Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb), amefungua rasmi Kiwanda cha Kuunganisha Matrekta cha TATDC kilichopo Mvomero, mkoani Morogoro tarehe 16 Juni 2026.
Ufunguzi huo umeashiria mikakati ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Mheshmiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, inayolenga kuleta mageuzi makubwa ya kilimo nchini kupitia uwekezaji wa viwanda na teknolojia ya kisasa.