Serikali Yajipanga Kujenga Kiwada cha Kubagua Korosho
Waziri wa kilimo chakula na ushirika Mh. Chiristopher Chiza amekutana na wawekezaji wa korosho kutoka katika taasisi mbalimbali za Maerekani (AFRICA HARVEST OF HOPE)’kujadili uwezekano wa kujenga kiwanda cha kubangua korosho hapa nchini.
Akizungumza na wawekezaji hao amesema kuwa Serikali ya Tanzania inalikaribisha wazo la kujenga kiwanda cha kubangua korosho kwa lengo la kuongeza ubora wa zao la korosho ili liweze kupata soko zuri hapa nchini na nje ya nchi.
Aidha Mhe. Naibu Waziri alisema kuwa, mkulima anapata hasara kwa kuuza korosho gafi hivyo kumfanya apate hasara na kushindwa kuondokana na umaskini.
Katika uwekezaji huo Naibu waziri amewataka wawekezaji hao kufanya mabo yafuatayo ili kukamilisha tarabu za uwekezaji, kwanza wakitembelee kituo cha uwekezaji (Tanzania Investment Centre), kwa ajili ya kupata mwongozo wa uwekezaji.
Pia wawekezaji hao wawe tayari kuwashirikisha wakulima katika shughuli zao na wawe tayari kuwa na kilimo cha mkataba kitakachomwezesha mkulima kuwa na uhakika wa kipato chake.
Akiongea kwa niaba ya wenzake Bw. Patrick Chiles alisema kuwa, mradi wao ‘AFRICA HARVEST OF HOPE’ unakusudia kwekeza Tanzania katika zao la korosho, baada ya kuona kuwa zao hili linazalishwa Tanzania lakini sehemu kubwa inasindikwa nchini India na kuuzwa nchi zingine, hivyo wameona ni vizuri korosho isindikwe hapa hapa Nchini.
Walitoa ahadi kwamba watafuata taratibu zote za uwekezaji,, kununua korosho nyingi kwa ajili ya kuongeza ajira ya muda mrefu, ambapo wamesma wamesea pia kuwa Taasisi yao haitakuwa ya kutengeneza faida kubwa.