Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli, amekutana na ujumbe kutoka Benki ya Kimataifa ya Japan (Sumitomo Mitsui Banking Corporation - SMBC) ulioongozwa na Makamu Mkurugenzi wake, Bw. Taro Otsu, tarehe 12 Juni 2026 katika Ofisi za Wizara ya Kilimo, Mtumba jijini Dodoma.
Benki hiyo ina nia ya kuwezesha upatikanaji wa mitaji kwa ajili ya ununuzi wa matrekta ili kusaidia jitihada za Serikali za kuongeza matumizi ya zana za kisasa za kilimo kwa kufikia lengo la kuwa na matrekta 10,000 ifikapo mwaka 2030.
Kikao hicho kilihudhuriwa na Bi. Ngobile Ngwenya, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Agricom.
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb), amekutana kwa mazungumzo na ujumbe ulioongozwa na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Frontier, Bw. Lars Tushuizen tarehe 11 Juni 2026, jijini Dodoma ambao wana nia ya kuwekeza katika Sekta ya Kilimo.