Wadau wa Kilimo katika mnyororo wa thamani wa tasnia ya Korosho nchini wampongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuinua zao hilo ambalo limekuwa likiendelea kufanya vizuri na kuleta tija kwa wakulima.
Wadau hao wamesema hayo wakati wa Kikao cha Tathmini ya Zao la Korosho kwa msimu wa 2025:2026, tarehe 14 Aprili 2026, ukumbi wa PSSSF Tower, jijini Dodoma.