Ole Nasha ajivunia kufutwa kwa baadhi ya kodi na tozo katika sekta ndogo ya mazao
Naibu Waziri wa Kilimo Mifugo na Uvuvi, Mhe. Wiliam Tate Ole Nasha (Mb) amesema kuwa kwa muda mrefu serikali imekuwa ikipata malalamiko kutoka kwa Wananchi mbalimbali hususan kwa wakulima nchini Tanzania wakipinga kodi na tozo mbalimbali zinazotozwa kwani zimekuwa zikiwanyonya badala ya kuwakwamua na wimbi kubwa la umasikini.