ASDPII Kuleta mabadiliko makubwa ya Sekta ya Kilimo
Programu ya kuendeleza sekta ya kilimo awamu ya pili (ASDPII) imejipanga kuimarisha matumizi ya maji, kuongeza uzalishaji na tija, uongezaji wa thamani za mazao na kutengeneza mazingira wezeshi
Akiongea kwenye Kituo cha Taifa cha Matangazo cha TBC -1 wakati wa kipindi cha Tunatekeleza kinachorushwa kila siku ya Alhamisi Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Dkt.Charles Tizeba amesema Tanzania kuna mvua za kutosha lakini hapakuwa na utaratibu wa kuyahidhi maji yasipotee lakini ASDPII imekuja na kipaumbele cha matumizi bora ya maji, kuongeza uzalishaji na tija, uongezaji wa thamani za mazao na kutengeneza mazingira wezeshi.
Aidha ifikapo 2021 kupitia program ya uendelezaji wa kilimo endapo ikitekel;ezwa vizuri kilimo kitachangia kwenye ukuaji wa uchumi kwa zaidi ya 40% ikilinganishwa na 29 ya sasa alisema Mheshimiwa Charles Tizeba.
Tofauti na mwanzo kwa sasa ASDP II imewahusisha Wizara ya Kilimo,Maji na umwagiliaji, Mifugo na Uvuvi TAMISEMI na wadau wa wote wa kilimo ili kuhakikisha kuwa kilimo kinazalisha malighafi za kutosha katika kipindi hiki cha uchumi wa viwanda alisistiza Dkt. Tizeba.