Wizara ya Kilimo imesema mafanikio makubwa yaliyopatikana katika tasnia ya mpunga nchini yametokana na uwekezaji wa kimkakati uliotekelezwa na Serikali, hatua iliyochangia kuimarika kwa usalama wa chakula, kuongezeka kwa ajira na kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kitaifa wa Wadau wa Zao la Mpunga uliofanyika Machi 30, 2026 mkoani Morogoro, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Prof. Peter L. M. Msoffe, amesema nchi imeendelea kushuhudia mageuzi makubwa kwenye kilimo kutokana na uwekezaji wa kuimarisha tasnia ya zao la mpunga.