Serikali imepiga marufuku uuzaji wa mazao ya biashara kwa mfumo wa lumbesa na kusisitiza kuwa mazao yote yauzwe kwa kutumia vipimo sahihi vinavyotambuliwa kisheria. Pia watendaji wa Serikali watakiwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kuwasaidia wananchi kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Maelekezo yametolewa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) tarehe 10 Machi 2026, mjini Sumbawanga wakati akihitimisha ziara yake ya kikazi ya siku tatu katika Mkoa wa Rukwa.
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) ametembelea Shamba la Pamoja la Chinangali lililopo wilayani Chamwino mkoani Dodoma tarehe 11 Machi 2026 kwa lengo la kukagua maendeleo ya uzalishaji pamoja na kusikiliza changamoto za vijana na wanawake wanufaika wa Programu ya Building a Better Tomorrow (BBT).