Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Bw. Gerald Mweli, amekutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Wakala wa Maendeleo wa Ufaransa (L' Agence Française de Développement - AFD), tarehe 25 Machi 2026, jijini Dodoma. AFD inajishughulisha na utoaji wa mikopo kwenye Sekta mbalimbali ikiwemo ya Kilimo kwa kuzingatia mazingira endelevu ili kuondoa njaa, umaskini na kuwa na usalama wa chakula kwa wakulima wadogo na lishe.
Uongozi huo umeongozwa na Bi. Celine Robert, Mkurugenzi Mkazi na Bi. Marion Vigneau, Afisa Mradi, Kilimo, Mazingira na Viumbe Hai wa AFD.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli ametoa wito kwa wadau wa Sekta ya Umma na Sekta Binafsi kuwasilisha maoni, fursa au changamoto zozote kwa kuwa milango ya Wizara hiyo iko wazi kuyapokea na kuyatatua ili kuzidi kuimarisha Sekta ya Kilimo nchini.
Amesema hayo wakati wa Kikao cha Kikundi Kazi cha Tatu cha Kilimo cha Baraza la Taifa la Biashara (TNBC), tarehe 25 Machi 2026, jijini Dodoma.