Skip to main content
Habari na Matukio

KATIBU MKUU MWELI AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA WIZARA

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli amewakumbusha watumishi wa Wizara hiyo  kufanya kazi kwa ushirikiano, bidi na ufanisi ili kuleta tija katika Sekta ya Kilimo.

Katibu Mkuu Mweli ameyasema hayo katika mkutano wa Watumishi wa Wizara ya Kilimo uliofanyika jijini Dodoma tarehe 22 Februari jijini Dodoma.

Katika mkutano huo watumishi walipokea  mawasilisho mbalimbali ya programu na miradi  inayotekelezwa na ya Wizara Kilimo.

AIha Watumishi hao waliweza kupata mafunzu yanayohusu afya zao ikiwa  ni pamoja na elimu ya kujilinda dhidi ya  Virusi vya UKIMWI, Kifua Kikuu  pamoja na  na magonjwa  yasiyoambukiza.

Katika kikao hicho Katibu Mkuu Mweli alisikiliza michango na maoni mbalimbali ya Watumishi  na kutolea ufafanuzi na maelekezo ya  utekelezaji wake kupitia Wakurugenzi na Wakuu  Vitengo  vilivyo chini ya Wizara ya Kilimo.

Mawasilisho yaliyowasilishwa ni ya utekelezaji wa Mradi wa Kusaidia Pembejeo za Kilimo Tanzania (TAISP),  Programu ya kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP); Programu ya Building a Better Tomorrow (BBT); na Programu ya Uvumilivu wa Mifumo ya Chakula Tanzania (TFSRP).