Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) amefanya kikao kazi na Wakurugenzi Wakuu na Wenyeviti wa Bodi za Taasisi zilizo chini ya Wizara: Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI); Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB); Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Mbegu Tanzania (TOSCI); na Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC), kujadili utekelezaji wa mikakati mbalimbali waliyojiwekea kwa mwaka wa fedha 2025/2026 pamoja na kuangalia mwelekeo wa mikakati ya mwaka ujao wa fedha 2026/2027.