AMAGRO Yakabidhiwa Vifaa vya Kupambana na Nzi wa Embe
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika imekabidhi vifaa vya kupambana na Nzi wa embe kwa Chama cha Wakulima wa Embe (AMAGRO) ili kuboresha kilimo cha embe hapa nchini, hafla hiyo ilifanyika katika kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Mikocheni kilichopo Jijini Dar es Salaamu.
Awali Mratibu wa Mradi wa Udhibiti Nzi wa waharibifu wa matunda kutoka kitengo cha Afya ya Mimea cha Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Janet Muganyizi alifahamisha kuwa vifaa hivyo vimetoka Kituo cha Kimatasifa cha kuthibiti Wadudu waharibifu (ICIPE) chenye makao makuu yake Nairobi nchini Kenya.
Kwa mujibu wa Muganyizi kituo hicho pia kilitoa mafunzo kwa wakulima huko Kibaha mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya msaada wa kituo hicho kuboresha kilimo cha embe hapa nchini miongoni mwa wakulima wa Tanzania.
“Jumla ya wakulima 150 toka ktika mikoa 15 watanufaika na msaada huo muhimu wa kukabiliana na Nzi wa Embe mingoni mwa wakulima wa zao hili” alifahamisha Muganyizi katika hotuba yake ya kumkaribisha mgeni rasmi.
Aliitaja baadhi ya mikoa hiyo kuwa ni Mbeya, Dar es Salaamu, Pwani, Morogoro, Tanga, Tabora, Dodoma, Mwanza , Iringa, Kilimanjaro, Songea, Arusha na Lindi.
Vifaa vilivyokabidhiwa katika hafla hiyo kuwa ni lita 20 za kivutia madume, lita 40 za chambo na mitego 3,000, vikiwa na thamani ya Dola za Kimarekani 6,071 ambayo ni sawa na zaidi ya 9,700,000 zikiwa gharama za ununuzi, alifahamisha Muganyizi.
Naye mgeni rasmi katika hafla hiyo ya makabidhiano ya vifaa hivyo Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao toka Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika Bwana Beatus Malema aliwataka wakulima wa embe walionufaika na msaada wa vifaa hivi kuwa viwe ni mchangamoto katika kuboresha uzalishaji wa embe zenye ubora ili kuweza kushinda na kupata nafasi katika soko la Afrika Mashariki na Dunia.
“Huu ndio mwanzo kwa ndugu zangu wakulima kuboresha zao la embe ili tuweze kupiga hatua na kupata soko la uhakika kwa maufaa yetu wenyewe” aliongeza Malema
Malema aliwataka wakulima kufuata misingi bora ya uazalishaji wa zao hili ikiwemo usafi katika shamba, kutumia wadudu rafdiki wa mkulima wanaoshambulia Nzi hawa na kwa kutumia mitego ya kunasa Nzi wa embe.
Pia aliwataka wakulima kuyatumia mafunzo wanayopata toka kwa watalaamu wa kilimo ili kuboresha zao hili la embe kwani vinginevyo wataishia kulima kilimo kisicho na tija.
“Tukiamua kufanya kweli kuboresha zao la embe tunaweza kubadili maisha yetu na kutoka hapa tulpo katika maisha yetu” Malema aliwasisitiza wakulima hao.
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Embe hapa nchini ndugu Burton Nsape aliishukuru sana serikali kwa msaada huu muhimu kwa wakulima wa embe hapa nchini, ambao utawasaidia sana kuboresha zao hili na pia utakuwa mwanzo wa kupambana na mdudu Nzi.
“Msaada huu mliotupa utakuwa changamoto kubwa kwao kuboresha zao hili kwa manifaa yao na Taifa kwa ujumla” alisisitiza Nsape wakati akitoa shukrani zake kwa serikali kwa niaba ya wanachama wenzake.
Pia Nsape aliitika serikali issiishie hapa bali iweze kuwafikia wakulima wengine wadogo ili kuboresha kilimo cha zao la embe miongoni mwa wakulima hapa nchini.
Naye mtalaamu wa kilimo toka kitengo cha Uthibiti Visumbufu wa Mimea Kibaolojia katika kituo cha Kibaha mkoani Pwani Nsami Elibariki aliwataka wakulima kufuata taratibu za matumizi sahihi ya vifaa hivi ili kuboresha zao la kilimo cha embe.
Chama cha Wakulima wa zao la Embe kilianza mwaka 2001 kwa kuwa wanachama toka mikoa 15 ya hapa nchini kikwa na lengo kuu la kuboresha kilimo cha embe kwa kuwatanisha wakulima wa zao hili kupambana na changamoto ya kilimo cha zao hili.