Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Prof. Peter L. M. Msoffe amefanya ziara ya kutembelea shamba la vijana wanaonufaika na Programu ya Jenga Kesho Iliyobora (BBT) tarehe 21 Februari 2026, Chinangali, jijini Dodoma, kwa lengo la kujionea utekelezaji wa programu hiyo na kuzungumza na vijana kuhusu mafanikio na changamoto wanazokutana nazo.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb) ameshiriki katika Mkutano wa hadhara mkoani Kilimanjaro tarehe 20 Februari 2026 na kujibu hoja mbalimbali za Sekta ya Kilimo zilizoibuliwa na wananchi waliojikusanya kufuatia uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa stendi ya Ngangamfumuni.
Mkutano huo wa hadhara ni sehemu ya ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) katika mkoa huo.