| |
|
 |
Mazao ya Bustani kutoa mchango mkubwa katika kilimo
Katibu mkuu, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bw. Mohamed Muya amewataka Wakulima wa Tanzania kuchangamkia fulsa ya kulima mazao yenye thamani kubwa kama matunda na mbogamboga kwa kuwa nchi ina maeneo mengi yenye uwezo wa kuzalisha kwa wingi mazao hayo ili kukifanya kilimo kichangie zaidi pato la taifa.
Katibu Mkuu aliyasema hayo wakati wa mkutano maalum na waandishi wa habari leo katika ukumbi wa Mikutano wa Wizara, mkutano huo ulikuwa na lengo la kuufahamisha umma kuhusu maandalizi ya mkutano wa tatu wa wadau wa kilimo cha mazao ya bustani, ambao utafanyika katika hotel ya Naura Spring, mjini Arusha kuanzia tarehe 31 Mei mpaka tarehe 1 Juni.
Bw. Muya aliyataja maeneo hayo ambayo yanafaa kwa Kilimo hicho kuwa ni Mkoa wa Morogoro, Arusha, Kilimanjaro, Mbeya, Tanga, Iringa, Ruvuma, Kigoma, Dodoma, Manyara, Shinyanga, Mara na Mkoa wa Rukwa.
Mazao yanayostawi katika mikoa hiyo ni pamoja na mboga kama kabichi, mchicha, spinanchi na mnavu.
Mazao mengine ni matunda mbalimbali kama maembe, ndizi, machenza, machungwa, mananasi, mapapai, maparachichi, matofaa na mapesheni. Mazao ya viungio ni pamoja na mdalasini, pilipili manga, karafuu, iliki na tangawizi.
Mazao mengine ni ya maua ambayo ni mawaridi ya aina mbalimbali.
Aidha Bw. Muya aliongeza kuwa soko la mazao hayo lipo wazi ndani na nje ya nchi na kutaja soko la nchi za jirani kama Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, masoko mengine ni Mashariki ya Kati, nchi za Jumuia ya Ulaya na Ulaya Mashariki.
Bw. Muya aliongeza kuwa mchango wa mazao ya kilimo cha bustani katika miaka ya hivi karibuni umekuwa ukiongezeka mpaka kufikia wastani wa Shilingi bilioni 150 kwa mwaka.
Ili kukiwezesha kilimo hicho kutoa mchango mkubwa zaidi kuliko ilivyo sasa, wadau wa mazao ya bustani watakutana Arusha wiki chache zijazo kwa ajili ya kuupitia mkakati wa Taifa wa kuendeleza kilimo cha mazao ya bustani (Horticultural Sector Development Strategy) mkakati ambao utajadiliwa na wadua wote. |
|
 |
Mradi wa Afrika Mashariki waanzishwa
Hivi karibuni Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kwa kushirikiana na nchi za Afrika Mashariki ilifanya Kongamano la Mradi wa Afrika Mashariki wa Uboreshaji wa Uzalishaji wa Mazao na Mifugo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Utafiti wa Mazao Bw. Hussein Mansoor alibainisha hayo alipokutana na waandishi wa Kitengo cha Habari wa Wizara.
Bw.Mansoor alisema kuwa mradi huo unashirikisha nchi za Tanzania, Kenya Uganda na Ethiopia.
Aidha Mansoor amesema kuwa mradi huo umeanzishwa kwa malengo ya kushirikiana baina ya nchi hizi nne kwa
kushirikiana teknolojia mbalimbali zinazotumiwa na nchi husika katika kukuza mradi huu.
Bw. Mansoor amesema kuwa mazao husika yamegawanya kwa kila nchi husika ambapo Tanzania itahusika na Kilimo cha mpunga, Ethiopia itahusika na zao la ngano, Uganda itahusika na muhogo na Kenya itahusika na ng’ombe wa maziwa.
Aliongeza kwa Tanzania mradi huu utaanzia katika Kituo cha Utafiti cha Katrini Ifakara na teknolojia zake katika kukuza zao hili zitasambazwa kwa njia ya mtandao katika vituo vya utafiti na taasisi mbalimbali za Kilimo.
Bw Mansoor amebainisha kuwa mazao haya yamegawanywa katika nchi hizi nne kutokana na umahiri wa nchi husika katika kukuza zao husika na utumiaji wa teknolojia za ukuzaji wa kasi wa zao husika. |
|
 |
Tanzania na Afrika kusini
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika inatarajia kuwa na mahusiano ya karibu na Wizara ya Kilimo Misitu na Uvuvi ya nchi Afrika Kusini.
Hayo yamebainika hivi karibuni Waziri wa Kilimo Mh Stephen Wasira alipokuwa na kikao kifupi na Waziri wa Kilimo wa nchi hiyo Bi. Tina Joematt. Peffusson na ujumbe wake ofisini kwake.
Mh. Wasira amesema kuwa mahusiano hayo yanategemewa kuanza hivi karibuni baada ya nchi hiyo kupitisha kisheria memorandam of understanding.
Aidha Mh Wasira amesema kuwa mahusiano hayo yatakuwa katika nyanja mbalimbali hasa katika mimea, kibiashara, usalama wa chakula, umwagiliaji, mazao ya samaki, mazao ya wanyama na mambo mengine ya sekta ya Kilimo. |
|
 |
Katibu aongea na waandishi
Katibu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bw. Mohamed Muya ameongea na waandishi wa habari ikiwa ni kampeni inayofanya na Wizara kupitia Vyombo vya habari
Muya ameeleza jinsi Wizara inavyoshughulikia suala zima la kudhibiti kwelea kwelea na nzige wekundu waliovamia maeneo mbalimbali.
Aidha Katibu Mkuu alieleza changamoto mbalimbali ambazo Wizara imekuwa ikikutana nazo.
Pamoja na hayo Muya alieleza majukumu ya Wizara
ikiwemo kuendeleza rasilimali
Watu, kuendeleza Ushirika, kusimamimia matumizi ya ardhi katika kuhakikisha ardhi inapimwa ili kuweza kutumika kwa matumizi sahihi na kuepukana na ugomvi wa kunyang’anyana ardhi. Pia kusimamia majukumu ya bodi za mazao na utendaji wake kiujumla
Aidha Muya alibainisha kuwa katika kuendeleza Ushirika Wizara imekuwa ikikutana na changamoto mbalimbali kama kutoka katika kilimo tegemezi kwenda kilimo cha umwagiliaji na jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi katika suala zima la kilimo.
Muya alieleza jinsi Wizara ambavyo inashiriki katika kukabiliana na changamoto ya uwekezaji mdogo katika kilimo. Muya amesema kuwa Wizara inashirikisha sekta binafsi katikia kilimo hasa katika vyuo binafsi vya kilimo katika kuelekeza jinsi wagani wanatakiwa kuwa.
Hata hivyo Bw. Muya alitumia fursa hiyo kuwaeleza waandishi kiasi cha pesa za EPA kilichoingia wizarani na mgawanyo wake kwa ajili ya matumizi ya kilimo.
|
|
 |
Wanajeshi wa Nchi Mbalimbali za Afrika Watembelea Wizara
Hivi karibuni wanajeshi wa Nchi mbalimbali za Afrika ambao pia ni wanachuo wa chuo cha kijeshi mjini Arusha walifanya ziara hapa kutembelea hapa Wizarani kwa lengo la kujifunza mambo mbalimbali ya kilimo hususan utekelezaji wa kaulimbiu Kilimo Kwanza
Ugeni Wanajeshi hao waliongozana na Brigedia Generali Ezekieli Elias Kyunga Mwenyeji wao Mkurungezi wa Sera na
Achayo na kwa niaba ya katibu Mkuu Aliwapokea na kujadili masuala ya kilimo ikiwemo kubadilishana mawazo katika dhana nzima ya kilimo.
Pamoja na hayo walipata fursa ya kujadiliana mambo yanayohusu Maendeleo ya kilimo na chakula na hatua zinazo chukuliwa na Wizara katika kilimo ili kutekeleza Kilimo Kwanza |
|
 |
Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Kilimo, Mifugo na Maji inakamilisha ziara yake
kwa kutembelea mashamba ya ngano ya West Kilimanjaro na pia katika Bwawa la Nyumba ya Mungu kabla ya Wajumbe hao kurejea jijini Dar es salaam.
Katika zira hiyo wajumbe walipata fursa ya kuona shughuli mbalimbali katika Miradi ya Kilimo na Umwagiliaji. Miongoni mwa miradi iliyotembelewa ni pamoja na Skimu ya umwagiliaji maji ya Mto wa Mbu. Aidha, wajumbe hao waliwatembelea wakulima wa maua ambayo yanasafirishwa nje ya nchi.
Kabla ya ziara hiyo Wajumbe hao walipata nafasi ya kupitia na kuijadili taarifa ya utekelezaji wa shughuli za Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika. |
|
 |
Ombi Letu ni Matrekta – Mhe. Waziri Mkuu
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Pinda amemweleza Naibu Waziri wa Kilimo na Uvuvi wa Jamhuri ya Watu wa China, Bw. Niu Dun kuwa Tanzania inahitaji msaada zaidi wa matrekta madogo na makubwa ili iweze kupiga hatua katika Kilimo cha kisasa na chenye tija.
Maelezo hayo ameyatoa kwa Naibu Waziri huyo kutoka China baada ya kumtembelea Ofisini kwake akiwa na ujumbe wa watu 12 akiwemo Balozi wa China nchini, Bw. Lik Xnsheng.
Awali kabla ya kutoa ombi hilo Waziri Mkuu alimpongeza Waziri huyo wa Serikali ya Watu wa China kwa kukubali kusaini mkataba wa ushirikiano katika biashara ya uvuvi wa samaki katika kina kirefu cha bahari ambapo Tanzania imekuwa ikiibiwa rasilimali hiyo muhimu kwa miaka kadhaa.
Kabla ya kwenda Ofisi ya Waziri Mkuu, Naibu Waziri huyo alitembelea Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika na kupokelewa na Naibu Waziri Mhe. Dkt. Mathayo David Mathayo.
Katika Mkutano huo Waziri Mathayo aliainisha maeneo ambayo yanahitaji ushirikiano zaidi katika kuyatekeleza kwa pamoja kati ya Tanzania na China kwa lengo la kuongeza ufanisi katika Sekta ya Kilimo. |
|
 |
Idara na Vitengo vijiandae kutekeleza nguzo za Kilimo Kwanza- NKM
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi. Sophia Kaduma hivi karibuni aliutumia mkutano wa Wakuu wa Idara na Vitengo kuwakumbusha Viongozi hao kuanza kuitekeleza kauli mbiu ya Kilimo Kwanza kivitendo.
Naibu Katibu Mkuu alisema kila Mkuu wa Idara au Kitengo anapaswa kukaa pamoja na watumishi wa Idara au Kitengo chake ili wapitie upya mipango kazi yao kwa ajili ya kutekeleza nguzo za Kilimo Kwanza kupitia kazi ambazo zilipangwa kutelezwa katika mwaka 2009/10
“Napenda kuwakumbusha ili kila mmoja ahakikishe shughuli za Idara au Kitengo chake zinatekeleza nguzo za Kilimo Kwanza” Alisisitiza, Naibu Katibu Mkuu.
“Anzeni na nguzo ya kwanza ambayo inatoa picha na dira ya taifa ya Kilimo Kwanza, hasa kipengele kinachohusu kuwaendeleza wakulima wadogo, wakati na wakubwa ili kilimo kiwe cha kisasa na cha kibiashara” alimalizia, Naibu Katibu Mkuu.
Aidha, Naibu Katibu Mkuu aliwaagiza Wakuu wa Idara na Vitengo hao kuhakikisha wanakisoma kitabu cha Kilimo Kwanza ili waweze kuainisha ni nguzo zipi Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika inahusika ili utekelezaji uanze mara moja. |
|
 |
.Wizara yajiandaa kwa tathmini ya kina kwenye maeneo tete
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika inajiandaa kufanya tathmini ya kina ili kubaini maeneo yenye upungufu wa chakula nchini.
Zoezi hilo linatarajiwa kuanza rasmi, Agosti 29 kwa kuzihusisha Wilaya 65 katika mikoa 17 nchini, huku jumla ya timu 25 za wataalam zikishiriki mchakato huo katika mikoa ya Tabora, Shinyanga, Mwanza, Mara, Mtwala, Lindi, Iringa na Mbeya kwa ajili ya kubaini uwezo wa wananchi katika kukabiliana na athari za uhaba wa chakula katika maeneo yao.
Bw. Ombaeli Lemweli, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Uratibu wa Mazao na Tahadhari ya Njaa, Idara ya Usalama wa Chakula alisema kimsingi tathmini hiyo Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika inajiandaa kufanya tathmini ya kina ili kubaini maeneo yenye upungufu wa chakula nchini. |
|
 |
Wizara yajizatiti kukabilian na magonjwa ya migomba
Wizara imeanza mkakati wa kuhakikisha kuwa tatizo la magonjwa yanayoshambulia zao la migomba yanatokomezwa.
Dkt. Rose Mohamed, Mtaalam wa kilimo, kutoka Kitengo cha Afya ya Mimea, Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika alisema Wizara ipo katika mkakati maalum kwa kuvitumia Vituo vya Tafiti za kilimo katika maeneo husika ili kuhakikisha tatizo la magonjwa yanayoathiri zao hilo yanapungua au kwisha kabisa.
Dkt. Rose aliongeza kuwa, serikali kupitia Wataalam wa kilimo katika mikoa iliyoathirika, elimu imeanza kutolewa kuanzia ngazi ya Kaya, namna ya kukabiliana na tatizo la ugonjwa ambao umetoka nchi jirani ya Uganda.
Hivi karibuni, katika Mkutano wa Wataalam wa Uthibiti wa Magonjwa ya Mimea huko mjini Arusha, Mkuu wa Mkoa huo, Bw. Isidory Shirima alipiga marufuku uingizwaji wa migomba kutoka nje ili kupunguza magonjwa kutoka nje na kuingia nchini.
Mkakati wa kupambana na magonjwa ya migomba ulianza mapema mwaka 2006 baada ya kugundulika kuwa migomba kutoka nchi jirani ya Uganda ndiyo chanzo cha athari hizo. |
|
 |
Serikali yapokea zana za Kilimo
Serikali ya Jamhuri ya Korea imeikabidhi serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zana za kilimo, ikiwa ni moja ya hatua za ushirikano zinazochukuliwa kati ya Korea na Tanzania kupitia Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika chini ya Mradi wa kuboresha Kilimo nchini Tanzania-KOIKA.
Lengo la mradi huo ni kuongeza uzalishaji katika kilimo kutokana na promosheni ya matumizi ya ya zana bora za kilimo.
Akikabidhi zana hizo kwa Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, Balozi wa Jamhuri ya Korea Mhe. Youn-Jun Kim, alisema Serikali yake imetenga jumla ya dola za kimarekani 1.7 kwa ajili ya kuboresha kilimo Zanzibar na mkoa wa Morogoro.
Zana zilizokabidhiwa ni matrekta madogo ya mkono 30, pampu za maji 20, trekta kubwa 1, mashine za kuvuna mazao 2, mashine za kupandia 12, mashine za kupandia zenye injini 2 majembe 15, na asilimia 20% ya vipuri, visanduku vya kupandia miche ya mpunga 42,000 |
|
|
|