Mbegu Zisizokizi Viwango ni Kikwazo katika Kumuinua mkulima
Utumiaji wa mbegu zisizokidhi viwango umechangia uzalishaji mdogo wa mazao kwa wakulima wengi hapa nchini.
Akiongea na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika maonesho ya nanenane yaliyofanyika katika viwanja vya nzuguni ,Dodoma Afisa masoko wa wa taasisi ya uzalishaji wa mbegu ASA bib Jacquiline Itatiro amesema, matumizi ya mbegu feki yanatokana na na uwezo mdogo wa wakulima….. ukilinganisha na mahitaji, elimu ya matumizi za mbegu bora kwa wakulima pamoja na wasambazaji wa mbegu feki ambao sio waaminifu wanajitokeza kuuza mbegu zisizo na viwango katika kukidhi mahitaji ya mazao.
Aidha alisema usambazaji na uhamasishaji wa matumizi ya mbegu bora kwa kushirikiana na sekta binafsi katika kuzalisha, kumechangia kumhamasisha mkulima kutumia mbegu hizo ambazo kwa kiasi kikubwa zimeleta tija.
Hata hivyo alibainisha kwamba pamoja na kushirikiana na vituo vya utafiti kuhakikisha mbegu mpya zinazalishwa na zinamfikia mkulima bado miundombinu ya umwagiliaji maji mashambani imeendelea kuwa tatizo kwa wakulima hivyo kutegemea kilimo cha mvua za msimu.