Mrajis wa Vyama vya Ushirika na Mtendaji Mkuu wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania, Dkt. Benson O. Ndiege akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni ya "Linda Ushirika, Chagua Uadilifu” iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 24 Aprili 2026.
Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb), amesema Serikali iko katika hatua za kupanga kushirikiana na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ili kuanzisha madawati maalum ya kipolisi yatakayoshughulikia masuala ya vyama vya ushirika nchini.
Akizungumza jijini Dodoma tarehe 24 Aprili 2026 wakati wa uzinduzi wa kampeni ya “Linda Ushirika, Chagua Uadilifu”, Mhe. Chongolo amesema kuwa lengo la mpango huo ni kuimarisha uwajibikaji, kudhibiti vitendo vya rushwa na ubadhirifu, pamoja na kuhakikisha wahusika wanachukuliwa hatua za kisheria bila upendeleo.