Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Dkt. Stephen Nindi ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), kuhakikisha sayansi pamoja na tafiti za kilimo zinawafikia wakulima wote nchini ili kuwawezesha kuzitumia tenkolojia hizo kuzalisha kwa tija.
Dkt. Nindi amesema hayo tarehe 3 Desemba, 2025 katika ufunguzi wa Siku ya Udongo Duniani iliofanyika katika viwanja vya Nane Nane vya John Malecela vilivyopo Nzuguni jijini Dodoma, ikiwa na Kauli mbiu “Afya Bora ya Udongo kwa Miji Maridhawa".