Home Up Feedback Search

Loan For New Tractors
Home Up

Soma kipeperushi cha kuhusu mikopo ya pembejeo

       

United Republic of Tanzania, Ministry of Agriculture, Food Security & Corperatives, Agricultural Inputs Trust Fund. AGITF.  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Mfuko wa Pembejeo.

Taratibu na Masharti ya Mikopo ya Kununua Trekta Jipya

 

1. Mwombaji atajaza fomu maalum ya maombi inayopatikana katika Ofisi za kilimo za Halmashauri za Wilaya na Makao makuu ya Mfuko wa Pembejeo, jijini Dar-es-salaam na katika tovuti yetu.

2. Fomu   za   maombi   zilizojazwa   na kuambatanishwa na vielelezo vinavyohitajika zitapitishwa/kuidhinishwa na Afisa Kilimo wa Maendeleo ya Mifugo wa Wilaya na Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya husika na baadaye kutumwa mapema kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Pembejeo.

3. 3. Mikopo ya kununua matrekta  inapitia benki, mwombaji sharti atimize yafuatayo:-

  1. Awe na dhamana binafsi kwa jina lake isiyohamishika yenye hati rriliki (title deed) na inayokubalika kisheria.

  2. Awe tayari kutekeleza masharti ya mikopo ya benki itakayotoa mikopo kwa  niaba ya Mfuko wa Pembejeo ikiwa ni pamoja na kufungua akaunti na benki husika, kulipa asilimia moja ya mkopo kabla haujatolewa na kusajili trekta kwa jina lake na benki au taasisi ya fedha itakayotoa mkopo.

  3. Awe tayari kulifanyia matengenezo madogo   na   makubwa   trekta  litakalonunuliwa kwa mkopo mara kwa mara kama atakavyoelekezwa na mtengenezaji au muuzaji wa trekta hilo.

4. Muda wa mkopo ni miaka mitatu kwa riba ya asilimia kumi (10%)

 

 

Send mail to agitf@mari.or.tz with questions or comments about this web site.
Last modified: 03/06/07