Wizara Kununua Mazao ya Nafaka Nchini
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imetangaza nia yake ya kutaka kununua mazao ya nafaka ili kumwekea mkulima wa hali ya chini soko la uhakika.
Miongoni mwa mazao yatakayonunuliwa kupitia Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ni mpunga,maharagwe,karanga,choroko,ulezi,ufuta na mahindi,na yatanunuliwa kwa bei ya ushindani ya soko mwaka huu.
Hayo ni kwa mujibu wa Mchumi wa bodi hiyo Bw. Edwin Mkwenda katika maonesho ya wakulima yaliyofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni Manispaa ya Dodoma.
Bw. Mkwenda alisema tayari Serikali imeikabidhi bodi hiyo maghala yote yaliyokuwa ya Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC),ambayo hayakubinafsishwa zilizoko kwenye kanda saba ili kutunza mazao yatakayonunuliwa.
Kuundwa kwa bodi hiyo ni ukombozi kwa wakulima kwani watakuwa na uhakika wa kupata soko la mazao husika.