DRD Yadhamaria Kusajili Watafiti
Idara ya Utafiti na Maendeleo imedhamiria kuweka mkakati wa kuwasajili watengeneza mbegu (Breeders) ili kuwabana wale ambao hawana sifa kama njia ya kuboresha upatikanaji wa mbegu bora.
Azimio hilo lilifikiwa na Wajumbe wa Mkutano wa Kitaifa wa Utafiti wa mbegu uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Safari uliopo mjini Arusha hivi karibuni.
Katika Mkutano huo, Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti na Maendeleo Dkt. Fidelis Myaka pamoja na Watafiti wengine, wamedhamiria kuanzisha mkakati wa usajili wa wazalisha mbegu baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa wakulima na baadhi ya Kampuni za kuzalisha mbegu walidai kuwapo mbegu ambazo zina kiwango duni na kukosa sifa kadhaa.
Katika usajili huo utaonyesha viwango vya kitaaluma anavyotakiwa kuwa navyo mzalishaji wa mbegu na aina za mazao ambazo anatafiti.
Dkt. Myaka aliendela kusema kuwa Idara itafanya ukaguzi wa Taasisi za utafiti kubaini kama kuna aina za watafiti wasiokidhi viwango ikiwa ni jitihada za kuimarisha uzalishaji wa mbegu. “Kwa kufanya hivi itasaidia kuwarekebisha baadhi ya Watafiti ambao wanataaluma tofauti na mbegu wanazozizalisha alisema Dkt. Myaka.
Naye Mwenyekiti wa Mkutano huo Bwana Geoffrey Kirenga amesema Usajili huo utamuweka huru mzalishaji mbegu atakayeamua kuzalisha mbegu tofauti na fani yake kusomea ili kupata taaluma husika, aliongeza kuwa kuwasajili wazalisha mbegu kutaliwezesha taifa kuzalisha mbegu zenye ubora na hatmae kuchangia katika kuinua kilimo alisisitizwa, Bwana Kirenga