Skip to main content
Habari na Matukio

Waziri Nchemba atoa wito kwa wakulima wa mihogo kuchangamkia fursa ya kuzalisha zao hilo kwani soko

Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba alitoa wito huo kwa Wakulima waktia wa mazungumzo ya kikazi na Balozi wa Ubeligiji nchini Mheshimiwa Paul Cartier wakati alipomtembelea ili kujitambulisha na kumpongeza.

Waziri Nchemba alisema lengo la Serikali ya Awamu ya Tano ni kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo na mkazo umewekwa kuongeza uzalishaji na uongezaji wa thamani mazao ya kilimo.

Waziri Nchemba alimwambia Balozi Cartier kuwa Serikali imedhamiria kubadilisha hali ya uchumi ya Watanzania wa kipato cha chini na cha kati na kwa maana hiyo mkazo ni kuongeza uzalishaji ambao kwa kipindi kirefu umekuwa ndiyo tatizo.

Waziri Nchemba amesema kwenye suala la ubora kwa zao hilo si tatizo kwani Serikali kupitia Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi imejenga mahabara ya kisasa kwa ajili ya kuzalisha vipando bora na kwamba watafiti katika Kanda ambazo mihogo imekuwa ikizalishwa, wamekuwa wakizalisha vipando bora na vya kutosha kwa ajili ya kutosheleza wakulima wengi. 

Waziri Nchema alimuakikishia Balozi huyo kuwa Mikoa ya Pwani, Kanda ya Ziwa na Ukanda wa Ziwa Tanganyika uzalishaji utaongezeka mara dufu kwamba ni nafasi ya Wakulima kuchangamkia fursa ya kulima zao hilo kwa wingi kwani soko lipo na uhakika.

Awali Bibi Margareth Ndaba Mkuu wa Kitengo cha Mahusiano ya Kimataifa, Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi alimueleza Waziri Nchemba kuwa Tanzania imepokea maombi ya kuuza mihogo yake nchini China na kuongeza kuwa ni fursa kwa Wakulima wa Tanzania kuichanghamkia fursa hiyo kwani kiwango kinachotakiwa ni kikubwa ukilinganisha na uzalishaji