Serikali imetenga eneo la ekari 200 mkoani Pwani kwa ajili ya mradi mkubwa wa kilimo cha mazao ya matunda na mbogamboga, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa mazao ya bustani na kufungua fursa za kiuchumi kwa wananchi.
Akiwa katika ziara ya kikazi mkoani humo tarehe 16 Machi 2026, Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) ameeleza kuwa eneo hilo liko katika kijiji cha Ruvu Station, kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Deodatus Mwanyika (Mb), akiwemo Makamu Mwenyekiti Mhe.Mariam Ditopile (Mb) na wajumbe wake walipotembelea mradi wa ukarabati na ujenzi wa Maabara ya mbegu ya Taifa ya Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI), tarehe 15 Machi 2026, Mkoani Morogoro.
Kamati imeipongeza Wizara ya Kilimo na Taasisi yake ya TOSCI kwa kazi nzuri ya ujenzi wa maabara na kusema ni moja ya mradi mzuri wa mfano hususan na hatua ya asilimia 86 ujenzi ulipofikia. “Ongezeni nguvu kwenye kushughulika na mbegu feki na toeni elimu ya kutosha kwa wakulima kuhusu mbegu zilizothibitishwa,” amesisitiza Mwenyekiti Mhe. Mwanyika.