Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bw. Andrew Massawe Akutana na Menejimenti ya Wizara.
Katibu Mkuu wizara ya Kilimo Bw. Andrew Massawe leo amekutana na Manejimenti ya wizara hiyo katika ukumbi wa mikutano wa kilimo IV uliopo Mjini Dodoma lengo likiwa kuwashukuru watumishi kwa ushirikiano waliouonesha tokea alipo apishwa mpaka siku ya leo.
Akiongea wakati wa kufungua kikao hicho Katibu Mkuu amewataka wakuu wa Idara na Vitengo kuhakikisha wanatekeleza maagizo ya Rais Mhe. Samia Suluhu aliyoyatoa hivi karibuni alipokuwa anawaapisha Makatibu Wakuu ya kutatua changamoto za masoko ya mazao ya wakulima