Miradi yote inayotekelezwa chini ya Wizara ya Kilimo imeelekezwa kuzingatia kikamilifu sheria, taratibu na kanuni za Serikali ili kuongeza ufanisi na kuhakikisha thamani halisi ya fedha inapatikana katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Ameelekeza hayo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Umwagiliaji na Zana za Kilimo, Mha. Athumani Kilundumya wakati akifunga rasmi mafunzo ya siku kumi na tano (15) kuhusu Usimamizi wa Miradi na Mikataba yaliyotolewa kwa Wahandisi wa Wizara ya Kilimo na Taasisi zake, tarehe 6 Machi 2026, Viwanja vya Nzuguni, Nanenane jijini Dodoma.