Skip to main content
Habari na Matukio

Muswada wa Umwagiliaji Wapitishwa

Muswada wa umwagiliaji(The National Irrigation Act, 2013)  uliowasilishwa na waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mh. Eng. Christopher Chiza bungeni hivi karibuni hatimaye umepitishwa.

Akihitimisha katika hotuba yake waziri wa kilimo chakula na ushirika amesema muswada huo wa umwagiliaji utatatua matatizo na changamoto zinazoikumba sekta ya kilimo cha umwagiliaji na  utaleta mafanikio makubwa katika kilimo cha umwagiliaji Tanzania.

Aidha akichangia katika muswada huo, Mbunge wa Busega, Titus Kamani, alisema pamoja na Watanzania zaidi ya asilimia 80 kutegemea kilimo, taifa limekuwa likiishia kukosa chakula, na akasema sheria hiyo imecheleweshwa ili kujibu matakwa ya wakulima.

“Muswada huu umechelewa, lakini ni heri umeletwa na sheria ikipitishwa itakuwa ni neema kwa mikoa ambayo hukumbwa na ukame wa mara kwa mara. Kwa kuwa kilimo cha umwagiliaji, kitasaidia kuinua kilimo na kuongeza tija kwa wakulima,” alisema.

Hata hivyo, alitaka kujua fedha za uendeshaji wa Tume itakayosimamia umwagiliaji zitatoka wapi, kwa kuwa uhaba wa fedha umekuwa ukikwamisha mipango mizuri ya serikali.

Mbunge wa Mbarali, Modesti Kirufi akichangia muswada huo, alisisitiza kuwepo na mkakati wenye kuwakomboa si wakulima tu, bali hata wafugaji kwa kile alichodai kama sheria itapita, itawakomboa wakulima kutoka utegemezi wa mvua