Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) imepongezwa kwa kazi nzuri ya kuleta mageuzi katika tafiti za mbegu nchini na kukabidhiwa pikipiki 71 zitakazoleta tija zaidi kwa watafiti.
Amesema hayo Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) tarehe 23 Aprili 2026 jijini Dodoma na kuongeza kuwa pikipiki hizo zitaleta mapinduzi makubwa katika utendaji kazi wa watumishi wa TARI katika vituo vyote vya utafiti na mashamba ya majaribio.