SUMUKUVU; MADHARA NA NAMNA YA KUDHIBITI
SUMUKUVU; MADHARA NA NAMNA YA KUDHIBITI
SUMUKUVU ni kemikali zinazozalishwa na aina za fangasi /ukungu/kuvu wanaoota kwenye punje za nafaka, mbegu za mafuta, mikunde na mazao ya mizizi (Smith et al., 2012)
Mahindi na unga wake na karanga na bidhaa zake huathiriwa zaidi na sumukuvu. Mazao mengine ni korosho, muhogo, alizeti, mtama na mchele.
SUMUKUVU pia hupatikana katika bidhaa za mifugo kama vile mayai, nyama na maziwa iwapo watakula chakula kilichochafuliwa na sumu
Hupatikana katika maziwa ya mama anayenyonyesha iwapo atakula chakula chenye sumu kuvu
Kuna SUMUKUVU za aina nyingi kulingana na kuvu anayezalisha sumu hiyo, mfano kwa mahindi aflatoxin, fumonisins, and ochratoxin ndiyo za muhimu zaidi.
SUMUKUVU hazionekani kwa macho, hazina harufu, ladha wala rangi. Lakini kuvu wanaozalisha sumu kuvu wanaweza kuwa na rangi kama vile kijani, kijivu, njano chafu au machungwa.
*download taarifa hii hapa chini*