|
|
|||||||
|
||||||||
|
||||||||
|
||||||||
Wizara Kushirikiana na Indonesia Kukuza Kilimo
Naibu Katibu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bi. Sophia Kaduma wa nne Kulia, akiwa pamoja na Tume ya Ushirikiano wa Pamoja katika sekta ya kilimo.
Tume ya pamoja ya Ushirikiano katika sekta ya kilimo ya Wizara ya Kilimo Chakula na ushirika imejadili maeneo ya kushirikina kwa awamu ya pili na serikali ya Indonesia ili kuongeza tija na uzalishaji katika kilimo. Akizungumza na tume kutoka pande zote mbili Tanzania na Indonesia Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Mama Sophia Kaduma alisema majadiliano hayo yanalenga kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya kilimo pamoja na upatikanaji wa masoko. Mama Kaduma alisema ushirikiano baina ya nchi hizo mbili utahusisha katika kujenga uwezo wa wakulima, masuala ya utafiti pamoja na upatikanaji wa masoko ya mazao. Katika kujenga uwezo Mama kaduma alisema Tanzania na Indonesia itashirikiana katika mafunzo ya Muda mfupi na mrefu pamoja na kubadilishana wakufunzi ambao wataenda kufundisha vyuo mbalimbali vilivyopo katika nchi hizo. Katika mafunzo ya muda mfupi serikali ya Indonesia itafadhili masomo ya Uchumi Kilimo na kilimo cha bustani hasa katika maeneo ya utafiti, usindikaji na mbegu. Aliongeza kuwa masoma hayo yataanza tarehe 1-9/07/1213 na Tanzania itagharamia nauli za washiriki wa program hiyo pamoja na pesa za kujikimu. Kwa upande wa mafunzo ya muda mrefu katika kujenga uwezo, serikali ya Indonesia itatoa ufadhili kwa watu watatu ambao watasoma shahada ya uzamili na uzamifu na mmoja ambaye atasoma masomo yalio chini ya shahada ya kwanza. Pia alisema nchi hizo mbili zitashirikana katika mambo ya utafiti wa mazao hasa katika mazao ya pamba, mpunga na viungo mbalimbali. Alifafanua kuwa utafiti huo utahusisha mambo ya GMO, majaribioa mashambani, uzalishaji wa mbegu bora, magonjwa, usindikaji na uimarishaji wa vituo vya utafiti. Mama Kaduma alisema pian nchi hizo zimekubalia kushirikiana katika katika masoko kwa kubadilishana taarifa za masoko na taratibu mbalimblia ili kuboresha biashara ya bidhaa za kilimo kati ya nchi zote mbili. Alifafaunua kuwa licha ya kushirikiana katika masoko pia Serikali ya Indonesia itashiriki katika maonesho ya kimataifa ya wafanya biashara yafanyika Dar es Salaam (Sabasaba) pamoja na maonesho ya wakulima ya Nane Nane. Ushirikianao baina ya nchi hizo mbili unalenga kuongeza tija katika kilimo, kuongeza upatikanaji wa masoko, kuongeza uzalishaji wa mazao pamoja na kukuza kipato cha mkulima.
|
|
|||||||
Mifumo ya Asili ya Kilimo Kuendelezwa Kuinua Kilimo
Mazao yaliyostawi vizuri yakionyesha mojawapo ya aina ya kilimo Asili cha Mseto Wadau wa kilimo, sera, mazingira, utawala, na mashirika ya kimataifa, wametoa wito wa kubaini mifumo asili ya Kilimo kwa kutambua mchango katika uhakika wa chakula na kipato. Wito huo ulitolewa katika warsha iliyofanyika jijini Dar es Salaam iliyojumuisha wadau hao ili kutathmini mchango wa mifumo asili ya kilimo na changamoto zilizopo ili kuiboresha na kiendeleza. Ilibainika kuwa Tanzania ina mifumo mingi ya asili ya kilimo na mifugo ambayo imedumu kwa taribani zaidi ya miaka 100 hadi 700. Katika kipindi hicho, mifumo mingi imekumbana na mabadiliko ya hali ya hewa lakini imekabili na kudumu, hii inaonyesha kuwa kuna vitu vingi vya kujifunza katika mifumo hiyo. Aidha, wadau wamependekeza mifumo ya asili ya kilimo na ufugaji kuingizwa katika sera kati ya zilizopo ili ipate nguvu ya kusimamiwa na kuendelezwa hasa ikizingatiwa umuhimu wake katika kuimarisha usalama wa chakula na kipato kwa kaya na taifa kwa ujumla. Afisa Mkuu wa Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Firmat Banzi alisema kuwa mifumo asili ya kilimo ina haja ya kuendelezwa ili kuboresha na kuimarisha maarifa asili kuwezesha ushiriki wa wakulima katika utunzaji wa mifumo hiyo. Alifafanua kuwa uendelezaji wa mifumo hiyo utawapa fursa wakulima kuweza kushiriki kikamilifu katika kilimo wakiwa na uhakika wa kupata mazao mengi kuweza kujitosheleza kwa chakula na kujiongezea kipato pamoja na kuboresha hifadhi ya mazingira hasa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Washiriki kwa pamoja wamepitisha azimio linalotambua mchango wa mifumo ya asili ya kilimo na ufugaji na wametoa wito wa kubaini mifumo asili iliyopo nchini, kutathmini mchango wake na changamoto kwa lengo la kuiboresha na kuiendeleza.
|
||||||||
Wakulima na Wafanyabiashara Kuhudhuria Maonesho ya Kilimo Sudani ya Kusini Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Eng Christopher Chiza katika picha ya pamoja na msafara wa watu 14 waliokwenda ziara ya mafunzo ya kilimo Sudani ya Kusini, Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Bibi Sophia Kaduma.
Serikali kupitia Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imepeleka wakulima na wafanya biashara wa mazao ya kilimo wapatao 14 katika ziara ya mafunzo katika nchi ya Sudani Kusini. Akizungumza na waandishi wa habari Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Christopher Chiza alisema hatua hiyo imekuja baada ya kupata mualiko kutoka kwa Waziri wa Kilimo wa nchini Sudan Kusini walipokuwa katika mkutano wa Jukwaa la Mapinduzi ya Kijani (Agra) uliofanyika mjini Arusha. “Tumewateua ninyi muwe mabalozi wetu huko Sudan Kusini ili mtakaporejea muweze kuwafikishia wakulima wetu yale mtakayojifunza huko, pia muainishe mazao ambayo yana masoko kwa wingi nchini Sudan.”alisema waziri. Waziri alisema kuwa mazao mengi ya Tanzania yamekuwa yakipatikana nchini Sudan kama vitunguu, na mchele kwa bei ya juu lakini mkulima wa Tanzania anakuwa hafaidiki hivyo kuwataka kuainisha fursa za masoko ili kuongeza kipato. Waziri aliwahimiza wakulima na wafanyabiashara hao kuainisha fursa mbalimbali ambazo wakulima wa Tanzania wanaweza kunufaika nazo. Wakulima kwa upande wao wameishukuru Serikali kwa kuwapatia fursa hiyo muhimu ambayo itawawezesha kujifunza na kuahidi kuwa mabalozi wazuri wa wakulima nchini na kuwa chachu ya mabadiliko pindi watakaporejea. Wakulima na wafanyabiashara wametakiwa kuangalia uwezekano wa kuongeza tija katika mazao kwa kusindika mazao na kuweka nembo ya Tanzania. Aidha, wakulima wametakiwa kutokuuza mazao mashambani kiholela bali wavune na kuyaongezea thamani. Naye mkuu wa msafara huo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Mbogo Futakamba alisema wakulima na wafanyabiashara hao watapata nafasi ya kuangalia na kujifunza vikwazo vya kibiashara vilivyopo nchini Sudan ya Kusini ili kuweza kuvifanyia kazi watakaporejea nchini ili kurahisisha ufanyaji biashara nchini humo. “Ziara hii ya mafunzo itawapa fursa wafanyabiashara na wakulima kujifunza uendeshaji biashara na pia watahudhuria maonesho ya wakulima” aliongeza Futakamba. Msafara huu pia utajumuisha wakuu wa wilaya ya Bahi Betty Mkwasa na wilaya ya Kakonko Ndugu Peter Toima Kiroya na utaongozwa na Naibu katibu Mkuu toka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Mbogo Futakamba, ziara hiyo ni ya siku tano.
|
||||||||
AMAGRO Yakabidhiwa Vifaa vya Kupambana na Nzi wa Embe Mtaalamu kutoka kitengo cha uthibiti Visumbufu wa Mimea Kibiolojia Nsami Elibariki akitoa maelezo ya matumizi sahihi ya moja ya vifaa vilivyotolewa na Kituo cha Kimataifa cha Uthibiti Wadudu Waharibifu wa Mazao.
Aliitaja baadhi ya mikoa hiyo kuwa ni Mbeya, Dar es Salaamu, Pwani, Morogoro, Tanga, Tabora, Dodoma, Mwanza , Iringa, Kilimanjaro, Songea, Arusha na Lindi. Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Embe hapa nchini ndugu Burton Nsape aliishukuru sana serikali kwa msaada huu muhimu kwa wakulima wa embe hapa nchini, ambao utawasaidia sana kuboresha zao hili na pia utakuwa mwanzo wa kupambana na mdudu Nzi.
|
||||||||
Tanzania Yahimizwa Kuwekeza Sudani ya Kusini Kiongozi wa msafara wa ziara ya mafunzo ya kilimo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Mbogo Futakamba akizungumza na Waandishi wa Habari Mda mfupi baada ya kurejea kutoka Sudani ya Kusini.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Eng. Mbogo Futakamba amesema kuwa Sudan ya Kusini ina fursa nyingi ambazo zinaweza kuinufaisha Tanzania kiuchumi kwa siku za usoni.
|
||||||||
|
Waziri wa Kilimo Chaklula na Ushirika Mhe. Eng Christopher Chiza akiongoza mkutano wa wataalamu kutoka Uturuki na maafisa wa wizara hiyo, kulia ni waziri wa Chakula Kilimo na Mifugo wa Uturuki Mhe. Mehdi Eker.
Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Eng. Christopher Kajoro Chiza ameainisha fursa za kilimo ambazo inaweza kushirikiana na serikali ya Uturuki katika kuinua kilimo hapa nchini. Eng. Chiza aliyasema hayo wakati akizungumza na ujumbe maalumu kutoka Uturuki ukiongozwa na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Mehdi Eker, ambao ulifika Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika kubadilishana mawazo katika kushirikiana uboreshaji wa kilimo. Moja ya fursa alizobainisha ni pamoja na uwekezaji wa sekta binafsi katika kilimo, sekta ambayo bado haijafanya vya kutosha katika kuinua kilimo. “Tanzania ina eneo kubwa la kuwekeza katika kilimo lakini bado sekta binafsi haijachukua nafasi yake katika kuinua kilimo” aliongeza Eng. Chiza Miundo mbinu katika kilimo cha umwagiliaji maji ni sehemu moja ambayo serikali ya Tanzania inaweza kushirikiana na Uturuki na watu wake katika kuboresha kilimo hapa nchini kwa kujenga miundo mbinu bora katika kilimo. “Bado nchi yetu ina miundo mbinu hafifu ya teknolojia ya matumizi ya maji katika kuinua kilimo hapa nchini” alifahamisha Eng. Chiza. Mheshimiwa Eng. Chiza aliitaka pia serikali ya Uturuki kushirikiana na Tanzania katika kuanzisha mpango kabambe wa kuwashirikisha vijana wa Tanzania katika kuinua kilimo hapa nchini. “ Vijana wetu wanahitaji kupewa moyo ili washiriki kikamilifu katika shughuli za kilimo ili kweli tuweze kufanikiwa katika kilimo chetu kwani vijana ndio nguvu kazi,” aliainisha Mhe. Chiza. Eneo lingine ambalo Mhe. Eng. Chiza aliuambia ujumbe wa Uturuki kuweza kushirikiana na Tanzania ni kilimo cha maua. Aliongeza kuwa mfumo wa usafirishaji wa bidhaa za maua hadi katika soko lake bado ni tatizo nchini kwetu, hinyo aliomba Uturuki kushirikiana na Tanzania katika eneo hili ili kuinua kilimo hiki. Mbali ya fursa hizo pia Mhe. Eng. Chiza pia aliwafahamisha wajumbe kuwa matumizi ya zana bora za kilimo bado ni kiwango cha chini sana, kwani ni wakulima asilimia 10 tu wanatumia zana bora katika kilimo zikiwemo tractor. Awali aliwafahamisha wajumbe hao kuwa Tanzania ina eneo zaidi ya milinoni 44 linalofaa kwa kilimo lakini ni asilimia 25 tu linatumika. Serikali ya Uturuki kupitia ujumbe huo imeonyesha nia ya kushirikiana Tanzania katika sekta ya umwagiliaji, uzalishaji wa mbegu na kuwekeza katika uzalishaji wa mbolea. Maeneo mengine ambayo serikali ya Uturuki imesema kuwa iko tayari kufanya kazi kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania kuwa ni eneo la afya ya mimea, kilimo cha maua na mifugo. Maamuzi yaliyofikiwa katika mkutano huo ni kuunda kamati maalumu kwa kushirikisha watalaamu wa Tanzania na Uturuki ili kuchambua na kuona maeneo ya kushirikiana katika kuinua kilimo. |
||||||||
Wizara Kufufua Mifumo Asili ya Kilimo
Mfumo wa Kilimo cha asili aina ya Kiamba unaotumiwa na kabila la Wachaga.
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imeanzisha Mradi wa kufufua Mifumo muhimu ya asili ya kilimo Duniani (Global Importance Agricutural Heritage System- GIAHS) ili kuendeleza Kilimo cha asili (Oranic Farming) na kumpunguzia mkulima gharama za uzalishaji. Mradi huo unatekelezwa na Shirika la chakula Duniani (FAO) ambao unalenga kutambua mifumo ya asili na endelevu ya kilimo na ufugaji ili kumsaidia mkulima. Afisa Mkuu wa Kilimo kutoka Idara ya Matumizi Bora ya Ardhi Bw. Firmat Banzi Alisema kuwa katika Afrika Mashariki nchi ya Tanzania na Kenya ilichaguliwa kufufua mifumo hiyo kwa kuwa na sehemu muhimu za kilimo zanazotumia mifumo hiyo. Aliongeza kuwa baada ya kuchanguliwa nchi ya Tanzani ilipendekeza mifumo mitatu ya kilimo asili ambayo ni Kihamba ambao hutumiwa na wachaga, Ndiva wa Wapare na Ngoro ambao hutumiwa na kabila la wamatengo. Alifafanua kuwa mifumo hiyo mitatu ilifanyiwa utafiti na baadaye mfumo wa kichanga ulichaguliwa na kuanza kutumika. Aidha, alisema kijiji cha Chimbe juu kilichopo wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro ndio kilichonufaika na mradi huo na sasa unafikia hatua ya mwisho katika utekelezaji wake. Hatua hiyo imekuja baada ya tafiti mbalimbali kuonesha kushuka kwa bei ya zao la kahawa na kusema kuwa kilimo asili huongeza bei za mazao kwa kuwa mazao yanayolimwa hayatumii kemikali na badala yake hutumia mbolea ya asili kama vile samadi, aliongeza Bw. Banzi. Mradi huo utasaidia kuboresha zao la kahawa kwa kutumia mbinu husishi za kukabiliana na wadudu waharibifu wa mazao. Alifafanua kuwa mradi unajumuisha utayarishaji wa vitalu vya miche, ukarabati wa mifumo asili ya umwagiliaji na utayarishaji wa mbolea za asili kama vile samadi. Ili kuhakikisha mradi huu unaendelea Bw. Banzi alisema wameshirikisha wadau mbalimbali ambao watasaidia kuangalia kwa karibu maendeleo ya mradi, alitaja wadau hao kuwa ni Chama cha Ushirika KNCU cha Kilimanjaro pamoja na halmashauri ya wilaya. Mifumo ya asili ya kilimo ilianza kupendekezwa dunia toka mwaka 2002 na baadhi ya nchi zimeanza kutumia mifumo hii, baadhi ya nchi hizo ni Japani, Philipino, China na Ujerumani. |
||||||||
Sekta Binafs Yatakiwa Kushirikiana na Serikali katika Kuendeleza Kilimo
Makamu wa raisi wa serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Gharib Bilal amewataka wakulima kushirikiana na Serikali pamoja na sekta binafi na kutumia rasilimali zilizopo ili kuharakisha mapindizi ya kijani. Dkt Bilal aliyasema hayo hivi karibuni katika maonesho ya sikukuu ya wakulima Nane Nane yaliyofikia kilele oktaba 8 mwaka huu katika viwanja vya Nzuguni mjini Dodoma. Alifafanua kuwa Serikali kupitia mpango wa kukuza kilimo katika ukanda wa kusini mwa Tanzania (Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania) imezamilia kuvutia uwekezaji huo wa sekta binafsi katika kilimo. Aidha, alisema serkali tayari imeanza kuuandaa mpango wa Awamu ya pili wa programu ya kuendeleza sekta ya kilimo utakaojulikana kama ASDPII. Hatua hiyo imekuja baada ya awamu ya kwanza ya programu ya kuendeleza sekta ya kilimo nchini iliyoanza mwaka 2006 kufikia kikomo mwezi juni 2013. Aliongeza kuwa katika hatua nyingine serikali kupitia programu kabambe ya kuendeleza kilimo barani Afrika (Comprehesive Africa Agricultural Development Programme-CAADP) pia imezamilia kuongeza ushirikishwaji huo wa sekta binafsi. Dkt Bilal aliwahamasisha wawekezaji kutoka sekta binafsi kujitokeza kwa wingi ili kuongeza nguvu za serikali katika kufika lengo la Mapinduzi ya Kijani.
|
||||||||
Mafunzo ya Nanenae Yawafurahisha Wakulima
Wakulima wamefurahia mafunzo mbalimbali ya kuendesha kilimo yaliyokuwa yanatolewa katika maonyesho ya wakulima Nane Nane yaliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Nzuguni mkoani Dodoma. “Nimefurahia sana maonyesho hayo kwani yameniwezesha kupata pembejeo kama vile mtambo wa kupukuchi mahindi (global cycle solution) ambao unazwa kwa bei nafuu”, alisema Bwana Alex Sori mkulima wa mahindi kutoka Hombolo. Bwana Sori aliwashauri wakulima kujenga tabia ya kutembelea maonyesho hayo kwani watawawezesha kupata mbegu bora na kwa bei nafuu. “Hakika maonyesho haya yamenipatia elimu ya namna ya kutumia zana mbalimbali za Kilimo ambazo nimekuwa sijawahi hata kiziona na nilizokuwa nazisikia, leo hii niomeweza kuziona kwa macho yangu na kupatiwa mafunzo ya jinsi ya kuzitumia”, alisema Bibi Magreti Haule, mkulima kutoka Wilayani Kongwa.
|
||||||||
Wakulima waaswa juu ya Sensa ya maendeleo ya KilimoWakulima na wadau wa Kilimo wameaswa kutopuuza zoezi la Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika tarehe 26 mwez huu.
|
||||||||
Msukumo wa Pamoja ni Muhimu Katika Kuongeza Uzalishaji wa Mpunga
Wakulima wametakiwa kuweka msukumo wa pamoja ili kuhakikisha kwamba zao la mpunga linaendelezwa kwa kiwango kikubwa ili kuinua kiasi cha uzalishaji na kuongeza usalama wa chakula na kipato. |
||||||||
Kuongezeka kwa Bei ya Bidhaa za Nafaka ni Furusa kwa Wakulima
Kupanda kwa bei ya bidhaa za chakula kama mchele na mahindi mijini kwa kiasi kikubwa kumechangiwa na kuongezeka kwa mahitaji ya bidhaa hizo katika nchi jirani.
|
||||||||
Mkakati wa Kupambana na Changamoto za Zao la Mpunga
Wizara ya Kilimo chakula na Ushirika na wadau wake imeanzisha mkakati wa kuendeleza zao la mpunga (National Rice Development Strategy – NRDS) ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo mara dufu ifikapo 2018. |
||||||||
|
Mheshimiwa Eng. Christopher Kajoro Chiza Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika (kushoto), Naibu Waziri wake Mheshimiwa Adam Malima (katikati) na Makatibu Wakuu wawili wa Wizara hiyo wakati wa mapokezi ya mawaziri hao baada yakuwasili makao makuu ya wizara wakitokea viwanja vya Ikulu walipokuwa wakiapishwa hivi karibuni
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imepata Mawaziri wapya baada ya kuhamishwa wizara aliyekuwa waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa Prof Jumanne Maghembe na kuwekwa Mhandisi Christopher Chiza ambaye hapo mwanzo alikuwa ni Naibu waziri wa wizara hii. Mheshimiwa Adam Malima ambaye hapo mwanzo alikuwa Naibu waziri wa wizara ya Nishati na madini kwa sasa ndiye Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika. Mabadiliko hayo yamekuja hivi karibuni baada ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri siku ya tarehe 4 Mei mwaka huu Ikulu jijini Dar es Salaam na kuunda baraza jipya. Baada ya kufika wizarani kutokea Ikulu walipokuwa wanaapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mawaziri hao waliongea na wakurukungezi na wakuu wa Idara na Vitengo ambapo Waziri mpya wa Wizara ya kilimo Chakula na Ushirika Mhandisi Christopher Chiza alisisitiza kuimarishwa ushirikiano baina ya wafanyakazi ili kufikia malengo walijiwekea “Ushirikiano ni chombo kitakacho tupeleka sehemu tunayotaka kwenda ,hivyo ni muhimu kuimarishwa ushirikiano baina yetu ili kuziimarisha huduma zetu. Kila mtumishi asimamie majukumu yake kikamilifu na kwa kufanya hivyo ndipo tutakapo weza kufikia malengo yetu” alifafanua Mhandisi Christopher Chiza. Kwa upande wake Naibu Waziri Mheshimiwa Adam Malima amewataka watumishi wote pamoja nakutekeleza majukumu kiufasaha kuwepo na uwazi katika utendaji wa kazi kama njia rahisi ya kutatua matatizo. “Uwazi ni jambo zuri sana katika utendaji wa kazi, kwani utatuwezesha kutatua matatizo mbalimbali yatakayokuwa yanatukabili alisema Mheshimiwa Adam Malima.
|
||||||||
Waziri Akutana na Wawezkezaji wa Zao la Miwa Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Prof Jumanne Maghembe amekutana na Bwana Issad Rab Rab kutoka nchini Algeria ambaye pia ni mfanya biashara mkubwa wa mazao yatokanayo na kilimo ili kuangalia uwezekano wa kuwekeza katika kilimo cha Miwa, Mpunga, Matunda na Ngano hapa nchini Tanzania. Mkutano huo umefanyika hivi karibu ofisini kwakena kumtaka mwekezaji huyo kuanza kuharakisha mipango yote ya uwekezaji na kuanza kazi hizo mara moja kutokana na mazao wanayotaka kuwekeza kuwa na uhitaji mkubwa hapa nchini na nje za nchi. “wakulima wetu wanazalisha kiasi kidogo cha sukari ambacho hakikidhi mahitaji ya watumiaji hapa nchini, tunaupungufu wa takribani tani nusu millioni za sukari”, alisema Maghembe. “Hata nchi za jirani kama vile Kenya, Uganda, Somalia na kongo wanahitaji sukari kutoka kwetu, hii ni fursa nzuri kwa kuwa itaongeza uzalishaji wa Sukari ambayo tutaweza kuuza katika nchi hizo”, aliongeza Prof Mahgembe. Aidha waziri aliongeza kuwa mbali ya kilimo cha miwa , pia zao la mpunga limekuwa likiihitajika kwa upana zaidi Afrika Mashariki na dunian kwa ujumla hivyo kumtaka mwekezaji pia kuangalia uwekezaji katika zao la mpunga hapa nchini. Alisema Tanzania ipo tayari kuwapatia ardhi katika sehemu tofautitofauti kutokana na kutokuwepo kwa eneo kubwa katika sehemu moja itakayowezesha kulima mazao hayo. Waziri aliwaomba kushirikiana na wakulima ili waweze kuona faida na matunda ya kutoa ardhi yao kwa wawekezaji. Kwa upande wake Bwana Issad Rab alisema endapo watakubaliana wataonza kulima katika msimu ujao ambao unaanza mwezi Novemba mwaka huu, na kuahidi kushirikiana na wakulima kwa kutoa mbegu bora, mbolea na teknolojia za umwagiliaji maji. Aliongeza kuwa serikali itapata asilimia 40% ya mapato yatokanayo na kilimo hichi pamoja na asilimia 1% kupewa wafanyakazi hodari watakaoshirikiana nao. Katika kufanikisha swala hilo kwa uharaka zaidi Wazriri Maghembe alisema atakutana na bodi ya sukari na baada ya muda mfupi kwa kushirikiana na na bodi hiyo watafanya mchakato kubaini sehemem husia.
|
||||||||
Uzalishaji wa pamba waongezeka
Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Prof. Jumanne Maghembe Akiongea na wawekezaji kutoka Algeria ambao pia ni wafanya biashara mashuhuri duniani walipomtembelela ofsini kwake
Uzalishaji wa zao la pamba nchini, umeongezeka kutoka kilo milioni 168 msimu wa mwaka 2010/11 hadi kufikia kilo million 224 katika msimu wa mwaka 2011/12 Akiongea na wawekezaji kutoka Algeria ambao pia ni wafanya biashara mashuhuri duniani , Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Prof. Jumanne Maghembe amesema kuwa katika msimu huu uzalishaji wa pamba umeongezeka kwa kiasi kikukbwa ambacho hakijawahi kutokea kwa kipindi cha miaka 50 iliyopita Aidha Profesa Maghembe aliwaambia wawekezaji hao kuwa moja kati ya mazao ambayo wanaweza kuwekeza hapa nchini ni kilimo cha miwa, ngano matunda na mpunga, pia aliwataka kuangalia uwezekano wa kuboresha miundombinu ya usafiri wa kutumia bandari ili kuboresha masoko ya mazao kutoka hapa nchini Naye Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba nchini, Marko Mtunga akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa wadau wa sekta ya pamba barani Afrika na Ulaya, aliwaambia ongezeko hilo limechangiwa na serikali kwa kutoa ruzuku za pembejeo. Mtunga alisema pia ongezeko hilo, limetokana na kuimarika kwa bei ya pamba , kuongezeka kwa mvua na usimamizi mzuri wa zao hilo ambalo ni tegemeo kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa. Alisema bado uzalishaji kwa heka moja katika maeneo mengi sio mzuri kwa kuwa kuna maeneo yanapata kilo 300 kwa heka na kwamba kwenye maeneo mengine, wanapata kilo 1,000 kwa heka. Alisema kutopatikana kwa kiasi kikubwa cha pamba katika kila heka kunatokana na kuwapo kwa huduma duni za maofisa ugani, matumizi duni ya zana za kilimo na pembejeo. Mkurugenzi huyo alisema pia kuyumba kwa bei ya pamba ambayo ni kati ya sh 1,100 mpaka sh 800 kwa kilo kunachangia wakulima kutoongeza bidii ya kilimo cha zao hilo. Alisema Tanzania ina uwezo wa kuzalisha kiasi kikubwa cha pamba kuliko nchi nyingine zilizopo Kusini na Mashariki mwa Bara la Afrika . “ Kwa sasa Tanzania inachuana na Zimbabwe katika kuzalisha kiasi kikubwa cha pamba, ’’alisema Mtunga. Mkurugenzi huyo alisema hivi sasa asilimia 70 ya pamba, inauzwa nje huku viwanda vya ndani vikitumia asilimia 30. Alipongeza jitihada za jumuiya ya Ulaya, Mfuko wa mazao Duniani (CFC) na wadau wengine katika kuboresha zao la pamba Barani Afrika.
|
||||||||
Kamati Yaidhinisha Matumizi ya Aina 26 za Mbegu
|
||||||||
Tumbaku ya Tanzania Kupata Soko Iran Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Profesa Jumanne Maghembe amekutana na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Iran, Bwana Mohsin Movahhed Ghomi na kumwambia kuwa Tanzania mwaka 2010/2011 ilizalisha kiasi kikubwa cha tumbaku zaidi ya tani 130,000 na kwamba fursa hiyo ya soko ipo nchini. Kwa upande wake Balozi wa Iran Bwana Mohsin Movahhed alisema hiyo ni habari njema kwa viwanda vya sigara vya Tehran na alimuhakikishia Waziri Maghembe kuwa tumbaku hiyo itapata wanunuzi na kuongeza kuwa juhudi zifanyike ili mawasiliano kati ya Ubalozi wake na Serikali ili kuwasiliana na wanunuzi hao ambao wapo tayari kununua kwa kiasi kikubwa Balozi Mohsin Movahhed aliongeza kuwa Tanzania na Iran zina mahusuano mazuli na ili kuendeleza ushirikiano huo, Iran itaanza kununua mbegu za mafuta kama korosho, karanga na alizeti ambazo nchi hiyo imekuwa ikununua kutoka Pakistan tena kwa bei kubwa wakati inaweza kununua hapa nchini. Waziri Maghembe alimueleza Balozi Mohsin kuwa Tanzania ina fursa nyingi za kuwekeza hususan katika usindikaji wa bidhaa za mazao ya chakula, mboga na matunda.
Naibu Waziri wa kilimo Chakula na Ushirika Christopher Kajolo Chiza (Mb) amezipongeza juhudi zinazofanywa na ASA katika juhudi za serikali za kuongeza uhakika wa upatikanaji wa mbegu bora hapa nchini,, kwa lengo la kupunguza utegemezi kutoka nchi zingine. Aliagiza kuza kuwa kuwepo na juhudi za makusudi za kuwashirikisha wakulima wadogo kuzalisha mbegu za kuazimiwa (QDS) Naibu Waziri vile vile aliwagiza Wahandisi wa Umwagiliaji kufanya uchunguzi (survey) katika mashamba ya Msimba kuhusiana na ujenzi wa miundombinu ikiwa ni pamoja utokaji wa maji (drainage) kwa lengo la kumwagilia mashamba ya mbegu ili kupunguza utegemezi wa mvua. Naibu Waziri alimwagiza mchimbaji wa visima kufanya majaribio ya matumizi ya Pampu kutoa maji visimani (pump test) ili kazi zingine zinazohusiana na umwagiliaji zianze mara moja. Mafunzo kuhusu Mtambo wa Kupokelea Mawasiliano
Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi Lilian Mapfa jana alifungua rasmi mafunzo ya uelewa kuhusu mtambo wa kupokelea taarifa za hali ya hewa wa Wizara. Mafunzo hayo yanaendeshwa na Kitengo cha Mazingira kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) Bibi Lilian alisema lengo la mafunzo hayo yanayofanyika katika Chuo cha Utalii, Tandika ni kuongeza uwezo wa kufuatilia, kujiweka tayari ili kukabiliana na mabadiliko ya kimazingira ikiwemo hifadhi endelevu ya mazingira inayochangia kupunguza umaskini. Bibi Mapfa aliongeza kuwa mtambo huu utasaidia kufanikisha shughuli za kilimo, utafiti katika kilimo hasa mbegu. Naye Mkuu wa Kitengo cha Mazingira cha Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi Shekwanande Natai alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia Wataalam wa Wizara kujua namna ya kutumia mtambo huo na faida zake. Wahandisi Umwagiliaji, Wasaidie Kuibua Miradi ya Umwagiliaji
Naibu Waziri wa Kilimo chakula na Ushirika Mhe. Christopher Kajolo Chiza amewagiza Wahandisi wa Umwagiliaji, Kuwawezeshe wakulima kuibua miradi ya umwagiliaji. Hayo aliyasema wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya Wahandisi wa Umwagiliaji wa Umwagiliaji wa Kanda, Sekretariati za Mikoa na Halmashauri za wilaya, yaliyofanyika mjini Morogoro hivi karibuni Mhe. Chiza aliagiza kuwa fedha zinazotolewa kwa ajili ya miradi ya umwagiliaji lazima zitumike kama zilivyokusudiwa. Alisisitiza kuwa wakulima wajulishwe kiasi cha fedha kinachotumika katika miradi ya umwagiliaji, maana ya mifuko (Vyanzo vya fedha) ikiwa ni pamoja na umoja wao unaowawezesha kutekeleza vizuri miradi ya umwagiliaji. Aidha Mhe. Chiza alisema kuwa serikali inalenga kuwa ifikapo mwaka 2015 asilimia 25 ya chakula chote kinachozalishwa nchini kitokane na kilimo cha Umwagiliaji, kwa kuongeza maeneo ya kilimo hicho kufikia hekta 1,000,000, na vile vile kulima kisasa katika maeneo yalioyopo Kituo cha Technolojia ya Kuendeleza Kilimo Chafunguliwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa, Dkt. Jakaya Kikwete amefungua kituo cha teknolojia ya kuendeleza kilimo kilichojengwa na Serikali ya Jamhuri ya watu wa China katika Kijiji cha Cholima, Dakawa, Wilayani Mvomero katika mkoa wa Morogoro. Awali akizungumza juu ya Kituo hicho, Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe alianza kwa kumshukuru mheshimiwa Rais kwa kukubali kuwa mgeni rasmi katika makabidhiano hayo. Kwa upande wake Rais Kikwete aliagiza Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika chini ya Waziri Maghembe kuhakikisha inasimamia kituo hicho kwa manufaa ya taifa na kuhakikisha hakifi baada ya waliokijenga kuondoka ndani ya miaka mitatu ijayo. |
||||||||
Kamati ya Bunge Yatoa ushauri Kwa Wizara Kamati ya Bunge iliyotembelea Wakala wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) hivi karibuni wameishauri Serikali kuongeza juhudi katika kusambaza chakula cha msaada kwa waathirika wa njaa katika Wilaya na Halmashauri zilizokumbwa na tatizo hilo. Wilaya ambazo zimepata upungufu wa chakula zimeshafanyiwa kazi na Wilaya nyingine zilizojitokeza na zinazoendelea kujitokeza zinashugulikiwa haraka alisema Naibu Katibu Mkuu. |
||||||||
Waziri Azungumza na Watumishi wa Makao Makuu
Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa Profesa Jumanne Maghembe amekutana na watumishi wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Makao Mkuu na kujadili mambo mbalimbali. Katika Mkutano huo Waziri Maghembe alianza kwa kuwapongeza Watumishi wote kwa juhudi zao katika utendaji wa kazi za kila siku. Kabla ya kusikiliza mawazo na michango ya Watumishi alisema kuwa ni lazima Watumishi waamue kwa makusudi kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kumuongezea kipato mkulima wa Tanzania. Waziri Maghembe aliongeza kuwa ni vyema kama Taifa kuitumia fursa ya kupanda kwa bei ya mazao ya biasha ra kwenye soko la dunia na kutoa mfano wa bei ya pamba imepanda na kufikia shilingi 800 kwa kilo tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ilikuwa ni shilingi 350. alisema katika shughuli za kilimo kumekuwa na changamoto nyingi zikiwemo za wakulima kutotumia mbolea, wadudu na wanyama waharibifu pamoja na elimu duni na matumizi finyu ya mbegu bora kwa wakulima. nchini hasa kwa kuzingatia mazingira husika ili kuepusha hasara kwa kuwa mbegu za ndani zinakuwa na sifa ya hali ya hewa ya hapa nchini na kuwa na ukinzani dhidi ya magonjwa tofauti na zile zinazozalisha nje ya nchi. Aidha Waziri Maghembe alisisitiza kuongezwa kwa eneo la kilimo cha umwagiliaji maji mashamba ambacho kina uhakika zaidi ya kilimo cha kutegemea mvua. |
||||||||
Japani Kuendeleza Kilimo cha Mpunga Nchini
Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Jumanne Maghembe na Balozi wa Japan Bwana Hiroshima Nakagawa Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe na Balozi wa Japan nchini Bw. Hiroshi Nakagawa, wamekutana na kuzungumzia uwezekano wa Japan, kushirikiana na Tanzania katika kuendeleza zao la mpunga kwa kuleta wataalam wa umwagiliaji ili waweze kutoa mafunzo na elimu wakishirikiana na wenzao wa hapa nchini. Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe amefanya mkutano huo na Balozi Hiroshi Nakagawa ofisini kwake hivi karibuni. Katika mkutano huo Waziri alitumia fursa hiyo kumshukuru Balozi Hiroshi Nakagawa wa Japan kwa ushirikiano mkubwa uliopo baina ya nchi hizi mbili katika masuala mbalimbali hasusan Kilimo. Pamoja na hayo Waziri Maghembe alisema maeneo ya ushirikiano ni pamoja na kuandaa wataalam wa umwagiliaji maji mashamba ili kutumia rasilimali zilizopo. katika umwagiliaji maji mashamba kwa kutoa mafunzo kwa wataalam na wakulima ni dhahiri kuwa Taifa litapiga hatua kwa kiasi kikubwa alisema Prof . Maghembe.
|
||||||||
SERIJALI YAJIPANGA KUJENGA KIWADA CHA KUBAGUA KOROSHO
Naibu Waziri wa kilimo chakula na ushirika Mh. Chiristopher Chiza amekutana na wawekezaji wa korosho kutoka katika taasisi mbalimbali za Maerekani (AFRICA HARVEST OF HOPE)’kujadili uwezekano wa kujenga kiwanda cha kubangua korosho hapa nchini. Aidha Mhe. Naibu Waziri alisema kuwa, mkulima anapata hasara kwa kuuza korosho gafi hivyo kumfanya apate hasara na kushindwa kuondokana na umaskini. Katika uwekezaji huo Naibu waziri amewataka wawekezaji hao kufanya mabo yafuatayo ili kukamilisha tarabu za uwekezaji, kwanza wakitembelee kituo cha uwekezaji (Tanzania Investment Centre), kwa ajili ya kupata mwongozo wa uwekezaji. Pia wawekezaji hao wawe tayari kuwashirikisha wakulima katika shughuli zao na wawe tayari kuwa na kilimo cha mkataba kitakachomwezesha mkulima kuwa na uhakika wa kipato chake. Akiongea kwa niaba ya wenzake Bw. Patrick Chiles alisema kuwa, mradi wao ‘AFRICA HARVEST OF HOPE’ unakusudia kwekeza Tanzania katika zao la korosho, baada ya kuona kuwa zao hili linazalishwa Tanzania lakini sehemu kubwa inasindikwa nchini India na kuuzwa nchi zingine, hivyo wameona ni vizuri korosho isindikwe hapa hapa Nchini. Walitoa ahadi kwamba watafuata taratibu zote za uwekezaji,, kununua korosho nyingi kwa ajili ya kuongeza ajira ya muda mrefu, ambapo wamesma wamesea pia kuwa Taasisi yao haitakuwa ya kutengeneza faida kubwa.
|
||||||||
DRD Yadhamaria Kusajili Watafiti
Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti na Maendeleo Dkt. Fidelis Myaka
Idara ya Utafiti na Maendeleo imedhamiria kuweka mkakati wa kuwasajili watengeneza mbegu (Breeders) ili kuwabana wale ambao hawana sifa kama njia ya kuboresha upatikanaji wa mbegu bora. Azimio hilo lilifikiwa na Wajumbe wa Mkutano wa Kitaifa wa Utafiti wa mbegu uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Safari uliopo mjini Arusha hivi karibuni. Katika Mkutano huo, Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti na Maendeleo Dkt. Fidelis Myaka pamoja na Watafiti wengine, wamedhamiria kuanzisha mkakati wa usajili wa wazalisha mbegu baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wakulima na baadhi ya Kampuni za kuzalisha mbegu walidai kuwapo mbegu ambazo zina kiwango duni na kukosa sifa kadhaa. Katika usajili huo utaonyesha viwango vya kitaaluma anavyotakiwa kuwa navyo mzalishaji wa mbegu na aina za mazao ambazo anatafiti. Dkt. Myaka aliendela kusema kuwa Idara itafanya ukaguzi wa Taasisi za utafiti kubaini kama kuna aina za watafiti wasiokidhi viwango ikiwa ni jitihada za kuimarisha uzalishaji wa mbegu. “Kwa kufanya hivi itasaidia kuwarekebisha baadhi ya Watafiti ambao wanataaluma tofauti na mbegu wanazozizalisha alisema Dkt. Myaka. Naye Mwenyekiti wa Mkutano huo Bwana Geoffrey Kirenga amesema Usajili huo utamuweka huru mzalishaji mbegu atakayeamua kuzalisha mbegu tofauti na fani yake kusomea ili kupata taaluma husika, aliongeza kuwa kuwasajili wazalisha mbegu kutaliwezesha taifa kuzalisha mbegu zenye ubora na hatmae kuchangia katika kuinua kilimo alisisitizwa, Bwana Kirenga |
||||||||
Jumuia ya Ulaya Kuendelea Kusaidia Sekta ya Kilimo
Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe na Balozi wa Jumuia ya Ulaya, Bwana Tim Clarke ofisini kwake Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa, Profesa Jumanne Maghembe amekutana na Balozi wa Jumuia ya Ulaya, Bwana Tim Clarke ofisini kwake hivi karibuni na kuzungumza masuala yanayohusu sekta ya kilimo nchini na namna ya kudumisha na kuendeleza ushirikiano baina ya Tanzania na Jumuia ya Ulaya. Balozi Clarke alimueleza Waziri Maghembe kuwa Jumuiya ya Ulaya imedhamiria kuendeleza zao la kahawa na mazao mengine kupitia programu mbalimbali zinazotekelezwa na Jumuia ya Ulaya Barani Afrika. Balozi Clarke aliainisha miradi ambayo Jumuiya hiyo inatilia mkazo kuwa ni pamoja na ule wa kuendeleza kilimo cha miwa uliogharimu Euro milioni 6, Progarmu ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo, ASDP Euro Milioni 32, utafiti wa zao la chai, Euro milioni 2 na Utafiti kwa kahawa Euro milioni 2. Balozi Clarke aliongeza kuwa Euro milioni 30 zipo tayari kusubiri utekelezaji na kuongeza kuwa Jumuia hiyo imeisaidia Tanzania kiasi cha Euro milioni 50 zilizowekezwa kwenye kilimo tu. “Jumuia ya Ulaya imetenga Euro bilioni 1 kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa chakula barani Afrika na katika mgao huo Tanzania itapata Euro milioni 32” alikaririwa Balozi Clarke. Balozi Clarke aliongeza kuwa Jumuia ya Ulaya inafadhiri miradi nane nchini ukiwemo ule wa Tanzania Agricultural Partnership – TAP ambao utatekelezwa kati ya Serikali na Jumuia hiyo katika kuendeleza sekta ya kilimo kwa kuangalia eneo la usalama wa chakula, virutubisho (nutritions) na kujenga uwezo wa wataalam katika Vyuo vya Mafunzo kama vile Tengeru alisema mwakilishi huyo wa Jumuia ya Ulaya. Kwa upande wake Waziri Maghembe alimueleza mwakilishi huyo nia ya Serikali katika kuhakikisha kilimo cha Tanzania kinakuwa cha kisasa, chenye tija na enedelevu kinacholenga kubadili maisha ya wakulima wadogo na wakubwa na kukuza uchumi wa Taifa kwani asilimia 85 ya Watanzania wanajihusisha na kilimo. |
||||||||
Naibu Waziri atembelea Mkoa wa kigoma
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Eng. Christopher Chiza akitoa maelekezo kwa mafisa wa wilaya ya Kibondo Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Eng. Christopher Chiza hivi karibuni alimaliza ziara ya kikazi ya siku sita katika Mkoa wa Kigoma katika Wilaya za Kigoma Vijijini, Kibondo,na Wilaya mpya ya Kakonko. Katika ziara hiyo Naibu Waziri alifanya ufuatiliaji wa utekelezaji wa usambazaji pembejeo ya ruzuku ikiwa ni pamoja na kupata maelezo na changamoto zilizojitokeza katika utaratibu mzima wa usambazaji wa pembejeo hizo. Moja ya changamoto kubwa iliyoelezwa na baadhi ya wakulima, ni kwa wakulima kuweka sahihi kwenye vocha bila ya kuchukua pembejeo husika kutokana na kutokuwa na uwezo wa kulipia pembejeo zikiwemo mbegu bora na mbolea Aidha Mhe. Eng. Chiza aliuagiza uongozi wa wilaya husika kufanya ufuatiliaji wa karibu katika zoezi zima la usambazaji wa pembejeo ili kubaini baadhi ya mawakala ambao sio waaminifu. Katika ufuatiliaji huo kila mkulima aliyeweka saini kwenye vocha itabidi athibitishe kuwa alipokea pembejeo, na kasha kuonyesha shamba lake zilipotumika pembejeo hizo. Mhe Eng. Chiza vile vile alipata fursa ya kutembelea wakulima wa zao la kahawa katika kijiji cha Muhange , Shughuli za kilimo cha umwagiliaji na katika kijiji cha Nyamtukuza na Kituo cha mpakani cha Mabamba katika wilaya ya Kibondo kinachoshughulikia Ukaguzi wa Mazao na Afya ya Mimea. |
||||||||
Tanzania na Israel Kuendeleza Mahusiano
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bwana Mohamed Muya na Balozi wa Israel Afrika ya Mashariki, Bwana Jacob Keidar ofisini kwake hivi karibuni Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bwana Mohamed Muya amesema nia ya Serikali ni kukuza na kuboresha kilimo ili sekta hiyo iwe ya manufaa Kitaifa na Kimataifa. Akizungumza na Balozi wa Israel wa Afrika ya Mashariki Bwana Jacob Keidar ofisini kwake hivi karibuni, Bwana Muya alisema kilimo kitaboreshwa kwa mikakati mbalimbali kama Kauli Mbiu ya KILIMO KWANZA na Mpango wa Maendeleo ya Kilimo Kusini mwa Jangwa la Sahara kupitia fursa za Tanzania unaojulikana kama (Southern Agricultural Corridor of Tanzania - SAGCOT) ambao ilizunduliwa na Waziri Mkuu Mheshimiwa, Mizengo Pinda wiki mbili zilizopita. Akizungumzia Azimio la KILIMO KWANZA, Bwana Muya alisema Kauli Mbiu hiyo ina dhamira ya kubadili kilimo kutoka kilimo cha kujikimu na kuwa cha kisasa na cha kibiashara kwa kushirikiana na sekta binafsi ili isaidie kuwekeza hasusan kwenye upatikanaji wa mbegu bora za kilimo na si kuiachia Serikali peke yake. Aliongeza kuwa mahitaji ya mbegu kwa wakulima wa Tanzania ni tani 120,000 kwa mwaka na uwezo wa ndani wa kuzalisha mbegu ni jumla ya tani 6,000 tu ambazo hazitoshelezi. “Kwa sasa tuna uwezo wa kuzalisha tani 6,000 tu za mbegu bora ambazo hazitoshi kwani mahitaji halisi kwa mwaka ni tani 120,000”. Alikaririwa Bwana Muya. Katibu Mkuu alieleza nia ya kuboresha sekta ya kilimo kwa kupitia kilimo cha umwagiliaji na kuhama kutoka matumizi ya jembe la mkono ambalo linatumia muda mwingi na uzalishaji mdogo na kuboresha miundombinu kama barabara ili kuwawezesha wakulima kusafirisha na kuuza mazao yao kwa urahisi. Naye Meneja wa Kampuni ya Balton, Tanzania Bwana Ilan Hanegbi alisema, Kampuni hiyo imejikita zaidi kwenye uuzaji wa miundombinu na mitambo ya kilimo cha umwagiliaji maji mashamba hususan umwagiliaji wa matone (Drip irrigation). |
||||||||
Marekani Kuisaidia Tanzania Katika Sekta ya Kilimo
Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe (kushoto) akiwa na Balozi wa Marekani nchini, Bwana Alfonso Lenhardt (kulia) Marekani imeahidi kuendelea kuisaidia Tanzania katika sekta mbalimbali hususan Kilimo. Hayo yemesemwa na Balozi wa Marekani nchini, Bwana Alfonso Lenhardt alipokutana na Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mhe. Prof. Jumanne Maghembe jana akiambatana na ujumbe maalum kutoka Marekani. |
||||||||
Speeches| Publications | Agricultural Statistics | Legislation and Regulations | About us|Contact us
Copyright 2008, Ministry of Agriculture Food Security and Cooperatives All rights reserved. |
||||||||