Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule ametoa ekari 100 kwa wadau wa Kilimo Ikolojia Hai kwa ajili ya kuendeleza shughuli za kilimo ikolojia hai hapa nchini na kuahidi Ofisi yake kuendelea kutoa ushirikiano.
Amesema hayo wakati wa hafla maalum ya ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na Taasisi Mwamvuli ya Kilimo Hai Tanzania (TOAM) tarehe 5 Machi 2026, jijini Dodoma. Hafla hiyo ikiwa ni kilele cha Mkutano wa Nne wa wa Kitaifa wa Kilimo Ikolojia Hai (National Ecological Organic Agriculture Strategy - NEOAS) uliofanyika kuanzia tarehe 3-5 Machi 2026, katika Mji wa Serikali Mtumba, Jijini Dodoma.