Wakulima wa Idofi, Wilaya ya Makambako wameishukuru Serikali kufuatia kusogezewa mradi mkubwa wa umwagiliaji unaotekelezwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NiRC) utakaonufaisha ekari zaidi ya 1.300. Kwa mujibu wa tathmini ya awali ya wataalamu, mradi huo utahusisha ujenzi wa bwawa la umwagiliaji na uwekaji wa miundombinu ya kisasa itakayowezesha uzalishaji wa mazao mwaka mzima.
Wamesema hayo wakati wa mkutano wa hadhara wa Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) katika viwanja vya shule ya Msingi ya Idofi ambapo amewaelekeza kuwa mradi huo wa ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji katika skimu ya Idofi, utawezesha kilimo chenye tija na kufungua fursa mbalimbali za maendeleo katika eneo hilo.
Wizara ya Kilimo imesema mafanikio makubwa yaliyopatikana katika tasnia ya mpunga nchini yametokana na uwekezaji wa kimkakati uliotekelezwa na Serikali, hatua iliyochangia kuimarika kwa usalama wa chakula, kuongezeka kwa ajira na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kitaifa wa Wadau wa Zao la Mpunga uliofanyika Machi 30, 2026 mkoani Morogoro, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Prof. Peter L. M. Msoffe, amesema nchi imeendelea kushuhudia mageuzi makubwa kwenye kilimo kutokana na uwekezaji wa kuimarisha tasnia ya zao la mpunga.