Serikali imelenga kuongeza uzalishaji na usafirishaji wa mazao katika Sekta za Kilimo, Mifugo na Uvuvi ili kuongeza thamani na kuvutia uwekezaji wa Sekta Binafsi katika kuongeza kipato cha wakulima, wafugaji na wavuvi.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Uendelezaji na Ukuzaji wa Shoroba za Kilimo, Mifugo, na Uvuvi uliofanyika tarehe 20 Februari 2026, mkoani Mtwara, Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Zainab Rajab amesema mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma ina fursa kubwa za kimkakati katika utekelezaji wa shoroba za kilimo, mifugo na uvuvi kutokana na rasilimali ardhi na bahari pamoja na maziwa katika mikoa hiyo.