Hassunga Aendesha Mkutano wa Uandaaji wa Sera Mpya ya Kilimo
Waziri wa Kilimo Mhe. Japheti Hassunga leo (16.09.2019) amekutana na Menejimenti ya wizara,wakuu wa Taasisi na Wenyeviti wa Bodi za Mazao zilizopo chini ya Wizara.
Lengo la mkutano huu wa siku mbili unaofanyika katika ukumbi wa wizara Jijini Dodoma ni kujadili taarifa za utekelezaji za mwaka mwaka 2018/2019 na maoni kujadili uandaaji wa sera mpya ya kilimo ya mwaka 2019
Akiongea katika kikao kazi hicho Mhe. Waziri Hasunga ameeleza umuhimu wa sera hiyo unalenga kukifanya kilimo kuwa na tija na cha kibiashara sera hivyo kuleta maendeleo makubwa katika sekta ya kilimo
Mhe. Waziri amebainisha kwamba sera hiyo inatakiwa kukamilika mapema mwaka huu ili kutoa fursa ya kuandaa sheria na kanuni za kilimo.
Kikao hicho kinahudhuriwa na Manaibu Waziri Hussein Bashe na Omary Mgumba,Katibu Mkuu Mhandisi Mathew Mtigumwe na Naibu Katibu Mkuu Prof.Siza Tumbo.
Mwisho.