Zidikheri Mundeme Ateuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Bwana Zidikheri Mgaya Mundeme kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika.
Bwana Mundeme anachukua nafasi ya Dkt. Yamungu Kayandabila ambaye amekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.
Kabla ya uteuzi huo Bwana Mundeme alikuwa Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
Baada ya kufika Wizarani, Bwana Mundeme alifanya ziara ya kutembelea Idara na Vitengo kwa lengo la kufahamiana na watumishi na shughuli zinazotekelezwa katika maeneo yao ya kazi.
Katika ziara hiyo aliambatana na Eng. Raphael Daluti, Naibu Katibu Mkuu pamoja na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala na Menejimenti ya Rasilimali Watu Bi. Hilda Kinanga.