Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb) ameshiriki katika Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Kilimo, Ardhi na Maendeleo Vijijini, unaofanyika kuanzia tarehe 24 hadi 28 Februari 2026 mjini Cartegina, nchini Colombia.
Lengo la mkutano ni nchi zinazoshiriki kutoa mapendekezo ya matumizi bora ya ardhi katika kilimo yanaweza kupunguza migogoro ya ardhi na kuharakisha maendeleo vijijini.
Matukio katika picha kati ya Waziri wa Kilimo Mhe. Daniel Chongolo (Mb) na Mhe. Prof. Kitila Alexander Mkumbo (Mb), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji; pamoja na Bw. Gerald Mweli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo baada ya kukaa kikao kazi cha pamoja cha maandalizi ya awali ya Mkutano wa Kikanda wa Sekta ya Mbogamboga na Matunda (Hortilogistica Africa) unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba 2026, mkoani Arusha.