Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb), amefungua rasmi Kiwanda cha Kuunganisha Matrekta cha TATDC kilichopo Mvomero, mkoani Morogoro tarehe 16 Juni 2026.
Serikali ipo katika hatua za mwisho za maandalizi ya kuanza ujenzi wa bwawa la umwagiliaji katika Kata ya Tingatinga, Wilaya ya Longido, mkoani Arusha, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha Sekta ya Kilimo; na Sekta ya Ufugaji kupitia uhakika wa upatikanaji wa maji.
Amesema Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) ambaye pia ni mlezi wa Mkoa wa Arusha, tarehe 02 Julai 2026 wakati akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuzungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Tingatinga, wilayani longido.