Skip to main content
Habari na Matukio

Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima –Nane Nane Mwaka 2017

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi anatangazia umma kuwa Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Wakulima – Nane Nane mwaka 2017, ngazi ya Ki-Taifa zitaadhimishwa katika Uwanja wa Maonesho ya Kilimo wa Ngongo, Manispaa ya Lindi. Maandalizi na maonesho hayo yanaratibiwa na Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na uongozi wa Mikoa ya Lindi na Mtwara.

Uratibu wa maonesho ya mwaka huu ngazi ya Ki-Taifa unafanywa na Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi kwa kuwa Taasisi ya Kilimo Tanzania (TASO) iliyokuwa inaratibu maandalizi na maonesho ya Wakulima (Nane Nane) miaka ya nyuma imefutiwa usajili wake mwezi Mei 2017. Washiriki wa maonesho ya kilimo na sherehe za Ki-Taifa wawasiliane moja kwa moja na Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi au Sekretarieti za Mikoa ya Lindi na Mtwara.

Aidha, maadhimisho ya Ki-Kanda yatafanyika katika  viwanja vya maonesho ya John Mwakangale –Mbeya; Mwalimu J.K. Nyerere –Morogoro; Themi – Arusha; Nzuguni -  Dodoma; Nyahongolo – Mwanza; na Fatuma Mwassa - Tabora. Maandalizi na maonesho ya  Ki-Kanda yanaratibiwa na uongozi wa  mikoa husika. Washiriki wa maadhimisho ya Ki-Kanda wanatakiwa kuwasiliana na Sekretarieti za Mikoa husika ili kupata maelekezo na taratibu zingine za ushiriki.

Hivyo kuanzia sasa utaratibu wa maandalizi na maonesho ya sherehe za wakulima (Nane Nane) ni kama ulivyotolewa katika tangazo hili. Maelezo zaidi kuhusu maonesho ya kilimo na sherehe za wakulima yataendelea kutolewa kupitia njia zifuatazo:-

www.kilimo.go.tz;

www.tzagriculture.blogspot.com;

www.facebook.com/tzagriculture;  na

www.twitter.com/tzagriculture

WOTE MNAKARIBISHWA