Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) ameeleza kuwa Tanzania na Italia zimekuwa zikishirikiana kwa miaka mingi katika masuala ya maendeleo ikiwemo Sekta ya Kilimo, ambapo miaka ya 1990 Tanzania ilipokumbwa na janga la ukame nchi ya Italia ilitoa msaada wa chakula kwa Serikali ya Tanzania.
Ameeleza hayo alipokutana kwa mazungumzo na Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mhe. Giuseppe S. Coppola tarehe 17 Machi 2026 jijini Dar es Salaam.