Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb); amesema kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkutano wa Afrika wa Matumizi Endelevu ya Zana za Kilimo (Africa Conference on Sustainable Agricultural Mechanization – ACSAM) utakaofanyika tarehe 03-06 Februari 2026, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Vyombo vya Habari tarehe 30 Januari 2026, Mhe. Chongolo amesema Mkutano huo utatoa fursa kwa washiriki kubadilishana uzoefu, kuimarisha ushirikiano, na kuharakisha matumizi ya zana na teknolojia za kisasa za kilimo kwa ajili ya mageuzi endelevu ya Sekta ya Kilimo nchini na Barani Afrika kwa ujumla. Mha. Athumani J. Kilundumya, Naibu Katibu Mkuu anayesimamia Umwagiliaji na Zana za Kilimo naye ameshiriki katika mkutano na waandishi wa habari.
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) ameelekeza mambo sita muhimu kuzingatia ili ushirika kuimarika zaidi na kuleta tija kwa wanaushirika.
Akizungumza tarehe 30 Januari 2026 jijini Dodoma wakati akizindua Bodi ya Makamishna wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania (TCDC), Waziri Chongolo amesema Kamisheni ihakikishe inaleta mageuzi ya kidigitali ili takwimu sahihi zipatikane kwenye mizani ya kidigitali na kupunguza udanganyifu kwa wanachama na wakulima.