Ujumbe wa Taasisi ya Kimataifa ya Kilimo cha Kitropiki (International Institute of Tropical Agriculture - IITA), umekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe.David Silinde (Mb) tarehe 8 Mei 2026 jijini Dodoma.
Ujumbe huo umeongozwa na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa IITA, Dkt. Tahirou Abdulaye ambaye ameeleza utayari wa IITA kutaka kuendeleza ushirikiano na Wizara ya Kilimo katika kukuza Sekta ya Kilimo. kupitia tafiti; maendeleo ya mazao na vinasaba; mapinduzi ya kidigitali; kujenga uwezo pamoja na kukabiliana na magonjwa mbalimbali ya mazao.
Mazungumzo hayo pia yalimshirikisha Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Mazao, Bi. Yasinta Nzogela, wakiwemo pia wawakilishi wengine kutoka IITA pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo (TARI).
Wizara ya Kilimo kwa kushirikiana na Mwamvuli wa Wadau wa Kilimo Hai Tanzania (TOAM) imekutana na Wizara mtambuka kujadili utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Kilimo Ikolojia Hai (NEOAS) unaolenga kuendeleza kilimo hicho nchini, tarehe 7 Mei 2026, jijini Dodoma.