Skip to main content
Habari na Matukio

Wizara Yapata Mawaziri Wapya

Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imepata Mawaziri wapya baada ya kuhamishwa wizara aliyekuwa waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika Mheshimiwa Prof Jumanne Maghembe na kuwekwa  Mhandisi Christopher Chiza ambaye hapo mwanzo alikuwa ni Naibu waziri wa wizara hii.

 Mheshimiwa Adam Malima ambaye hapo mwanzo alikuwa Naibu waziri wa wizara ya Nishati na madini kwa sasa ndiye Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika.

Mabadiliko hayo yamekuja hivi karibuni baada ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri siku ya tarehe 4 Mei mwaka huu Ikulu jijini Dar es Salaam na kuunda baraza jipya.

Baada ya kufika wizarani kutokea Ikulu walipokuwa wanaapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Mawaziri hao waliongea na wakurukungezi na wakuu wa Idara na Vitengo ambapo Waziri mpya wa Wizara ya kilimo Chakula na Ushirika Mhandisi Christopher Chiza alisisitiza kuimarishwa ushirikiano baina ya wafanyakazi ili kufikia malengo walijiwekea

 “Ushirikiano ni chombo kitakacho tupeleka sehemu tunayotaka kwenda ,hivyo ni muhimu kuimarishwa ushirikiano baina yetu ili kuziimarisha huduma zetu. Kila mtumishi asimamie majukumu yake kikamilifu na kwa kufanya hivyo ndipo tutakapo weza kufikia malengo yetu” alifafanua Mhandisi Christopher Chiza.

Kwa upande wake Naibu  Waziri  Mheshimiwa Adam Malima amewataka watumishi wote pamoja nakutekeleza majukumu kiufasaha kuwepo na uwazi katika utendaji wa kazi kama njia rahisi ya kutatua matatizo.

“Uwazi ni jambo zuri sana katika utendaji wa kazi, kwani utatuwezesha kutatua matatizo mbalimbali yatakayokuwa yanatukabili alisema Mheshimiwa Adam Malima.