanzania  kutoa maoni katika kufanikisha zoezi la ukusanyaji maoni kwa ajili ya Katiba mpya.

 

 

Msukumo wa Pamoja ni Muhimu Katika Kuongeza Uzalishaji wa Mpunga

Wakulima wametakiwa kuweka msukumo wa pamoja ili kuhakikisha kwamba zao la mpunga linaendelezwa kwa kiwango kikubwa ili kuinua kiasi cha uzalishaji na kuongeza usalama wa chakula na kipato.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. E.ng. Christopher Kajoro Chiza alipokuwa akiwahutubia mamia ya wakulima waliohudhuria maadhimisho ya maaonyesho ya zao la mpunga yaliyofanyika katika uwanja wa Mnazi mmoja jijini Dar es salaama
Aidha msukumo huo utawasaidia wakulima kuendeleza uchumi na kuwakwamua wananchi walioko katika ukanda wa mashariki mwa Afrika kutoka kwenye umaskini hususan kwa wakulima wadogo ambao wanahitaji kupata teknolojia mbalimbali zinazoweza kuwasaidia katika kuongeza uzalishaji na tija.
‘Hapa kwetu tunatambua umuhimu wa zao la mpunga. Zao hili ni la pili kwa uzalishaji katika mazao ya nafaka baada ya zao la mahindi na hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Tabora, Mwanza, Mbeya, Rukwa, Morogoro, Arusha, Manyara, Iringa, Mara, Tanga na Kigoma. Aidha uzalishaji wa mpunga unaongezeka mwaka hadi mwaka na takwimu zinaonyesha kwamba eneo la uzalishaji liliongezeka kutoka hekta 490,000 mwaka 1998 mpaka hekta 854,000 mwaka 2011’.
Waziri alisema kuwa  mwaka 2010/2011 uzalishaji wa Mpunga ulifikia wastani wa tani 2,213,020.  Hii inaonyesha uzalishaji wa mpunga unaongezeka kwa kasi kubwa kutokana na kuongezeka kwa ruzuku kwenye mbegu, mbolea pamoja na kupanuliwa kwa eneo la umwagiliaji ambalo kwa sasa limefikia hekta 381,000 ambalo kwa sehemu kubwa linalimwa zao la mpunga.
Inakadiriwa kuwa ongezeko la matumizi ya zao la mpunga kama chakula duniani ni zaidi ya asilimia 6 kwa mwaka. Kwa Tanzania mahitaji yetu ya mchele kwa mwaka 2009/2010 yalikuwa tani 788,570 ikilinganishwa na uzalishaji wa tani 1,699,830. Mwaka 2010/2011 mahitaji yaliongezeka na kufikia  tani 816,648 ikilinganishwa na uzalishaji wa tani 1,461,648 alisema Mh. Chiza.

 

Kuongezeka kwa Bei ya Bidhaa za Nafaka ni Furusa kwa Wakulima

Kupanda kwa bei ya bidhaa za chakula kama mchele na mahindi mijini kwa kiasi kikubwa kumechangiwa  na kuongezeka kwa mahitaji ya bidhaa hizo katika nchi jirani.
Hayo yamesemwa na waziri wa Kilimo chakula na ushirika Mh.Christopher Chiza alipokuwa anaongea na waandishi wa habari katika uwanja wa Mnazi mmoja hivi karibuni
Chakula kutoka Tanzania kimekuwa kikisafirishwa katika nchi za Sudani, Somalia na baadhi nchi jirani hivyo kusababisha ongezeko la mahitaji ya chakula na kufanya bei yake kuwa juu.
Aidha,  bei ya mchele mijini hususan katika jiji la Dar es Salaam imefikia shilingi 2,300 kwa kilo. Pamoja na jitihada za kuingiza mchele kutoka nje, bei yake na hata mahindi haijashuka. Hii ni ishara ya mahitaji makubwa ya nafaka (hasa mchele na mahindi) katika ukanda wa Afrika ya Mashariki na Pembe ya Afrika.
Kutokana na kuongezeka kwa mahitaji kutoka katika nchi za jirani, wakulima na wadau wa kilimo nchini Tanzania wametakiwa kutumia fursa hiyo kuongeza uzalishaji kwa kuwa kuna uhakika wa soko la mazao hayo.

 

 

Mkakati wa Kupambana na Changamoto za Zao la Mpunga

Wizara ya Kilimo chakula na Ushirika na wadau wake imeanzisha  mkakati wa kuendeleza zao la mpunga (National Rice Development Strategy – NRDS) ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo mara dufu ifikapo 2018.
Waziri wa kilimo chakula na ushirika Mh. Eng. Christopher Chiza ametaja upatikanaji mdogo wa mbegu bora kama mojawapo ya changamoto inayokumba zao la mpunga, wakati akiwahutubia wakulima na wadau wa zao hilo ambao walihudhuria maonyesho ya zao la mpunga yaliofanuyika katika uwanja wa Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam yaliyoanza tarehe 18-22 Juni 2012.
Changamoto nyingine ni upatikanaji mdogo wa teknolojia bora za uhifadhi na ufungashaji  (grading and packaging) pamoja na kutokuwepo kwa miundombinu ya umwagiliaji ya kutosha kuongeza uzalishaji wa mpunga alisema Mh. Chiza.
Aidha,  ukosefu wa  masoko ya uhakika  na teknolojia duni za usindikaji zimekuwa zikirudisha nyuma juhudi za wakulima kuuza mazao yao yakiwa ghafi badala ya kuuza kama bidhaa.
Katika mkakati huo maeneo ya kipaumbele ni kuboresha uzalishaji wa mbegu bora, umwagiliaji maji, matumizi ya zana za kisasa, uongezaji thamani kwa zao la mpunga, huduma za ugani na utafiti na masuala ya masoko na mikopo katika kuendeleza zao la mpunga.
Ukosefu wa mikopo kwa wakulima, imekuwa inachangiwa kwa kiasi kikubwa na masharti magumu yanayotolewa na taasisi za kifedha, hivyo wakulima kukosa mitaji ya kuwekeza katika  kilimo alisema Mh Chiza.
Matumizi madogo ya teknolojia rahisi na kasi ndogo ya kusambaa kwa teknolojia miongoni mwa wadau, masuala mtambuka kama maambukizi kwa virus vya Ukimwi na Malaria, pamoja na Ushiriki mdogo wa sekta binafsi katika kilimo ni changamoto  ambazo zinahitaji jitihada maalum katika kuimarisha sekta ya kilimo hapa nchini,  alihitimisha Mhemiwa Waziri.

 

Wizara Yapata Mawaziri Wapya

Mheshimiwa Eng. Christopher Kajoro Chiza Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika (kushoto), Naibu Waziri wake Mheshimiwa Adam Malima (katikati) na Makatibu Wakuu wawili wa Wizara hiyo wakati wa mapokezi ya mawaziri hao baada  yakuwasili makao makuu ya wizara wakitokea  viwanja vya Ikulu walipokuwa wakiapishwa  hivi karibuni

 

Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imepata Mawaziri wapya baada ya kuhamishwa wizara aliyekuwa waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa Prof Jumanne Maghembe na kuwekwa  Mhandisi Christopher Chiza ambaye hapo mwanzo alikuwa ni Naibu waziri wa wizara hii.

 Mheshimiwa Adam Malima ambaye hapo mwanzo alikuwa Naibu waziri wa wizara ya Nishati na madini kwa sasa ndiye Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika.

Mabadiliko hayo yamekuja hivi karibuni baada ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri siku ya tarehe 4 Mei mwaka huu Ikulu jijini Dar es Salaam na kuunda baraza jipya.

Baada ya kufika wizarani kutokea Ikulu walipokuwa wanaapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mawaziri hao waliongea na wakurukungezi na wakuu wa Idara na Vitengo ambapo Waziri mpya wa Wizara ya kilimo Chakula na Ushirika Mhandisi Christopher Chiza alisisitiza kuimarishwa ushirikiano baina ya wafanyakazi ili kufikia malengo walijiwekea

 “Ushirikiano ni chombo kitakacho tupeleka sehemu tunayotaka kwenda ,hivyo ni muhimu kuimarishwa ushirikiano baina yetu ili kuziimarisha huduma zetu. Kila mtumishi asimamie majukumu yake kikamilifu na kwa kufanya hivyo ndipo tutakapo weza kufikia malengo yetu” alifafanua Mhandisi Christopher Chiza.

Kwa upande wake Naibu  Waziri  Mheshimiwa Adam Malima amewataka watumishi wote pamoja nakutekeleza majukumu kiufasaha kuwepo na uwazi katika utendaji wa kazi kama njia rahisi ya kutatua matatizo.

“Uwazi ni jambo zuri sana katika utendaji wa kazi, kwani utatuwezesha kutatua matatizo mbalimbali yatakayokuwa yanatukabili alisema Mheshimiwa Adam Malima.

 

 

 

Waziri  Akutana na Wawezkezaji wa Zao la Miwa

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Prof Jumanne Maghembe amekutana na Bwana Issad Rab Rab kutoka nchini Algeria ambaye pia ni mfanya biashara mkubwa wa mazao yatokanayo na kilimo ili kuangalia uwezekano wa kuwekeza katika kilimo cha Miwa, Mpunga, Matunda na Ngano hapa nchini Tanzania.

Mkutano huo umefanyika hivi karibu ofisini kwakena   kumtaka  mwekezaji huyo kuanza kuharakisha mipango yote ya uwekezaji na kuanza kazi hizo mara moja kutokana na mazao wanayotaka kuwekeza kuwa na uhitaji mkubwa hapa nchini na nje za nchi.

“wakulima wetu wanazalisha  kiasi kidogo cha sukari ambacho hakikidhi mahitaji ya watumiaji  hapa nchini, tunaupungufu wa takribani tani nusu millioni za sukari”, alisema Maghembe.

“Hata nchi za jirani kama vile Kenya, Uganda, Somalia na kongo wanahitaji sukari kutoka kwetu, hii ni fursa nzuri kwa kuwa itaongeza uzalishaji wa Sukari ambayo tutaweza kuuza katika nchi hizo”, aliongeza Prof Mahgembe.

Aidha waziri aliongeza kuwa mbali ya kilimo cha miwa , pia zao la mpunga limekuwa likiihitajika kwa upana zaidi Afrika Mashariki na dunian kwa ujumla hivyo kumtaka mwekezaji pia kuangalia uwekezaji katika zao la mpunga hapa nchini.

Alisema Tanzania ipo tayari kuwapatia ardhi katika sehemu tofautitofauti kutokana na kutokuwepo kwa eneo kubwa katika sehemu moja itakayowezesha kulima mazao hayo.

Waziri aliwaomba kushirikiana na wakulima ili waweze kuona faida na matunda ya kutoa ardhi yao kwa wawekezaji.

Kwa upande wake Bwana Issad Rab alisema endapo watakubaliana wataonza kulima katika msimu ujao ambao unaanza mwezi Novemba mwaka huu, na kuahidi kushirikiana na wakulima kwa kutoa mbegu bora, mbolea na teknolojia za umwagiliaji maji.

Aliongeza kuwa serikali itapata asilimia 40% ya mapato yatokanayo na kilimo hichi pamoja na asilimia 1% kupewa wafanyakazi hodari watakaoshirikiana nao.

Katika kufanikisha swala hilo kwa uharaka zaidi Wazriri Maghembe alisema atakutana na bodi ya sukari na baada ya muda mfupi kwa kushirikiana na na bodi hiyo  watafanya mchakato kubaini sehemem husia.

 

 

 

 

Uzalishaji wa pamba waongezeka

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Prof. Jumanne Maghembe  Akiongea na wawekezaji kutoka Algeria ambao pia ni wafanya biashara mashuhuri duniani walipomtembelela ofsini kwake

 

Uzalishaji wa zao la pamba nchini, umeongezeka kutoka kilo milioni 168 msimu wa mwaka 2010/11 hadi kufikia kilo million 224 katika msimu wa mwaka 2011/12

Akiongea na wawekezaji kutoka Algeria ambao pia ni wafanya biashara mashuhuri duniani ,  Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Prof. Jumanne Maghembe  amesema kuwa katika msimu huu uzalishaji wa pamba umeongezeka kwa kiasi kikukbwa ambacho hakijawahi kutokea  kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita

Aidha Profesa Maghembe aliwaambia wawekezaji hao kuwa moja kati ya mazao ambayo wanaweza kuwekeza hapa nchini ni kilimo cha miwa, ngano matunda  na mpunga, pia aliwataka kuangalia uwezekano wa kuboresha miundombinu ya usafiri wa kutumia bandari ili kuboresha masoko ya mazao kutoka hapa nchini

Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba nchini, Marko Mtunga akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa wadau wa sekta ya pamba barani Afrika na Ulaya, aliwaambia  ongezeko hilo limechangiwa na serikali kwa kutoa ruzuku za pembejeo.

Mtunga alisema pia ongezeko hilo, limetokana na kuimarika kwa bei ya pamba , kuongezeka kwa mvua na usimamizi mzuri wa zao hilo ambalo ni tegemeo kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Alisema bado uzalishaji kwa heka moja katika maeneo mengi sio mzuri kwa kuwa kuna maeneo yanapata kilo 300 kwa heka na kwamba kwenye maeneo mengine, wanapata kilo 1,000 kwa heka.

Alisema kutopatikana kwa kiasi kikubwa cha pamba katika kila heka kunatokana na kuwapo kwa huduma duni  za maofisa ugani, matumizi duni ya zana za kilimo na pembejeo.

Mkurugenzi huyo alisema pia kuyumba kwa bei ya pamba   ambayo ni kati ya sh 1,100 mpaka sh 800 kwa kilo kunachangia wakulima kutoongeza bidii ya kilimo cha zao hilo.

Alisema Tanzania ina uwezo wa kuzalisha kiasi kikubwa cha pamba kuliko nchi nyingine zilizopo Kusini na Mashariki mwa Bara la Afrika .

“ Kwa sasa Tanzania inachuana na Zimbabwe katika kuzalisha kiasi kikubwa cha pamba, ’’alisema Mtunga.

Mkurugenzi huyo alisema hivi sasa asilimia 70 ya pamba, inauzwa nje huku viwanda vya ndani vikitumia asilimia 30.

Alipongeza jitihada za jumuiya ya Ulaya, Mfuko wa mazao Duniani (CFC) na wadau wengine  katika kuboresha zao la pamba Barani Afrika.

 

 

 

 

Kamati Yaidhinisha Matumizi ya Aina 26 za Mbegu


Kamati ya Taifa ya mbegu imeidhinisha matumizi ya aina 26 za mbegu mpya za mazao ya kilimo, ambazo zinatarajiwa kuuanza kutumika msimu wa 2012/2013.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika bwana Mohamed Muya alisema hayo jijini Arusha na kueleza kuwa kuidhinishwa kwa aina hizo za mbegu kumetokana na mapendekezo yaliyofanywa na kamati hiyo katika kikao chake kilichofanyika januari 12 na 13 mwaka huu.
 Bwana Muya alisema kamati hiyo imechukua hutua hiyo baada ya utafiti wa kina ambao umewezesha kugundulika kwa aina hizo za mbegu zenye sifa mbalimbali ikiwemo ya kutoa mazao mengi.
Alisema licha ya kutoa mazao mengi sifa nyingine ya mbegu hizo ni kustahimili ukame, ukinzani dhidi ya magojwa, kukomaa mapema na zinapendwa na walaji kwa kuwa zina ladha nzuri.
Katibu Mkuu alisema kati ya aina hizo za mbegu, aina tano ni za kahawa jamii ya Arabika, aina tisa ni za mahindi, aina moja ni ya shayiri, aina nne zao la chai, aina mbili ulezi, aina moja ni ya maharage na aina nne ni za muhogo.
Aliongeza kuwa mbegu hizo zimefanyiwa utafiti wa kina na vituo vya utafiti vya umma na sekta binafsi hapa nchini.Alivitaja vituo vilivyofanya utafiti huo kuwa ni pamoja na Uyole kilichopo mkoani Mbeya, Naliendele kilichopo mkoani Mtwara, Taasisi ya Utafiti wa Zao la Chai (TRIT) ya Iringa, na Taasisi ya  Utafiti wa kahawa (TaCRI) ya Kilimanjaro.
Taasisi binafi zilizofanya utafiti huo ni pamoja na kampuni binafsi za Suba-Agro Trading and Engineering, Pioneer Overseas, Tanzania Breweries, Mansonto na Maru Agro-tours and Consultants.

 

Tumbaku ya Tanzania Kupata Soko Iran

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Profesa Jumanne Maghembe  amekutana na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Iran, Bwana Mohsin Movahhed Ghomi na kumwambia kuwa Tanzania mwaka 2010/2011 ilizalisha kiasi kikubwa cha tumbaku zaidi ya tani 130,000 na kwamba fursa hiyo ya soko ipo nchini.

Kwa upande wake Balozi wa Iran Bwana Mohsin Movahhed  alisema hiyo ni habari njema kwa viwanda vya sigara vya Tehran na alimuhakikishia Waziri Maghembe kuwa tumbaku hiyo itapata wanunuzi na kuongeza kuwa juhudi zifanyike ili mawasiliano kati ya Ubalozi wake na Serikali ili kuwasiliana na wanunuzi hao ambao wapo tayari kununua kwa kiasi kikubwa

Balozi Mohsin Movahhed aliongeza kuwa Tanzania na Iran zina mahusuano mazuli na ili kuendeleza ushirikiano huo, Iran itaanza kununua mbegu za mafuta kama korosho, karanga na alizeti ambazo nchi hiyo imekuwa ikununua kutoka Pakistan tena kwa bei kubwa wakati inaweza kununua hapa nchini.

Waziri Maghembe alimueleza Balozi Mohsin kuwa Tanzania ina fursa nyingi za kuwekeza hususan katika usindikaji wa bidhaa za mazao ya chakula, mboga na matunda.
“Balozi tunawakaribisha ili muwekeze hapahapa nchi kwa kujenga viwanda vya kusindika korosho kwa kuwa Tanzania ina maeneo ya kutosha na fursa zipo” Alikaririwa Waziri Maghembe.

Naibu Waziri  Aipongeza  ASA

Naibu Waziri wa kilimo Chakula na Ushirika   Christopher Kajolo Chiza (Mb) amezipongeza juhudi zinazofanywa na  ASA katika juhudi za serikali za kuongeza uhakika wa  upatikanaji wa mbegu bora hapa nchini,, kwa lengo la kupunguza utegemezi kutoka nchi zingine. Aliagiza kuza kuwa kuwepo na juhudi za makusudi za kuwashirikisha wakulima wadogo kuzalisha mbegu za kuazimiwa (QDS)

Naibu Waziri vile vile aliwagiza Wahandisi wa Umwagiliaji kufanya uchunguzi (survey) katika mashamba ya Msimba kuhusiana na  ujenzi wa miundombinu ikiwa ni pamoja utokaji wa maji (drainage) kwa lengo la kumwagilia mashamba ya mbegu ili kupunguza utegemezi wa mvua.

Naibu Waziri alimwagiza mchimbaji wa visima kufanya majaribio ya matumizi ya Pampu kutoa maji visimani (pump test) ili kazi zingine zinazohusiana na umwagiliaji zianze mara moja.

Mafunzo kuhusu Mtambo wa Kupokelea Mawasiliano

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi Lilian Mapfa jana alifungua rasmi mafunzo ya uelewa kuhusu mtambo wa kupokelea taarifa za hali ya hewa  wa Wizara.

Mafunzo hayo yanaendeshwa na Kitengo cha Mazingira kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA)
yana lengo la kuongeza uelewa kuhusu masuala ya taarifa za hali ya hewa ambapo Wizara itakuwa na uwezo wa kutoa taarifa sahihi za kiwango cha mvua kwa wakulima wa Tanzania.

Bibi Lilian alisema  lengo la mafunzo hayo yanayofanyika katika Chuo cha Utalii, Tandika ni kuongeza uwezo wa kufuatilia, kujiweka tayari ili kukabiliana na mabadiliko ya kimazingira ikiwemo hifadhi endelevu ya mazingira inayochangia kupunguza umaskini.

Bibi Mapfa aliongeza kuwa mtambo huu utasaidia kufanikisha shughuli za kilimo, utafiti katika kilimo hasa mbegu.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Mazingira cha Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi Shekwanande Natai alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia Wataalam wa Wizara kujua namna ya kutumia mtambo huo na faida zake.

Wahandisi Umwagiliaji,  Wasaidie  Kuibua Miradi ya Umwagiliaji

Naibu Waziri wa Kilimo chakula na Ushirika Mhe. Christopher Kajolo Chiza amewagiza Wahandisi wa Umwagiliaji,  Kuwawezeshe wakulima kuibua miradi ya umwagiliaji.

Hayo aliyasema wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya Wahandisi wa Umwagiliaji wa Umwagiliaji wa Kanda, Sekretariati za Mikoa na Halmashauri za wilaya, yaliyofanyika mjini Morogoro hivi karibuni

Mhe. Chiza aliagiza kuwa fedha zinazotolewa kwa ajili ya  miradi ya umwagiliaji lazima zitumike kama zilivyokusudiwa.

Alisisitiza kuwa  wakulima wajulishwe  kiasi cha fedha kinachotumika katika miradi ya umwagiliaji, maana ya mifuko (Vyanzo vya  fedha)  ikiwa ni pamoja na umoja wao unaowawezesha kutekeleza vizuri miradi ya umwagiliaji.

Aidha Mhe. Chiza alisema kuwa serikali inalenga kuwa ifikapo mwaka 2015 asilimia 25 ya chakula chote kinachozalishwa nchini kitokane na  kilimo cha Umwagiliaji, kwa kuongeza maeneo ya kilimo hicho kufikia hekta 1,000,000, na vile vile kulima kisasa katika maeneo yalioyopo

Kituo cha Technolojia ya Kuendeleza Kilimo Chafunguliwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Dkt. Jakaya Kikwete amefungua kituo cha teknolojia ya kuendeleza kilimo kilichojengwa na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China katika Kijiji cha Cholima, Dakawa, Wilayani Mvomero katika mkoa wa Morogoro.
Kituo hicho kina ukubwa wa ekari 62 kilijengwa kufuatia ziara ya Rais Kikwete nchini China ambapo serikali ya China ilikubali kujenga kituo hiko ikiwa ni mojawapo ya Vituo 14 vitakavyojenga barani Afrika katika kusaidia sekta ya kilimo.

Awali akizungumza juu ya Kituo hicho, Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe alianza kwa kumshukuru mheshimiwa Rais

kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika makabidhiano hayo.
Mheshimiwa Waziri alibainisha kuwa kituo hicho cha kuendeleza teknolijia ya kilimo ni matokea ya mkutano uliofanyika nchini China baina ya viongozi wa Afrika na Serikali hiyo. Na katika mkutano huo Serikali ya China ilikubali kujenga vituo 20 vya kuendeleza kilimo katika Bara la Afrika.
“Ujumbe wa wataalam kutoka China ulitembelea Tanzania mwaka 2008 na kuweka saini makubaliano ya ujenzi wa kituo hicho na baada ya kuweka saini hiyo serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitenga eneo kwa ajili ya mradi huo ambapo mwezi Oktoba 2009 ujenzi ulianza na kukamilika baada ya miezi 13” aliongeza Waziri.
Ujenzi na gharama ya vifaa katika kituo hiki umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 8.8 za Kitanzania huku shughuli muhimu zitakazokuwa zikifanywa na kituo hicho zikiwa ni pamoja na kufanya majaribio kwa mbegu mpya za mazao mbalimbali, kufanya utafiti na kufanya maonyesho ambayo yatawafanya wakulima kujifunza namna ya kukuza mazao mbalimbali, kuendeleza mifugo kama kuku na kuimarisha mashamba yao kwa kupambana na visumbufu vya mazao na kadhalika alikaririwa Profesa Maghembe.
“Aidha Kituo kitaendesha mafunzo ya muda mfupi na semina kwa Wagani na wakulima kuhusu teknolojia za kisasa katika kilimo kwani ni kituo kikubwa kabisa nchini kwetu Tanzania na kimekuja wakati muafaka na kwamba nchi yetu inatekeleza miradi mbalimbali ya kilimo kupitia programu ya ASDP na Azimio la KILIMO KWANZA” alisema Mheshimiwa Maghembe

Kwa upande wake Rais Kikwete aliagiza Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika chini ya Waziri Maghembe kuhakikisha inasimamia kituo hicho kwa manufaa ya taifa na kuhakikisha hakifi baada ya waliokijenga kuondoka ndani ya miaka mitatu ijayo.

 

Kamati ya Bunge Yatoa ushauri Kwa Wizara

Kamati ya Bunge iliyotembelea Wakala wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) hivi karibuni wameishauri Serikali kuongeza juhudi katika kusambaza chakula cha msaada kwa waathirika wa njaa katika Wilaya na Halmashauri zilizokumbwa na tatizo hilo.
Wakiongea kwa nyakati tofauti Wajumbe wa Kamati hiyo wamesema kuwa inachukua muda mrefu kwa chakula cha msaada kuwafikia walengwa kwa sababu ya kuwepo kwa kamati nyingi za ugawaji wa chakula hicho hivyo kuzidi kuwapa hali ngumu walengwa.
Aidha Wajumbe wa Kamati hiyo wamesistizia Idara ya Usalama wa Chakula kutoa ushirikiano mkubwa  kwa  Halmashauri wakati wanapofanya tathimni ili kupata Idadi kamili ya waathirika wa njaa na kuepuka taarifa zisizo sahihi.
Naibu Katibu Mkuu wa  Wizara ya Kilimo Chakaula na Ushirika  Bibi Sophia Kaduma aliieleza Kamati ya Bunge ya Kilimo Maji na Mifugo kuwa  changamoto kubwa kwa Wakala wa Hifadhi ya Chakula ni upatikanaji wa magunia ya kuhifadhia nafaka na idadi ndogo ya maghala.
Alibainisha kuwa kiwanda kinachozalisha magunia ya katani hapa nchini hakina uwezo wa kutosha wa kuzalisha, hivyo kushindwa kusambaza magunia katika taasisi za Wizara ya Kilimo hasa ikizingatiwa kuwa Wizara ina uhitaji mkubwa wa magunia ya kuhifadhia kahawa, pamba na mazao mengineyo katika tasisi zake.
Kuhusu uhaba wa chakula Bibi Sophia Kaduma  amesema kuwa tathimini hufanywa  mapema pindi taarifa zinapopatikana kutoka katika vyanzo  husika.

Wilaya ambazo zimepata upungufu wa chakula zimeshafanyiwa kazi na Wilaya nyingine zilizojitokeza na zinazoendelea kujitokeza zinashugulikiwa haraka alisema Naibu Katibu Mkuu.
Upungufu wa Magala ni changamoto nyingine inayoikabili Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirka ambapo, Wizara ina uwezo wa kuhifadhi Tani Laki Mbili na Elifu Arobaini na Moja tu (241,000) katika maghala yote ingawa lengo ni kuwa na uwezo wa kuhifadhi Tani Laki Nne alisema Naibu Katibu Mkuu

 

Waziri Azungumza na Watumishi wa Makao Makuu

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe  amekutana na watumishi wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Makao Mkuu na kujadili mambo mbalimbali.

 Katika Mkutano huo Waziri Maghembe alianza kwa kuwapongeza Watumishi wote kwa juhudi zao katika utendaji wa kazi za kila siku.

Kabla ya kusikiliza mawazo na michango ya Watumishi alisema kuwa ni lazima Watumishi waamue kwa makusudi kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kumuongezea kipato mkulima wa Tanzania.

Waziri Maghembe aliongeza kuwa ni vyema kama Taifa kuitumia fursa ya kupanda kwa bei ya mazao ya biasha ra kwenye soko la dunia na kutoa mfano wa bei ya pamba imepanda na kufikia shilingi  800 kwa kilo tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ilikuwa ni shilingi 350.

alisema katika shughuli za kilimo kumekuwa na changamoto nyingi zikiwemo za  wakulima kutotumia mbolea, wadudu na wanyama waharibifu pamoja na elimu duni na matumizi finyu ya mbegu bora kwa wakulima.
“Kama wagani wataweza kufanya kazi yao vizuri  na wakulima wakapata ujumbe wetu vizuri na tukawapatia soko la bidhaa zao basi tutazalisha  zaidi ya asilimia 6” alikaririwa Waziri Magheme.
Hata hivyo Waziri alisisitiza kuwa ili kilimo kiwe na mafanikio ni lazima mbegu bora zizalishwe hapa…..

nchini hasa kwa kuzingatia mazingira husika ili  kuepusha hasara kwa kuwa mbegu za ndani zinakuwa na sifa ya hali ya hewa ya hapa nchini na kuwa na ukinzani dhidi ya magonjwa tofauti na zile zinazozalisha nje ya nchi.

Aidha Waziri Maghembe alisisitiza kuongezwa kwa eneo la kilimo cha umwagiliaji maji mashamba ambacho kina uhakika zaidi ya kilimo cha kutegemea mvua.

 

 

Japani Kuendeleza Kilimo cha Mpunga Nchini

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Jumanne Maghembe na Balozi wa Japan Bwana Hiroshima Nakagawa

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe  na Balozi wa Japan  nchini Bw. Hiroshi Nakagawa, wamekutana na kuzungumzia uwezekano wa Japan, kushirikiana na Tanzania  katika kuendeleza zao la mpunga kwa kuleta wataalam wa umwagiliaji ili waweze kutoa mafunzo na elimu wakishirikiana na wenzao wa hapa nchini.

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe amefanya mkutano huo na Balozi Hiroshi Nakagawa ofisini kwake hivi karibuni.

Katika mkutano huo  Waziri  alitumia fursa hiyo kumshukuru Balozi Hiroshi Nakagawa wa Japan kwa ushirikiano mkubwa uliopo baina ya nchi hizi mbili katika masuala mbalimbali hasusan Kilimo.
Aidha Waziri Maghembe alimueleza Balozi Nakagawa kuwa ushirirkiano huo unalenga  kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji maji mashamba na barabara ili kuimarisha uzalishaji wa zao la mpunga nchini kwa lengo la kumuongezea mkulima kipato.

Pamoja na hayo Waziri Maghembe alisema maeneo ya  ushirikiano ni pamoja na kuandaa wataalam wa umwagiliaji maji mashamba ili kutumia rasilimali zilizopo.
Waziri Maghembe aliongeza kuwa Tanzania ni nchi ya kwanza Afrika ambayo ina maji mengi ambayo hayajatumika, hivyo Japan itashirikiana na Tanzania

katika umwagiliaji maji mashamba kwa kutoa mafunzo kwa wataalam na wakulima  ni dhahiri kuwa Taifa litapiga hatua kwa kiasi kikubwa alisema Prof . Maghembe.
 
Naye Balozi Nakagawa alisema kuwa Japan ilishaanza kutoa mafunzo ya umwagiliaji katika Chuo cha Kilimo cha KATC kilichopo Moshi Mkoani Kilimanjaro ambapo katika ushirikiano huo mbinu hizo zitatumika katika kuwafikia wakulima

 

 

 

SERIJALI YAJIPANGA KUJENGA KIWADA CHA KUBAGUA KOROSHO

Naibu Waziri wa kilimo chakula na ushirika Mh. Chiristopher Chiza amekutana na  wawekezaji wa korosho  kutoka katika taasisi mbalimbali za Maerekani (AFRICA HARVEST OF HOPE)’kujadili uwezekano wa kujenga  kiwanda cha kubangua korosho hapa nchini.
 
Akizungumza na wawekezaji hao amesema kuwa  Serikali ya Tanzania inalikaribisha wazo la kujenga kiwanda cha kubangua korosho   kwa lengo la kuongeza ubora wa zao la korosho ili liweze kupata soko zuri hapa nchini na nje ya nchi.

Aidha Mhe. Naibu Waziri  alisema kuwa, mkulima anapata hasara kwa kuuza korosho gafi hivyo kumfanya apate hasara na kushindwa kuondokana na umaskini.

Katika uwekezaji huo Naibu waziri amewataka  wawekezaji hao  kufanya mabo yafuatayo ili kukamilisha tarabu za uwekezaji, kwanza wakitembelee kituo cha uwekezaji (Tanzania Investment Centre), kwa ajili ya kupata mwongozo wa uwekezaji.

Pia wawekezaji hao wawe tayari kuwashirikisha wakulima katika shughuli zao na wawe tayari kuwa na kilimo cha  mkataba  kitakachomwezesha mkulima kuwa na  uhakika wa kipato chake.

Akiongea kwa niaba ya wenzake Bw. Patrick Chiles alisema kuwa, mradi wao ‘AFRICA HARVEST OF HOPE’ unakusudia kwekeza Tanzania katika zao la korosho, baada ya kuona kuwa zao hili linazalishwa  Tanzania lakini sehemu kubwa inasindikwa  nchini India na kuuzwa nchi zingine, hivyo wameona ni vizuri korosho isindikwe hapa hapa Nchini.

Walitoa ahadi kwamba watafuata taratibu zote za uwekezaji,, kununua korosho nyingi kwa ajili ya kuongeza ajira  ya muda mrefu, ambapo wamesma wamesea pia kuwa  Taasisi yao haitakuwa ya kutengeneza faida kubwa.

 

DRD Yadhamaria Kusajili Watafiti

Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti na Maendeleo Dkt. Fidelis  Myaka

 

Idara ya Utafiti na Maendeleo imedhamiria kuweka mkakati wa kuwasajili watengeneza mbegu (Breeders) ili kuwabana wale ambao hawana sifa kama njia ya kuboresha upatikanaji wa mbegu bora.

Azimio hilo lilifikiwa na Wajumbe wa Mkutano wa Kitaifa wa Utafiti wa mbegu uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Hoteli ya Safari uliopo mjini Arusha hivi karibuni.

Katika Mkutano huo, Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti na Maendeleo Dkt. Fidelis Myaka pamoja na Watafiti wengine, wamedhamiria kuanzisha mkakati wa usajili wa wazalisha mbegu baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wakulima na baadhi ya Kampuni za kuzalisha mbegu walidai kuwapo mbegu ambazo  zina kiwango duni na kukosa sifa kadhaa.

Katika usajili huo utaonyesha viwango   vya kitaaluma anavyotakiwa kuwa navyo mzalishaji wa mbegu na  aina za mazao ambazo  anatafiti.

Dkt. Myaka aliendela kusema kuwa Idara itafanya ukaguzi wa Taasisi za utafiti kubaini kama kuna aina za watafiti wasiokidhi viwango ikiwa ni jitihada za kuimarisha uzalishaji wa mbegu. “Kwa kufanya hivi itasaidia kuwarekebisha baadhi ya  Watafiti ambao wanataaluma tofauti na  mbegu wanazozizalisha alisema Dkt. Myaka.

Naye Mwenyekiti wa Mkutano huo Bwana Geoffrey Kirenga amesema Usajili huo utamuweka huru mzalishaji mbegu atakayeamua kuzalisha mbegu tofauti na fani yake kusomea ili kupata taaluma husika, aliongeza kuwa kuwasajili wazalisha mbegu kutaliwezesha taifa kuzalisha mbegu zenye ubora na hatmae kuchangia katika kuinua kilimo alisisitizwa, Bwana Kirenga

 

Jumuia ya Ulaya Kuendelea Kusaidia Sekta ya Kilimo

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe na Balozi wa Jumuia ya Ulaya, Bwana Tim Clarke ofisini kwake

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa, Profesa Jumanne Maghembe amekutana na Balozi wa Jumuia ya Ulaya, Bwana Tim Clarke ofisini kwake hivi karibuni na kuzungumza masuala yanayohusu sekta ya kilimo nchini na namna ya kudumisha na kuendeleza ushirikiano baina ya Tanzania na Jumuia ya Ulaya.

      Balozi Clarke alimueleza Waziri Maghembe kuwa Jumuiya ya Ulaya imedhamiria kuendeleza zao la kahawa na mazao mengine kupitia programu mbalimbali zinazotekelezwa na Jumuia ya Ulaya Barani Afrika.

   Balozi Clarke aliainisha miradi ambayo Jumuiya hiyo inatilia mkazo kuwa ni pamoja na ule wa kuendeleza kilimo cha miwa uliogharimu Euro milioni 6, Progarmu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo, ASDP Euro Milioni 32, utafiti wa zao la chai, Euro milioni 2 na Utafiti kwa kahawa Euro milioni 2.

    Balozi Clarke aliongeza kuwa Euro milioni 30 zipo tayari kusubiri utekelezaji na kuongeza kuwa Jumuia hiyo imeisaidia Tanzania kiasi cha Euro milioni 50 zilizowekezwa kwenye kilimo tu.

     “Jumuia ya Ulaya imetenga Euro bilioni 1 kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa chakula barani Afrika na katika mgao huo Tanzania itapata Euro milioni 32” alikaririwa Balozi Clarke.

    Balozi Clarke aliongeza kuwa Jumuia ya Ulaya inafadhiri  miradi nane nchini ukiwemo ule wa Tanzania Agricultural Partnership – TAP ambao utatekelezwa kati ya Serikali  na Jumuia hiyo katika kuendeleza sekta ya kilimo kwa kuangalia eneo la usalama wa chakula, virutubisho (nutritions) na  kujenga uwezo wa wataalam katika  Vyuo vya Mafunzo kama vile Tengeru alisema mwakilishi huyo wa Jumuia ya Ulaya.

   Kwa upande wake Waziri Maghembe alimueleza mwakilishi huyo nia ya Serikali katika kuhakikisha  kilimo cha Tanzania kinakuwa cha kisasa, chenye tija na enedelevu kinacholenga  kubadili maisha ya wakulima wadogo na wakubwa na kukuza uchumi wa Taifa kwani asilimia 85 ya Watanzania wanajihusisha na kilimo.


 

 

Naibu Waziri atembelea Mkoa wa kigoma

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Eng. Christopher Chiza akitoa maelekezo kwa mafisa wa wilaya ya Kibondo

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Eng. Christopher Chiza  hivi karibuni alimaliza ziara ya kikazi ya  siku sita katika  Mkoa wa Kigoma katika Wilaya za Kigoma Vijijini, Kibondo,na Wilaya mpya ya Kakonko.

Katika ziara hiyo Naibu Waziri alifanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa usambazaji pembejeo  ya ruzuku ikiwa ni pamoja  na kupata maelezo na changamoto zilizojitokeza katika utaratibu mzima wa usambazaji wa pembejeo hizo. Moja ya changamoto kubwa iliyoelezwa na baadhi ya wakulima, ni kwa wakulima  kuweka sahihi kwenye vocha bila ya kuchukua  pembejeo husika kutokana na kutokuwa na uwezo wa kulipia  pembejeo zikiwemo mbegu bora na mbolea

Aidha Mhe. Eng. Chiza aliuagiza  uongozi wa wilaya husika  kufanya ufuatiliaji wa karibu katika zoezi  zima la usambazaji wa pembejeo ili kubaini baadhi ya mawakala ambao sio waaminifu. Katika ufuatiliaji huo kila mkulima aliyeweka saini kwenye vocha itabidi athibitishe kuwa alipokea  pembejeo, na kasha kuonyesha shamba lake zilipotumika  pembejeo hizo.

Mhe Eng. Chiza  vile vile alipata fursa  ya kutembelea wakulima wa zao la kahawa katika kijiji cha Muhange , Shughuli za kilimo cha umwagiliaji na katika kijiji cha Nyamtukuza na Kituo  cha mpakani cha Mabamba katika wilaya ya Kibondo kinachoshughulikia  Ukaguzi wa Mazao na Afya ya Mimea.  

 

 

Tanzania na Israel Kuendeleza Mahusiano

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bwana Mohamed Muya na Balozi wa Israel Afrika ya Mashariki, Bwana Jacob Keidar ofisini kwake hivi karibuni

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bwana Mohamed Muya amesema nia ya Serikali ni kukuza na kuboresha kilimo ili sekta hiyo iwe ya manufaa Kitaifa na Kimataifa.

Akizungumza na Balozi wa Israel wa Afrika ya Mashariki Bwana Jacob Keidar ofisini kwake hivi karibuni, Bwana Muya alisema kilimo kitaboreshwa kwa mikakati mbalimbali kama Kauli Mbiu ya KILIMO KWANZA na Mpango wa Maendeleo ya Kilimo Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia fursa za Tanzania unaojulikana kama (Southern Agricultural Corridor of Tanzania - SAGCOT) ambao ilizunduliwa na Waziri Mkuu Mheshimiwa, Mizengo Pinda wiki mbili zilizopita.
Aliongeza kuwa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika inatekeleza programu ya ASDP (Agricultural  Sector Development Program)

Akizungumzia Azimio la KILIMO KWANZA,  Bwana Muya alisema Kauli Mbiu hiyo ina dhamira ya kubadili kilimo kutoka kilimo cha kujikimu na  kuwa cha kisasa na cha kibiashara kwa kushirikiana na sekta binafsi ili isaidie kuwekeza hasusan kwenye upatikanaji wa mbegu bora za kilimo na si kuiachia Serikali peke yake.

Aliongeza kuwa mahitaji ya mbegu kwa wakulima wa Tanzania ni tani 120,000 kwa mwaka na uwezo wa ndani wa kuzalisha mbegu ni jumla ya tani 6,000 tu ambazo hazitoshelezi.

“Kwa sasa tuna uwezo wa kuzalisha tani 6,000 tu za mbegu bora ambazo hazitoshi kwani mahitaji halisi kwa mwaka ni tani 120,000”. Alikaririwa Bwana Muya.

      Katibu Mkuu alieleza nia ya kuboresha sekta ya kilimo kwa kupitia kilimo cha umwagiliaji na kuhama kutoka matumizi ya jembe la mkono ambalo linatumia muda mwingi na uzalishaji mdogo na kuboresha miundombinu kama barabara ili kuwawezesha wakulima kusafirisha na kuuza mazao yao kwa urahisi.

     Naye Meneja wa Kampuni ya  Balton, Tanzania Bwana Ilan Hanegbi alisema, Kampuni hiyo imejikita zaidi kwenye uuzaji wa miundombinu na mitambo ya kilimo cha umwagiliaji maji mashamba hususan umwagiliaji wa matone (Drip irrigation).
 
    Aliongeza kuwa Kampuni hiyo imewekeza katika Mikoa kadhaa nchini kwa lengo la kuhamasisha kilimo cha umwagiliaji maji mashamba kwa wakulima wadogo na wakubwa. Aliitaja Mikoa hiyo kuwa ni Dodoma (Chilangali SACCOS) na Kilimanjaro (Miwaleni- Moshi) ambapo ufanisi umeanza kuonekana. 
  
    Bwana Hanegbi alisema Balton ipo tayari kugharamia na kuwasomesha wakulima wadogo kupitia ofisi zao za Mikoani ili wapate elimu ya umwagiliaji maji mashamba na elimu ya uhifadhi wa mazao mara baada ya kuvunwa.

Marekani  Kuisaidia Tanzania Katika Sekta  ya Kilimo

Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akiwa na Balozi wa Marekani nchini, Bwana Alfonso Lenhardt (kulia)

Marekani imeahidi kuendelea  kuisaidia Tanzania katika sekta mbalimbali hususan Kilimo. Hayo yemesemwa na Balozi wa Marekani nchini, Bwana Alfonso Lenhardt alipokutana na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe jana akiambatana na ujumbe maalum kutoka Marekani.
Balozi Alfonso Lenhardt alimueleza Waziri Maghembe kuhusu mradi wa “FEED THE FUTURE” kwa kusema kuwa sasa ni wakati muafaka kwa mradi huo kuanza kutekelezwa nchini kwa kuwa una faida kubwa kwa taifa, Balozi Alfonso alizitaja nchi nyingine zilizo katika mradi huo kuwa ni Salvado, Philipines na Ghana.
“Tanzania imechaguliwa kutokana na hatua kubwa iliyopiga katika sekta ya kilimo na dhamira yake ya dhati katika kutekeleza
usalama wa chakula, virutubisho vya mazao na ongezeko la uzalishaji”. Balozi Alfonso Lenhardt  alisema, katika mkutano wa Milenia Rais Obama aliitolea mfano Tanzania kama nchi inayotambulika na Marekani kwa kuonesha kwa nadharia na vitendo jinsi ilivyodhamiria kuendeleza kilimo nchini. Vilevile nchi ya Marekani kutoka kwenye mradi wake wa Millennium Challenge Compact imetenga Dola milioni 600 kwa Tanzania maalum
kwa ujenzi wa barabara na miundo mbinu mingine ili kusaidia sekta ya kilimo kukua na kupanuka kwa haraka. “FEED THE FUTURE inalenga kuwaunganisha Wakulima kwa kutumia miundombinu mbalimbali ndani ya nchi na nje ya nchi jirani kwa lengo la kupata masoko” aliongeza Balozi Alfonso.
Mradi huo wa FEED THE FUTURE pia utasaidia katika maeneo mbalimbali kama vile matumizi bora ya ardhi, kusaidia wakulima wadogo na usafirishaji wa mazao. Kadhalika, nafasi ya mwanamke itawekewa mkazo sambamba na  mipango maalum ili Tanzania iweze kufikia malengo yake katika Kilimo.
FEED THE FUTURE utalenga katika kusaidia mazao ya mpunga, mahindi na mazao ya bustani. Katika mkoa wa Arusha kumekuwa na maendeleo makubwa kwa mazao hayo hivyo kuifanya Serikali ya Marekani kuzidi kusaidia Tanzania na watu wake. Mojawapo ya mradi wa barabara mkubwa ni ule wa kutoka Tunduma mpaka Sumbawanga. Miradi ya umwagiliaji ni pamoja na skimu 7 zilizo mkoani Morogoro.
Kwa upande wake Waziri Maghembe alichukua fursa hiyo kuishukuru Marekani kupitia Balozi na ujumbe wake na kuahidi ushirikiano madhubuti baina ya nchi hizo mbili. Vilevile Waziri Maghembe alizungumzia jinsi ya kuongeza fursa zaidi baina ya nchi hizi mbili katika soko la mazao ya kilimo.

     
Speeches| Publications | Agricultural Statistics | Legislation and Regulations | About us|Contact us
Copyright 2008, Ministry of Agriculture Food Security and Cooperatives All rights reserved.