Skip to main content
Habari na Matukio

Waziri na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza Baraza jipya la Mawaziri ambalo lina jumla ya Mawaziri 19 na Naibu Waziri 15.

Katika Baraza hilo, iliyokuwa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imeunganishwa na iliyokuwa Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi na kuwa Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi.

Katika Baraza hilo jipya la Serikali ya Awamu ya Tano lililotangazwa, Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) amekuwa Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, wakati Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, ni Mhe. William Tate Ole Nasha (Mb).

Watumishi wa Wizara wamepongeza na kuwakaribisha sana Viongozi hao Wakuu.

Wakiongea kwa nyakati tofauti, Bwana Rashid Likiligo wa Kitengo cha Mifumo ya Kopyuta, amesema, “Uteuzi aliofanya Mhe. Rais Magufuli ni mzuri na umelenga kuleta ufanisi katika Wizara hasa kwa kuzingatia uchapakazi wa viongozi hao”.

Naye Caltas Kabyemela wa Idara ya Utafiti na Maendeleo alisema, “Nimependa uteuzi huo, hao wote waliochaguliwa ni wachapakazi na naamini Wizara yetu mpya itafanikiwa na kuwa na maendeleo yatakayoonekana kwa wananchi ambao ni zaidi ya asilimia 75 ya Watanzania”.