Skip to main content
Habari na Matukio

Sensa ya Kilimo Kufanya Nchi Nzima- Ruboha

Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanajiandaa kufanya sensa ya kilimo nchi nzima lengo likiwa ni kukusanya taarifa mbalimbali za Kilimo.

Akiongea na Kitengo cha Mawasiliano  Serikalini Mkurungezi Msaidizi wa Ufuatiliaji  Tathimini na Takwimu Bwana Oswald Ruboha walipokutana ofisini kwake hivi karibuni amesema, sensa hiyo inategemewa kuanza mwaka ujao wa fedha ili kupata taarifa mbali mbali za kilimo.

Aidha, Wizara za Kisekta zikiwemo Wizara ya Kilimo, Wizara ya Mifugo, Wizara ya Viwanda na Biashara, na Tamisemi zitashiriki kikamilifu katika Sensa hiyo ambapo wasimamizi wakuu ni Ofisi Taifa ya Takwimu, alisema Bwana Ruboha.

Alisisitiza kwamba sensa hiyo itagharimu kiasi cha fedha za Kitanzania bilioni 11,129,742,319 ambapo umoja wa Ulaya (EU) wametoa shilingi bilioni 5.24 kwa ajili ya sensa hiyo na kiasi kilichobaki Wizara zitatakiwa kuchangia.

kwa upande mwingine Bwana Ruboha. ametoa wito kwa  watumishi na wadau wote wa kilimo kutumia  mfumo wa kielekitroniki wa  ufuatiliaji na tathimini ambao umekwisha kamilika  kwa matumizi na upatikanaji wa takwimu mbalimbali za kilimo

timu kutoka kurugeni hiyo inajipanga kutoa wasilisho kwa menejimenti na watumiaji wa twakwimu kwa namna  ambavyo mfumo huo utafanya  kazi alisema Bwana Ruboha.

Aidha katika mfumo huo  zipo fomu ambazo  zinatumika kukusanya takwimu za kila  mwezi, kila robo mwaka  na kila mwaka ambapo zitawasaidia  wataalamu katika tafiti mbalimbali na uimarishaji wa sekta ya kilimo .  alisema bwana Ruboha.

hata hiyo mfumo huo ambao utatumika kufanya ufuatiliaji na tathimini ya ASDP II umeandaliwa kwa kuweza kutoa taarifa kutoka kila Kata nchi nzima ambazo hutumika kuandaa taarifa za kila Wilaya na  Mkoa ili kupata takwimu za kitaifa alisistiza Bwana Ruboha.