Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wizara ya Kilimo

Bw. Gerald G. Mweli

Bw. Gerald G. Mweli
Katibu Mkuu

Prof. Peter L. M. Msoffe

Prof. Peter L. M. Msoffe
Naibu Katibu Mkuu (Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula)

Mha. Athumani J. Kilundumya

Mha. Athumani J. Kilundumya
Naibu Katibu Mkuu (Umwagiliaji na Zana za Kilimo)

Slide Photo
Tanzania na Kenya zaahidi kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika Sekta ya Kilimo hususan katika nyanja za kukuza biashara, uwekezaji pamoja na kuimarisha usalama wa chakula ukanda wa Afrika Mashariki. Hayo yamebainishwa wakati wa majadiliano kati ya Bw. Gerald Mweli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo na Mhe. Catherine Wahome, Balozi wa Jamhuri ya Kenya nchini Tanzania tarehe 20 Mei 2026, Mtumba - jijini Dodoma.
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Wadau wanaotekeleza Mradi wa (TANRICE3) wamekutana katika kikao cha sita kujadili taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kutoka kwa wadau pamoja na Vyuo 6 vya Mafunzo ya Kilimo (MATI) vya Ilonga; Mtwara; Igurusi; Kituo cha Mafunzo ya Kilimo Kilimanjaro (KATC); Tumbi; Ukiriguru pamoja na Shule ya Kilimo Zanzibar, kwa lengo la kuwezesha ushiriki wa kutosha katika kutekeleza mradi huo. Kikao hicho kimefanyika tarehe 13 Mei 2026 mkoani Kilimanjaro, na kuhudhuriwa na wawakilishi kutoka Wizara ya Kilimo; Wakala wa Taifa wa Mbegu za Kilimo (ASA); Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC); Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI); Taasisi ya Uthibiti wa Ubora wa Mbegu (TOSCI); Wakufunzi kutoka Vyuo vya Mafunzo ya Kilimo (MATI); Wizara ya Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar; Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar na wawakilishi kutoka Serikali za Mitaa.
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Slide Photo
Wakulima wa zao la Alizeti katika Halmashauri za Wilaya za Ikungi, Itigi, Iramba na Mkalama mkoani Singida wameendelea kunufaika na elimu ya kanuni bora za kilimo cha Alizeti kupitia mashamba darasa yaliyoanzishwa na Mradi wa Kuwezesha Upatikanaji wa Pembejeo za Kilimo Tanzania (TAISP) unaotekelezwa na Wizara ya Kilimo. Zoezi la ufuatiliaji wa mashamba darasa ya Alizeti limefanyika tarehe 12-13 Mei 2026 mkoani Singida katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida na Singida Manispaa kwa lengo la kuhakikisha wakulima wanazingatia kanuni bora za kilimo na kuongeza uzalishaji wa zao la alizeti.
Slide Photo
Taasisi na Bodi za Wizara