Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb), amekutana kwa mazungumzo na Waziri wa Kilimo na Maendeleo Vijijini wa nchini Romania, Mhe.Florian -Emil Dumitru tarehe 10 Februari 2026.
Viongozi hao wamejadili masuala mbalimbali yanayohusu Sekta ya Kilimo hususan kuimarisha mashirikiano katika masuala ya tafiti za mbegu za kilimo, kilimo cha Ngano, upatikanaji wa mbolea, teknolojia za kilimo cha umwagiliaji na zana za kisasa za kilimo.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb), ameshiriki kikazi katika Mkutano wa Kuhamasisha Sekta Binafsi kwa Biashara Endelevu na Uwekezaji katika Sekta ya Chakula Barani Afrika, jijini Nairobi nchini Kenya.
Mkutano huo umeandaliwa kwa pamoja kati ya Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo (OECD) na Serikali ya Jamhuri ya Kenya na kufunguliwa na Mhe. William Kabogo (Mb), Waziri wa Habari, Mawasiliano na Uchumi wa Kidigiti wa Kenya. Washiriki wengine ni pamoja no Makamu wa Rais Mstaafu wa Nigeria; Mawaziri wa Kilimo kutoka Barani Afrika na nchi ya Romania; wakiwemo wawekezaji kutoka Umoja wa Ulaya.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb), amepokea ujumbe kutoka mashirika ya KUKE na FASPOL ya nchini Poland, ulioongozwa na Bw. Janusz Wladyczak, Rais wa Bodi ya Shirika la Bima ya Mikopo ya Usafirishaji (KUKE), akiambatana na Bw. Marcin Kaleta, Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya FASPOL, tarehe 4 Februari 2026, jijini Dodoma.