Wizara ya Kilimo imetoa elimu ya mwongozo wa matumizi ya ghala za umma katika mikoa ya Kigoma, Katavi, Rukwa, Songwe na Mbeya tarehe 11 hadi 24 Mei 2026 kwa lengo la kuwajengea wakulima na wadau wa sekta ya kilimo uelewa kuhusu matumizi sahihi ya ghala za umma ili kuhakikisha mazao yanahifadhiwa kwa usalama na ubora unaotakiwa.
Tanzania na Kenya zaahidi kuimarisha ushirikiano wa kimkakati katika Sekta ya Kilimo hususan katika nyanja za kukuza biashara, uwekezaji pamoja na kuimarisha usalama wa chakula ukanda wa Afrika Mashariki.
Hayo yamebainishwa wakati wa majadiliano kati ya Bw. Gerald Mweli, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo na Mhe. Catherine Wahome, Balozi wa Jamhuri ya Kenya nchini Tanzania tarehe 20 Mei 2026,
Mtumba - jijini Dodoma.