Serikali ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuanza ujenzi wa bwawa la umwagiliaji katika Kata ya Tingatinga, Wilaya ya Longido, mkoani Arusha, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha Sekta ya Kilimo; na Sekta ya Ufugaji kupitia uhakika wa upatikanaji wa maji.
Amesema Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) ambaye pia ni mlezi wa Mkoa wa Arusha, tarehe 02 Julai 2026 wakati akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Tingatinga, wilayani longido.
Kamati ya Uongozi (Steering Committee) ya Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula Tanzania (Tanzania Food Systems Resilience Program – TFSRP) imekutana jijini Dar es Salaam tarehe 29 Juni 2026 katika mkutano wake wa nne tangu kuanza kwa utekelezaji wa programu hiyo.
Lengo la Mkutano ni kujadili maendeleo yaliyofikiwa, kutathmini utekelezaji na kuweka mikakati ya kuimarisha utekelezaji ili kuhakikisha malengo yaliyowekwa yanafikiwa kwa wakati.