Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. David Silinde (Mb), amepokea ujumbe kutoka mashirika ya KUKE na FASPOL ya nchini Poland, ulioongozwa na Bw. Janusz Wladyczak, Rais wa Bodi ya Shirika la Bima ya Mikopo ya Usafirishaji (KUKE), akiambatana na Bw. Marcin Kaleta, Rais na Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya FASPOL, tarehe 4 Februari 2026, jijini Dodoma.
Mhe. Daniel G. Chongolo (Mb.), Waziri wa Kilimo amefanya kikao na Bw. Ernest Ruzindaza, Mratibu Msimamizi wa Programu ya Mifumo Himilivu ya Chakula (TFSRP) na Mchumi Mkuu kutoka Benki ya Dunia ambayo ni programu iliyo chini ya Wizara ya Kilimo.
Kikao hicho kimefanyika pembezoni mwa Mkutano wa Afrika kuhusu Matumizi Endelevu ya Zana za Kilimo (Africa Conference on Sustainable Agricultural Mechanization – ACSAM) unaofanyika kuanzia tarehe 3-6 Februari 2026.