Skip to main content
News and Events

Mafunzo kuhusu Mtambo wa Kupokelea Mawasiliano

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi Lilian Mapfa jana alifungua rasmi mafunzo ya uelewa kuhusu mtambo wa kupokelea taarifa za hali ya hewa  wa Wizara.

Mafunzo hayo yanaendeshwa na Kitengo cha Mazingira kwa kushirikiana na Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA)
yana lengo la kuongeza uelewa kuhusu masuala ya taarifa za hali ya hewa ambapo Wizara itakuwa na uwezo wa kutoa taarifa sahihi za kiwango cha mvua kwa wakulima wa Tanzania.

Bibi Lilian alisema  lengo la mafunzo hayo yanayofanyika katika Chuo cha Utalii, Tandika ni kuongeza uwezo wa kufuatilia, kujiweka tayari ili kukabiliana na mabadiliko ya kimazingira ikiwemo hifadhi endelevu ya mazingira inayochangia kupunguza umaskini.

Bibi Mapfa aliongeza kuwa mtambo huu utasaidia kufanikisha shughuli za kilimo, utafiti katika kilimo hasa mbegu.

Naye Mkuu wa Kitengo cha Mazingira cha Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Bibi Shekwanande Natai alisema kuwa mafunzo hayo yatasaidia Wataalam wa Wizara kujua namna ya kutumia mtambo huo na faida zake.