Rais wa Jamhuri ya Shirikisho la Ujerumani, Mhe. Frank-Walter Steinmeier amefungua rasmi Maonesho ya Kimataifa ya Wiki ya Kijani (Green Week) ambayo kwa mwaka huu yametimiza miaka 100 tangu kuanzishwa kwake katika mji wa Berlin mwaka 1926 nchini Ujerumani.
Maonesho hayo yana kauli mbiu ya “Water. Harvests. Our Future” yanashabihiana na Maonesho ya Wakulima ya Kitaifa na Kimataifa ya Nane Nane yanayofanyika chini Tanzania kila mwaka katika wiki ya kwanza ya mwezi Agosti.