Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli akiongea mbele ya mamia ya washiriki wakati wa uzinduzi wa usajili wa Jukwaa la Hotikacha la Kimataifa (HortiLogistica Africa 2026) tarehe 22 April 2026.
Uzinduzi wa usajili ulizinduliwa rasmi na Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo Jukwaa husika linatarajiwa kufanyika tarehe 8 hadi 10 Novemba 2026, jijini Arusha.
HortiLogistica Africa 2026 itahusisha wazalishaji hapa nchini na kufungua fursa za kibiashara, uwekezaji na masoko kwa wakulima.