|
| |
|
|
|
Taratibu na Masharti ya Mikopo ya Pembejeo za Kilimo na
Mifugo
|
|
-
Waombaji wa mikopo ya pembejeo watatakiwa kujaza
fomu maalim za maombi
zinazopatikana kwenye Halmashauri za Wilaya husika. Afisa
kilimo wa Wilaya husika atathibitisha shughuli za mwombaji pamoja na
vielelezo vinavyohitajika kabia ya kuzipitisha. Fomu zilizokamilika
na kupiitshwa na Afisa Kilimo wa Wilaya, zitaidhinishwa pia na Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya kabia ya kutumwa kwa Mkurugenzi Mtendaji
wa Mfuko wa
Pembejeo. Ili maombi haya yashughulikiwe ipasavyo inashauriwa yawasilishwe
mapema
katika muda maalum kama ifuatavyo:-
 |
Maombi kutoka mikoa ya Ruvuma, Rukwa,
Mbeya, Iringa, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, Kigoma, Kagera, Mara
na Mwanza yatumwe kwa Mkurugenzi wa Mfuko wa Pembejeo katika kipindi cha
kati ya mwezi Machi
hadi Juni. |
 |
Maombi kutoka mikoa ya Arusha,
Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro,Mtwara, Lindi na Dar es salaam
yatumwe kwa Mkurugenzi wa Mfuko wa Pembejeo katika kipindi cha kati ya
mwezi Julai hadi Septemba. |
Maombi ya wauza pembejeo binafsi,
wakulima na wafugaji binafsi sharti watimize masharti yafuatayo:-
 |
Wawe na dhamana binafsi
isiyohamishika yenye hati miliki (title deed) na inayokubalika kisheria. |
 |
Watatakiwa kutekeleza masharti ya mikopo ya benki au taasisi nyingine ya
kifedha itakayotoa mikopo kwa niaba ya Mfuko wa Pembejeo ikiwa ni pamoja
na kufungua akaunti na benki husika na
kulipa asitimia moja ("1%) ya mkopo kabia
mkopo haujaidhinishwa na
kutolewa. |
-
Maombi ya Mifuko ya Pembejeo ya Wilaya
isiyo na dhamana zenye hati miliki sharti idhaminiwe na Halmashauri za
Wilaya husika.
-
Maombi ya Vyama vya kuweka na kukop (SACCOS),
vikundi vya wakulima na wafugaji visivyo na dhamana za hati miliki sharti
viwe wanachama wa Shirikisho la Vyama vya Kuweka na Kukopa Tanzania (SCCULT,
1992 Ltd.). Kiasi cha mkopo utakaotolewa ni mara tatu ya akiba ya mwombaji
itakayowekwa SCCULT, (1992) Ltd. kama dhamana.
|
|
|
| |
|