Skip to main content
Habari na Matukio

Siku ya Wakulima wa Mpunga Makifu Yafana

Juhudi za Serikali kuzalisha mpunga kwa Wingi zimeanza kuonekana kwa wakulima wa kijiji cha Makifu, Wilaya ya Iringa, katika mkoa wa Iringa. Hali hiyo ilijidhihirisha katika maadhimisho ya siku ya wakulima iliyofanyika kijijini hapo katika skimu ya umwagiliaji ya Makifu. Katika siku hiyo Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Bi. Wamoja Ayoub alikuwa mgeni rasimi.