Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb) ametoa rai kwa wakulima wanaojishughulisha na kilimo ikolojia hai kuwa Serikali itaendelea kushirikiana nao ili kufikia malengo ya kilimo endelevu na kuwa na utoshelevu wa chakula kwa kuzingatia utunzaji wa mazingira.
Naibu Waziri Silinde amesema hayo wakati akimwakilisha Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) kwenye Mkutano wa Nne wa wa Kitaifa wa Kilimo Ikolojia Hai (National Ecological Organic Agriculture Strategy - NEOAS), tarehe 3 Machi 2026, jijini Dodoma.