Changamoto za Pamba kupatiwa Ufumbuzi
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bwana Zidikheri Mundeme amewataka wadau wa zao la pamba kuwalinda wakulima wadogo wa zao hilo kwa kuwapatia pembejeo za kilimo kama mbegu bora na viuatilifu kwa wakati ili kuboresha zao hilo.
Bwana Mundeme alitoa wito huo, wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau wa zao hilo kutoka nchini Kenya, Brazili na Tanzania, ambapo washiriki wa Tanzania walitoka katika Vituo vya Utafiti wa Mazao. Mkutano huo ulianza mapema wiki hii katika Hoteli ya Whitesands.
"Kilimo cha mkataba, ukosefu wa soko na uongezaji thamani wa zao hilo na kipato kidogo kwa wakulima wa zao hilo ni baadhi ya changamoto zinazomkabili mkulima mdogo wa pamba. Alieleza Bwana Mundeme
"Washiriki wa mkutano huo wanapaswa kujadili kwa kina namna ambavyo watatoa majibu ya changamoto hizo". Alikaririwa, Bwana Mundeme.